Madudu ya Morogoro Paralegal yasiachwe yaendelee

Madudu ya Morogoro Paralegal yasiachwe yaendelee

Status
Not open for further replies.

Inkognito

Member
Joined
Feb 13, 2011
Posts
86
Reaction score
108
Morogoro Paralegal ni Kituo cha Wasaidizi wa kisheria kinachofanya kazi zake Mkoani Morogoro.Kituo hicho ambacho kilianzishwa mwaka 1993 na wanachama wapatao 8. Tangu kuanzishwa kwa kituo hicho mwaka 1993 mpaka hivi sasa bado kipo katika ofisi ya kupanga licha ya kupokea misaada na ufadhili kwa ajili ya kufanikisha malengo yake.Pamoja na ukweli kuwa kituo hicho kimekuwa kikipata ufadhaili kutoka kwa mashirika mbalimbali ikiwemo shirika la Foundation for Civil Society pamoja na mashirika mengine lakini uchunguzi uliofanywa na baadhi ya watafiti wa masuala ya uendeshaji wa taasisi zisizo za kiserikali wameweza kubaini mambo yafuatayo ambayo wafadhili na mashirika yanayotoa fedha kwa kituo hicho hawaujui ukweli wake.

Licha ya taarifa juu ya madudu hayo kuwafikia watu wenye dhamana hiyo ikiwemo msajili wa NGO na wafadhili pamoja na wadau mbalimbali, taarifa hizo zimekuwa zikifichwa kutokana na ukweli kuw mkurugenz wa kituo hicho ana uhusiano wa kifamilia na mtu mmoja nyeti aliyeko Ikulu (nitamtaja baadae).


Morogoro Paralegal imekuwa ikitumiwa na viongozi walio katika sehemu nyeti za serikali kama sehemu ya kupiga dili za fedha za miradi.

Baadhi ya Madudu hayo ni haya yafuatayo:
1. Mkurugenzi wa kituo hicho Bi. Flora Masoy amekuwa akishikilia nafasi hiyo ya ukurugenzi tangu mwaka 1993 mpaka leo na hakuna uchaguzi wowote uliowahi kufanyika kwa ajili ya kumchagua tena kushika nafasi hiyo au kumchagua mtu mwingine kuendesha shirika hilo licha ya kuwepo kwa wanachama-wakiwemo wanachama waanzilishi wa kituo hicho.

2. Mkurugenz wa kituo hicho amekigeuza kituo hicho kuwa mali ya wanafamilia kinyume na taratibu na masharti ya NGO. Katika kudhihilisha kuwa kituo hicho ni mali rasmi ya familia, Bi. Flora Masoy amemwajiri mtoto wake wa kiume ajulikanaye kwa jina la Bob kuwa dereva wa gari la kituo pasipo kufuata taratibu za ajira na masharti ya wafadhili katika kutangaza nafasi hiyo ili watu wawasilishe maombi.

3. Fedha nyingi zinazokuja kwa ajili ya kusaidia miradi ya kijamii zimekuwa zikitumika kwa manufaa ya familia badala ya kituo. Mkurugenz wa kituo hicho Bi. Flora Masoy amekuwa akimtumia Mhasibu Binti kijana aitwaye Regina Solomon katika kufoji nyaraka mbalimbali ikiwemo risiti za manunuzi, usafiri, malazi nk (Vielelezo Vipi na wahusika wapo tayari kutoa ushahidi) ili kuhalalisha WIZI unaofanywa na Mkurugenz huyo. Watu kadhaa waliowahi kufanyakazi katika kituo hicho (wakiwemo maafisa miradi) wana ushahidi wa kutosha na wapo tayari kutoa ushirikiano katika kuthibitisha ukweli wa maelezo haya.

