Leo kuna watu tuliitwa pale LearnIT kufanya aptitude test kwa nafasi za kazi za Sales zilizotangazwa. Cha ajabu tukiwa pale mapokezi kuna mtu mmoja akatoka ofisini ndani na kuja pale tulipo akasogea pembeni kidogo kisha mmoja wetu(mfupi hivi) akaenda kuongea naye na kisha kukabidhi CV yake,akaenda nayo ndani kisha akatoka tena na kuongea na jamaa mwingine aliyekuwa amesimama pembeni kabisa(nadhani akimsuibiri) akachukua CV ya huyu mtu then akaingia ofisin tena. Muda ulifika tukaitwa na mtu mwingine ambaye ndio muhusika tukaenda kufanya test(pamoja na wale wawili) kisha wote tukampa CV zetu kasoro wale wawili. Sasa nashindwa kuelewa kwanini wale walimpa mtu tofauti,muda tofauti na kwa njia tofauti. Test ilikuwa poa na nitafaulu ila kwenye kupata kazi sina imani kabisa. Nawaomba watu wa LearnIT wapitie vizuri mchakato huu wa hizi nafasi bila upendeleo.