Bush Dokta
JF-Expert Member
- Apr 11, 2023
- 36,228
- 60,546
Katika Bandika bandua inayoendelea chini ya Kiongozi Mahiei Mh John Heche ambaye ni Makamu mwenyekiti wa Chadema Taifa huko Kahama.
Zaidi ya Wananchi 5000 ktk mkutano mmoja wamekubali kwa kauli moja na kuitaka serikali ijali maoni na matakwa yao.
Wamesema wanaiomba mamlaka kusikiliza wananchi ili uchaguzi wa Oktoba usogezwe na marekebisho ya sheria na katiba yafanyike.
Ikumbukwe Kitendawili kikubwa kwa serikali ilikuwa ni kupata muda wa kuweza kushughulikia malalamiko ya wadau wakiwemo wananchi ktk swala la demokrasia na uongozi.
Awali serikali na chama cha ccm kilikubali kuwa hoja za mageuzi ni muhimu na kwamba kwa upande wao wanaziunga mkono na hivyo wako tayari kutekeleza. Pamoja na utayari huo walitoa sababu kuwa kwa sasa haiwezekani kwa kuwa muda ni mchache tunapoelekea uchaguzi Mkuu wa oktoba 2025.
Hata hivyo baada ya kushiriki majadilianao mbali mbali kwa wadau wa Maswala ya Sheria, Katiba, Chaguzi za kidemokrasia wadau wa haki za binadamu na wa maendeleo wengi wamekuja na suluhu kuwa Kuna uwezekano wa kusogeza uchaguzi mbele.
Wakasema hili litampa Muda Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Samia Suluhu Hassan aliyeko madarakani pamoja na vyombo vingine kujipanga na kutuletea mifumo bora ya utawala.
Huko Kahama kwa Mkutano wa leo Wananchi wameonesha kuunga mkono hoja hiyo kwa 100%.
No reform no election
View: https://www.youtube.com/live/78R43Ag8GaA?si=fX6J3i3Tncf6VC_r
Zaidi ya Wananchi 5000 ktk mkutano mmoja wamekubali kwa kauli moja na kuitaka serikali ijali maoni na matakwa yao.
Wamesema wanaiomba mamlaka kusikiliza wananchi ili uchaguzi wa Oktoba usogezwe na marekebisho ya sheria na katiba yafanyike.
Ikumbukwe Kitendawili kikubwa kwa serikali ilikuwa ni kupata muda wa kuweza kushughulikia malalamiko ya wadau wakiwemo wananchi ktk swala la demokrasia na uongozi.
Awali serikali na chama cha ccm kilikubali kuwa hoja za mageuzi ni muhimu na kwamba kwa upande wao wanaziunga mkono na hivyo wako tayari kutekeleza. Pamoja na utayari huo walitoa sababu kuwa kwa sasa haiwezekani kwa kuwa muda ni mchache tunapoelekea uchaguzi Mkuu wa oktoba 2025.
Hata hivyo baada ya kushiriki majadilianao mbali mbali kwa wadau wa Maswala ya Sheria, Katiba, Chaguzi za kidemokrasia wadau wa haki za binadamu na wa maendeleo wengi wamekuja na suluhu kuwa Kuna uwezekano wa kusogeza uchaguzi mbele.
Wakasema hili litampa Muda Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Samia Suluhu Hassan aliyeko madarakani pamoja na vyombo vingine kujipanga na kutuletea mifumo bora ya utawala.
Huko Kahama kwa Mkutano wa leo Wananchi wameonesha kuunga mkono hoja hiyo kwa 100%.
No reform no election
View: https://www.youtube.com/live/78R43Ag8GaA?si=fX6J3i3Tncf6VC_r