4.Mkurugenz wa kituo hicho Bi. Flora Masoy amekuwa akihodhi nafasi zote za kiofisi kwa mfano. Hakuna mtu anayekaimu nafasi yake anapokuwa safarini. Kila kitu huwa kinasimama mpaka atakaporudi yeye mwenyewe. Wahusika wengi katika kituo hicho hawajui majukumu yao hata kama ni maafisa miradi.Licha ya ukweli kwamba katiba ya kituo hicho inaunda idara mbalimbali lakini idara hizo kwa zaidi ya miaka 15 sasa hazijawahi kuwa na wahusika wala kufanya kazi yoyote. Kwa watakaofuatilia na kuzifanyia kazi taarifa hizi nitaomba watakapofikika katika ofisi hizo waombe nakala ya katiba ya kituo, majina ya wahusika na nafasi zao ndani ya kituo hicho,uchunguzi wao uanze kwa kuhoji wajumbe watakaowakuta kabla ya kumhoji Mama Masoy, wanaweza kushangaa mpaka wakome.

5. Wanachma waanzilishi wa kituo hicho wengi wao wameamua kujitoa. Mfano mzuri ni Mama Ashton Balaigwa, Bertha Mdundu na wengineo ambao waliamua kujiondoa baada ya kutoridhishwa na uongozi wa mama Masoy.taarifa za uchunguzi zinadai kuwa hata vijana wanasheria waliojitolea kusaidia kituo hicho waliamua kuondoka bila kuaga kutokana na madudu ya Bi. Flora Masoy.

6.Mkurugenz wa kituo cha Morogoro Paralegal amekuwa akitumia vifaa vya kiofisi kwa manufaa yake na familia yake kwa mfano. Ipo gari aina ya hiace ambayo ilinunuliwa kupitia mradi wa Mama Ardhi, mradi uliofadhiliwa na shirika la ActionAid Tanzania. Gari hilo baada ya kumalizika kwa mradi sasa hivi linafanya biashara ya kubeba wanafunzi na kukodiwa lakini fedha za gari hilo huashiwa kwenye familia ya Mkurugenz wa kituo.

7. Hivi karibuni, nimepata taarifa nyeti kuwa Shirika hilo limepewa fedha za mradi kutoka mfuko wa legal Sector kwa ajili ya kuhamasisha upatikanaji wa haki maeneo ya vijijini. katika hatua za awali tu, tayari fedha hizo zimeshaanza kuliwa huku Bi. Flor Masoy akijigeuza kuwa ndiye afisa wa mradi akishirikiana na Askari Magereza mmoja itwaye Msumba Lisungu. Ningependa Wahusika wa LSF waanze kufuatilia taarifa hizi kwa ukaribu kabla fedha hazijapotea mikononi mwa Mama Masoy. Kinchofanyika katika miradi yote ikiwemo huu wa LSF ni usanii mtupu, tafadhalini fuatilieni taarifa hizi mtagundua ukweli ulivyo.

8. Upo Mradi mwingine ambao shirika hilo limepata fedha kutoka Oxfarm na shirika lingine kwa ajili ya kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika mabaraza ya katiba mpya. Taarifa zilizopo ni kwamba hakuna cha maana kinachofanyika zaidi ya usanii kwakuwa shughuli inayofanywa katika uhamasishaji huo ni sawa na kazi ya tume ya katiba kwani badala ya shirika kuwafunuliwa mwanga washiriki wa mradi kwa kuwafundisha na kuwaelezea changamoto zilizopo katika rasimu ya katiba mpya hususan masuala ya wanawake, Bi. Flora Masoy na timu yake ya watu wachache wasio na uzoefu wa kusimamia miradi wamekuwa wakiwagawa washiriki katika makundi na kuwaomba wajadili rasimu kisha wawakilishe walichojadili. Baada ya kumaliza kufanya hivyo hukusanya makaratasi waliyowakilishi washiriki, na kuwasainisha shs.10,000 kila mmoja kisha hurudi zao mjini kugawana fedha.

