Maelezo kutoka kwa Katibu Mkuu Utumishi

Kasomi

JF-Expert Member
Sep 3, 2014
11,036
20,337
MAELEZO KUTOKA KWA KATIBU MKUU UTUMISHI.

1. Malimbikizo ya salary, yatalipwa automatic baada ya areas kuwa approved na maafisa utumishi, kuanzia pale ulipopanda. Hakuna tena kudai area

2. Uhamisho, kuhamisha mshahara ni jukumu la mwajiri wa awali, kama umehama

3. Kuhama mkoa ni lazima jina litokee kwenye orodha ya watumishi wanaohama.

4. Kwa wastaafu wanaodai areas, wanatakiwa kujaza fomu na viambatanishi ili ulipwe nje y

5.Malimbikizo ya mshahara kuonekana kisha kufutika, haijapotea ila inahitaji kuidhinishwa upya.

6.Kama hujapata areas, na madai ni ya muda mrefu fuatilia kwa afisa utumishi ili ujaze form maalum.

7. Ukipanda cheo, kiri haraka.

8.Posho za safari za kikazi zinatokana na status ya mtumishi, upandishaji wa vyeo vya watumishi hutegemea vikao vya DED, upandaji cheo inategemea fungu lililopangwa, mtumishi haruhusiwi kudai cheo. Hii ni kanuni. Promotion ni motisha kwa watumishi, si automatic. Mwajiri lzm apate taarifa za utendajikazi wa utumishi ndipo aandae promotion.

9.Madai kwa watumishi waliohama, yatashughulikiwa na mwajiri wa sasa baada ya kuwasiliana na mwajiri wa awali.

10. Upatikaji wa nyaraka www. Tanzania. Go. Tz, www. Utumishi. go. Tz na www. Tamisemi. Go. Tz, utapata nyaraka na huduma kwa kutumia simu au computer.

11. Nauli za likizo, inategemea bajeti ya halmashauri, ilipwe kabla ya kusafiri, akijisafirisha atadai. Maombi ya nauli za likizo yatahakikiwa kwa kutumia nauli za SUMATRA. Marufuku kulipwa nusu nauli.

12. Kusoma nje ya nchi, kama upo kwenye mpango wa mwajiri utalipiwa na kulipwa mshahara, kama haupo mwenye mpango, utachukua likizo bila malipo. Kibali kitatolewa na katibu mkuu kusafiri nje.

13. Rufaa ya matibabu, mwajiri alipe nauli na posho ya kujikimu. Ukijigharamia, mwajiri anatakiwa kukulipa.

14. Kutofautiana kwa mishahara kwa watumishi wenye sifa zinazofanana, kuna tume ya job evaluation inafanya utafiti hatua za mwisho, pia tatizo lilikuwa tsd kutoshirikiana na mkurugenzi. Lkn tsd imekuwa tsc, tatizo litakwisha.

15. Disturbance allowance italipwa kwa 10% ya mshahara wake wa mwaka. Kwa watumishi waliohama destination, hata kama ni ndani ya km5.

16. Tumekumbushwa kutunza nyaraka, kufuatilia mifuko ya jamii na michango ili kuhakiki uwasilishaji wa michango kabla ya kustaafu

17.Uteuzi wa wakuu wa idara huzingatia: utendaji kazi, uongozi, royality, elimu, nk.

18. Tange kwa kila kada ijazwe na kuwasilishwa kwa afisa utumishi.

19. Waliocheleweshwa kupanda daraja, wanatakiwa kwenda kwa afisa utumishi ili ajenge hoja ya kupanda kwa mseleleko na kuomba kibali kwa katibu mkuu.

20. Kama uliwekwa kwenye mpango wa mafunzo halafu ukajipia, mwajiri anatakiwa akurudishie gharama alizotakiwa kukulipia.

21. Punguzo la kodi ya mshahara 9% linahusu wenye mishahara ya chini. Yeye katibu mkuu anakatwa 30% ya mshahara.

22.May 2016 promotion zilisitishwa pamoja na mishahara ilisitishwa kwa ajili ya watumishi hewa. Vyeo vyao vipo, ila marekebisho yao yamesitishwa. Watarejeshwa ktk vyeo vyao vipya soon.

23. Uhakiki bado serikali kuu.

24.Vyeo vya kielimu ktk nchi kimuundo ni mpaka 1st degree. Masters, phd ni mbwembwe

25. Mishahara ya watumishi italingana na uzito wa kazi, miundo ya utumishi kurekebishwa ili watu wasifike bar/vidato vya mshahara.

26. Madeni yaliyokataliwa, yafuatiliwe ili kama ni tatizo la document, zitafutwe na kuprossess upya deni.

27. Walimu wa sayansi wanaofundisha na kufanya laboratory technicians wapewe allowances. Wataalam wa laboratory wanaandaliwa.

28. Kukaimu madaraka mwisho miezi 6, athibitishwe au asitishwe.
 
Nimesoma Na. 17. Pita sifa za uteuzi wa mkuu wa idara ya sekondari, Halmashauri ya meru, Arusha Tanzania. Utagundua tamisemi kuna tatizo kubwa kwenye uteuzi.
 
Kipengele no. 28. Wakurugenzi wa Halmashauri za wilaya na mji kuna watu wamekaimu sasa ni miaka. Miwili
 
Yametamkwa lin haya mkuu maana hapo kwenye arrears kuna wadau wanadai mwaka wa tatu huu na waliambiwa hivyo kuwa pesa zitalipw automatically
Inaonesha mam SSH yupo serious hii itaongeza Morales kwa watumish
 
24.Vyeo vya kielimu ktk nchi kimuundo ni mpaka 1st degree. Masters, phd ni mbwembwe
Hii hai'apply pote; kuna taasisi maslahi yake yanaendana na kiwango cha elimu cha mtumishi hasa taasisi za elimu ya juu; taasisi za utafiti n.k
Lakini pia hayo maelezo mbona kama yamebase zaidi TAMISEMI then kwa watumishi wa kada ya ualimu zaidi; TSD ni nini?!
 
Nilivyoona neno DED na halmashauri tu nimeacha kusoma, hayanihusu.
Walimu na watendaji wa mitaa, kata na manesi wa huko halmashauri ndio wahusika. Mimi wa shirika la umma sihusiki
 
Nilivyoona neno DED na halmashauri tu nimeacha kusoma, hayanihusu.
Walimu na watendaji wa mitaa, kata na manesi wa huko halmashauri ndio wahusika. Mimi wa shirika la umma sihusiki
🤣🤣🤣Sawa mkuu
 
Back
Top Bottom