8.Kitu cha Morogoro Paralegal kimekuwa ni sehemu ya kupiga dili za wakubwa kutoka kwenye mashirika yanayotoa ruzuku ambao baadae huchukua asilimia zao baad ya kituo kupokea fedha hizo. Mimi,Shirika la Foundation for Civil Society limesha washtukia Morogoro Paralegal kwakuwa wameshagundua madudu ya Bi. Flora Masoy na mpaka hivi leo Foundation for Civil Society kwa takriban miezi nane sasa halijatoa fedha ya utekelezaji wa mradi

9.Morogoro Paralegal, licha ya kuwa na muda mrefu tangu kuanzishwa kwake,licha ya kupata ruzuku na support kwa ajili ya kununua kiwanja chake kwa ajili ya shughuli za ofisi lakini mpaka sasa kituo hicho bado kimepanga ndani ya Majengo ya New Savoy Hotel. Taarifa zilizopo ni kwamba wafadhili, wamewahi kutoa kiasi kisichopungua milioni 11 kwa ajili ya kituo hicho kununua kiwanja kwa ajili ya ofisi miaka saba iliyopita lakini fedha hiyo ilishaliwa zamani.

10.Bi. Flora Masoy amekuwa akiwachukia wanasheria na hata maafisa mradi wenye moyo wa kufanya kazi zao kwa mujibu wa taaluma zao na taratibu za mradi husika.Anachotaka yeye ni kuendesha mradi husika kwa maslahi yake kwanza


swali kubwa wanalopaswa kujiuliza wadau wa maendeleo ni hili, nini Mchango wa Morogoro Paralegal katika kusaidia Wananchi Morogoro ukilinganisha na ruzuku inazopata kutoka kwa wafadhili?ukiachilia mbali mradi wa Mama Ardhi ambao umeacha alama nzuri ya ujenzi wa masjala za ardhi huko vijijini, mradi ambao inasemekana mafanikio yake yalitokana na juhudi binafsi, taaluma na uvumilivu wa mwanasheria kijana Mwaipaja ambaye naye inasemekana aliondoka katika kituo hicho kutokana na Madudu ya Bi. Flora Masoy

Pamoja na haya niliyoyaandika,naowamba wadau mnaohusika muweze kuzifuatilia taarifa hizi ili uwe mwanzo mzuri wa uutendaji hasa wa mashirika yasiyo ya kiserikali yanayotafuna fedha za wafadhili badala ya kusaidia wananchi kama ilivyokusudiwa. kwa watakaohiitaji kuwasiliana na Mama Masoy juu ya Tuhuma hizi wanaweza kumpata kwa namba yake ya 0655477928

11.Niandikapo ujumbe huu, nina vielelezo vya kutosha kuthibitisha WIZI,USANII NA KILA AINA YA MADUDU yanayofaywa na kituo cha Morogoro Paralegal katika kutafuta fedha zinazotoka kwa wafadhili.kwa wenye taarifa nyingine za ziada azimwage humu ili wadau wengine wapate picha kamili ya badhi ya mashirika yanayoendeshwa kimagumashi

12. Morogoro Paralegal haijawahi kuitisha mkutano mkuu wa mwaka kwa kufuata taratibu za NGO. wajumbe waliobaki wengi wao hutumika kama rubber stamp tu za kupitisha agenda za Mama Masoy

13. Morogoro Paralegal haijawahi kupeleka taarifa zake za kila mwaka kwa Msajili wa NGO kama inavyotakiwa. Wanachama wake hawajui mapato wala matumizi ya kituo hicho yakoje
 
-Kama vipi mplekee Said Mwema faili you know, ni kamanda wa ukwee ataliza mambo
 
Hata PCCB wanatosha, ninachojua hizi Nothing Going On (NGO) ni kama mtandao mwingine wa ufisadi tu hapa nchoni, japo wanasema ya wenzao ya kwao hawayaoni, na mbaya zaidi mtandao huu umezama hadi kwa mashirika hisani yenyewe, kwani nao hudai cha juu, tatzo kubwa hakuna udhibiti wa kutosha kwa mashirika haya, mfano mdogo yamekuwa yakifanya PETS wakati yenyewe hayana accountability mechanism ya kuweka wazi mapato na matumizi yao kama sheria inavyoyataka ila wao ni wepesi wa kusonda kidole kwa Serikali.........
 
I know in and out kuhusu hiyo NGO, actually I have seen it toka inaanza, huyo mama kaitoa mbali kwa mahangaiko mengi. Anzisha na wewe NGO yako uone mziki ulivyo mzito hadi kufikia kupata wahisani. Then wahisani wapatikane fungu la kumi litake liwa na watu wengine...
 
Mods msiondoe huu uzi hizo taarifa zina ukweli ndani yake wahusika ebu fatilieni epa nyingine hyo hili huyo mama flora na mafisadi wanaokula nae wafikishe mahakamani,mkuu big up kwa kuibua madudu uzalendo kwanza.
 
I know in and out kuhusu hiyo NGO, actually I have seen it toka inaanza, huyo mama kaitoa mbali kwa mahangaiko mengi. Anzisha na wewe NGO yako uone mziki ulivyo mzito hadi kufikia kupata wahisani. Then wahisani wapatikane fungu la kumi litake liwa na watu wengine...

Acha ukenge wewe kwani lengo la kuanzisha hyo NGO ni kula fedha? Au wahisani wanatoa fedha kwa ajili ya huyo mama ili azile yeye na familia yake? Jipange nyie ndio mnaorodisha taifa nyuma kwani ndio mnaonufaika na ufisadi serikalini na kwenye hayo ma NGO.
 
Acha ukenge wewe kwani lengo la kuanzisha hyo NGO ni kula fedha? Au wahisani wanatoa fedha kwa ajili ya huyo mama ili azile yeye na familia yake? Jipange nyie ndio mnaorodisha taifa nyuma kwani ndio mnaonufaika na ufisadi serikalini na kwenye hayo ma NGO.

mleta mada ana lake jambo, kwa mtu ambaye hauijui na jinsi post ilivyoandikwa unaweza sema kuna watu wananufaika kupindukia hata issue ipewe national audiance. sikatai uwepo wa NGO mismanagement, ila si kwa kiasi ambacho mleta habari kakitoa, this is just like character assacination, na kwenye hilo mleta mada kafanikiwa.
 
MAJUNGU! MAJUNGU! MAJUNGU! MAJUNGUUUUU!!! Imejidhirisha wewe ni mbumbumbu wa maswala ya NGOs. Wapi ulishasikia ED anapatikana kwa kupigiwa kura? Jitahidi uipate katiba yao uisome vizuri ndo uje hapa na hizo tuhuma kuliko kupost vitu utafikri umekoswakoswa kukamatwa ugoni! Ila Wajita kwa majungu hamjambo! Hata mimi niliwahi kufanya kazi na Mjita wa design yako akawa anaandika taarifa za majungu kama zako anazipeleka -----KUU na kwa DSO lakini kesho yake anazikuta ofisini kwangu!! Ilibidi awe mdogo kama piriton! Sasa na wewe umekuja na majungu lukuki. Unajua ni jinsi gani huyo mama alivyoteseka kuanzisha hiyo NGO? Au anavyoteseka kutafuta wafadhili? Unadai hajapeleka taarifa kwa msajili? Wewe unafanya kazi huko? Acha fitina wewe!
 
mleta mada ana lake jambo, kwa mtu ambaye hauijui na jinsi post ilivyoandikwa unaweza sema kuna watu wananufaika kupindukia hata issue ipewe national audiance. sikatai uwepo wa NGO mismanagement, ila si kwa kiasi ambacho mleta habari kakitoa, this is just like character assacination, na kwenye hilo mleta mada kafanikiwa.

Mkuu nothin z personal here ushaidi upo kama wautaka fata kama Inko alivyosema.
 
MAJUNGU! MAJUNGU! MAJUNGU! MAJUNGUUUUU!!! Imejidhirisha wewe ni mbumbumbu wa maswala ya NGOs. Wapi ulishasikia ED anapatikana kwa kupigiwa kura? Jitahidi uipate katiba yao uisome vizuri ndo uje hapa na hizo tuhuma kuliko kupost vitu utafikri umekoswakoswa kukamatwa ugoni! Ila Wajita kwa majungu hamjambo! Hata mimi niliwahi kufanya kazi na Mjita wa design yako akawa anaandika taarifa za majungu kama zako anazipeleka -----KUU na kwa DSO lakini kesho yake anazikuta ofisini kwangu!! Ilibidi awe mdogo kama piriton! Sasa na wewe umekuja na majungu lukuki. Unajua ni jinsi gani huyo mama alivyoteseka kuanzisha hiyo NGO? Au anavyoteseka kutafuta wafadhili? Unadai hajapeleka taarifa kwa msajili? Wewe unafanya kazi huko? Acha fitina wewe!

umejuaje kama ni mjita?
 
Majungu kwa nini na wewe usianzishe yako? Halafu leo sijui ni chungu ya ngapi maana hii swaumu.
 
duh classmate wangu katajwa,ukitaka kumsema mtu weka sifa au mafanikio na mapungufu yake,ili tuone mizania ya zuri na baya
 
Hata PCCB wanatosha, ninachojua hizi Nothing Going On (NGO) ni kama mtandao mwingine wa ufisadi tu hapa nchoni, japo wanasema ya wenzao ya kwao hawayaoni, na mbaya zaidi mtandao huu umezama hadi kwa mashirika hisani yenyewe, kwani nao hudai cha juu, tatzo kubwa hakuna udhibiti wa kutosha kwa mashirika haya, mfano mdogo yamekuwa yakifanya PETS wakati yenyewe hayana accountability mechanism ya kuweka wazi mapato na matumizi yao kama sheria inavyoyataka ila wao ni wepesi wa kusonda kidole kwa Serikali.........



I second you mdau!!!!wanajifanya wasafi kumbe WIZI mtupuuuuuuuu,nlishawah kufanya NGO moja ina ina lakini mh hayo madudu yake,pdesa za Foundation for Civil Society zilitafunwa sana sana!!!Upo John Ulanga -the Boss???hizi ndo Ngo za kibongo.mdomo mwingiii,ndani wachafuuuuuuuuuuuuu
 
I know in and out kuhusu hiyo NGO, actually I have seen it toka inaanza, huyo mama kaitoa mbali kwa mahangaiko mengi. Anzisha na wewe NGO yako uone mziki ulivyo mzito hadi kufikia kupata wahisani. Then wahisani wapatikane fungu la kumi litake liwa na watu wengine...

Naomba nikuambie hata kama kaitoa mbali cvyo alivyotakiwa kuifanya yaan mama masoy ameover use her power kwenye lile shirika,alipata vijana wazuri wanasheria toka vyuon wenye ari ya kufanya kazi alichokifanya ni kuchukua kazi zo hata field hawakuenda alighushi reports yeye na huyo mhasibu(regina) ambaye ni ndugu yake,kuna wizi wa kufanya ila yeye alizidisha..kingine kibaya kwenye shirika hili ni utawala wa kimangimeza wafanyakazi hata hao interns hawakupewa nafasi ya kutoa maoni yao Bi Flora Masoy na kibibi flani kingine ni Paralegal na Mhasibu(Regina) ndo wenye usemi wa mwisho,na wakitia neno ofisi yaweza msipate mshahara miezi minne,MPLC ilikuwa ni one of the best paralegals zilizoanzshwa na muasisi wao mkuu WLAC(WOMEN LEGAL AID CENTER) nadhani its high wai assess.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
nenda polisi, kwanza inaonekana ht shule huna ndio mana huelewi ht jinsi NGO zinavyo run.una ugomvi binafsi na huyo mama labda amekunyima
 
Wadau Asanteni kwa michango yenu mizuri,nipo katika mchakato wa kuiscan katiba ya Morogoro Paralegal ingawa haionekani vizuri kutokana na wino kuwa faint but nitaibandika muda si mrefu ili wanaojenga hoja na kufanya ufuatiliaji wajue kuwa yanayozungumzwa humu ndani sio majungu.
Kwa ufupi tu, katiba ya Morogoro Paralegal ina kurasa 14, by the way, pamoja na Katiba hiyo kuwa na bodi lakini bodi hiyo kwa muda wa miaka mitano iliyopita imekuwa inactive. Kwa wale wanaofuatilia taratibu za uendeshaji wa NGO watajua ninachokiongea,

Morogoro Paralegal ni Kituo/Shirika lisilo la kiserikali, ni kweli hapo nyuma lilifanya vizuri sana lilipokuwa na vijana wenye hari lakini hali hiyo ilikuwa kubadilika baada ya kuanza kwa madudu ya Bi. Flora Masoy. Kwa mujibu wa katiba ya Morogoro Paralegal, Mwenyekiti wa kituo/Mkurugenzi anateuliwa na Bodi n jina lake kuthibitishwa na mkutano mkuu, katika mazingira ambayo hakuna bodi ya Shirika au kama ipo haifanyi kazi ni vigumu sana kuchaguliwa Mkurugenz au Mwenyekiti mwingine kwakuwa mpaka bodi ifanye uteuzi.

Mkutano mkuu wa shirika unaozungumzwa na katiba ya MPLC ambao uhusisha wanachama wa MPLC haujawahi kufanyika kwa takribani miaka mitano iliyopita. nitaiweka nakala hiyo soon.Tunapozungumza masuala maito kama haya ni vizuri wahusika wakazifnyia kazi, tusiwe kama policcm ambao wanapopewa taarifa za uhalifu badala ya kufuatilia taarifa kuona kama zina ukweli wao wao wanaanza kumshambulia mtoa taarifa.

Watu wafuatao wanaweza kusaidia sana uchunguzi dhidi ya tuhuma za ubadhilifu zinazofanywa na mama Masoy na shirika lake la kifamilia la Morogoro Parallegal
1. Bi. Mary Balaigwa (Mmoja wa waanzilishi wa shirika-aliamua kujiondoa kutokana na Madudu ya Flora Masoy)
2. Mwalimu Bertha Mdundu (Huyu ni mkuu wa shule ya Mafiga-alikuwa member wa shirika akaachana nalo)
3. Amani Mwaipaja (Aliwahi kuwa Mwanasheria wa Morogoro Parallegal kwa miaka minne)
4.Theodora Mlelwa (Huyu ni Mwanasheria na Afisa Mradi wa Foundation-Hajapata Mshahara wake kwa miezi nane sasa baada ya Foundation kusimamisha malipo ya fedha za mradi)
5. Mr. Sakware-Alikuwa Mwenyekiti wa UNGO-Moro, Baada ya kustaafu amemsaidia sana mama Masoy katika uandishi wa miradi alafu akatoswa)
6.Mourine Msangi-(Hawa)-Alikuwa Afisa Mradi wa Foundation-aliamua kukatisha mkataba baada ya kuona mambo hayaeleweki)
7. Wahasibu wa Deloit, wanajua madudu ya Morogoro Paralegal, walifanya ukaguzi wa mahesabu na taarifa kuituma foundation,taarifa ilijaa madudu lukuki
8.Sylivesta Masawe, ingawa hajui kinachoendelea nyuma ya pazia lakini anajua madudu yanayoendelea
9.Bi.Isabela Katungutu, Ni bibi Mwanzilishi wa shirika ambaye mpaka leo anaishi nyumba ya udongo wakati Flora Masoy akibadilisha magari na kuwekeza katika vitega uchumi kwa fedha za mradi
10.Regina Solomon-Mhasibu, ni binti mdogo aliyeingia katika mchezo mchafu wa mama Masoy, anajua mengi sana

Orodha bado inaendelea,nakusanya ushahidi wa kutundika humu ndani
baadae
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom