Nicholaus Kilunga
JF-Expert Member
- Feb 15, 2014
- 1,188
- 570
CHADEMA YAENDELEA KUHUJUMIWA,MADIWANI WAKE WAKE DODOMA WANUNULIWA KUJIUNGA NA CCM.
Wakuu hii habari sio tetesi tena ,naiweka hapa jukwaani kama habari kamili.
Madiwani wa CHADEMA mkoani Dodoma wamedaiwa kunuliwa na CCM ili kuisaliti CHADEMA siku yoyote kuanzia sasa,madiwani hao 3 wanaotajwa kutoka ji,bo la Mtera na 1 hajatajwa anatokea jimbo wala kata gani ndani ya mkoa huo, mpango huo unaoendelea kuratibiwa na viongozi wa CCM mkoa Dodoma kwakwa ushirikiano wa karibu na viogozi wa ACT pamoja na aliyekuwa mgombea wa CHADEMA jimbo la Mtela mwaka 2010 bwana John Lameck Robote/Lugose,mpango ulioratibiwa kwa mda wa takribani mwezi 1 sasa.
Kwa mujibu wa chanzo cha taarifa hii,awali wasaliti hao walikuwa wamepanga wajiuzuru baada ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan,kutokana na mpango huo haramu kugunduliwa na intelegensia ya CHADEMA,wameamua kuuharakisha na sasa hautasubiri mwezi mtukufu uishe na mda wowote kuanzia sasa wataitisha mkutano wa waandishi wa habari,ama watarudisha kadi kwenye mkutano wa hadhara unaoandaliwa na CCM Dodoma ,mkutano utakaofanyika mda wowote kuanzia sasa na wamependekeza Jk awepo.
Kwa mujibu wa chanzo cha taarifa hii kilichopo miongoni mwa waratibu wa mpango huo muovu dhidi ya CDM,kinadokeza vikao vya awali vilifanyikia katika mikoa ya Daressalam,Morogoro na sasa waratibu wa mpango huo, wapo mkoani Dodoma wakiendelea na uratibu huo kikao kilichoandsliwa kufanyikia Dodoma Hotel,
Mpango huu unaratibiwa na Samwel Malichela (Mtoto wa John Samwel Malichela ambaye anaungwa mkono na viongozi wa CCM jimbo la Mtera na Dodoma katika jitihada zake za kuhakikisha mbunge wa sasa jimbo la Mtera Livingstone Lusinde"kibajaji"anang'olewa kwenye kiti cha ubunge uchaguzi ujao) kwa kushirikiana na viongozi wa CCM mkoa Dodoma kupitia kwa katibu mwenezi wa mkoa, katibu mkuu wa CCM mkoa wa Dodoma bwana Mgumba ambaye mpaka sasa ndiye alieidhinisha malipo ya kugharamia nauli ya kuwaleta madiwani wa CDM kutoka jimboni Mtera,gharama za ukumbi, malazi jumla ya fedha hiyo ni shili Laki 4 na elfu 70(470,000)
Na miongoni mwa magari yaliyotumiwa katika safari za kuratibu shughuli zote hizo za kutaka kuihujumu CDM ni gari namba T 645 CUG aina ya NADIA, Nyaraka zinaonesha mmliki wa Gari hilo ni bwana Kyamani Elpidius, ambaye hadi sasa haijulikani anajishughulisha na nini, Hata hivyo, mtoa taarifa anaendelea kupasha kuwa CCM hadi sasa wameingizwa mkenge kwani mpango uliopo ni kuwa, madiwani hao watajiunga na CCM kwa muda tu, baadae watarudi kujiunga na Chama kipya cha ACT wakati wa uzinduzi wake mwezi wa 9 mwaka huu.
Na mwisho wa siku wameahidiwa kupewa pesa yote ambayo wangelipwa kama madiwani kwa kipindi cha kuanzia siku watakayojiudhuru mpaka mwakani,pia katika sakata hili kuna mtu mmoja anatajwa kwa majina ya Gwakisa Burton anatajwa kuwa nyuma ya mpango huu.
Wakuu hii habari sio tetesi tena ,naiweka hapa jukwaani kama habari kamili.
Madiwani wa CHADEMA mkoani Dodoma wamedaiwa kunuliwa na CCM ili kuisaliti CHADEMA siku yoyote kuanzia sasa,madiwani hao 3 wanaotajwa kutoka ji,bo la Mtera na 1 hajatajwa anatokea jimbo wala kata gani ndani ya mkoa huo, mpango huo unaoendelea kuratibiwa na viongozi wa CCM mkoa Dodoma kwakwa ushirikiano wa karibu na viogozi wa ACT pamoja na aliyekuwa mgombea wa CHADEMA jimbo la Mtela mwaka 2010 bwana John Lameck Robote/Lugose,mpango ulioratibiwa kwa mda wa takribani mwezi 1 sasa.
Kwa mujibu wa chanzo cha taarifa hii,awali wasaliti hao walikuwa wamepanga wajiuzuru baada ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan,kutokana na mpango huo haramu kugunduliwa na intelegensia ya CHADEMA,wameamua kuuharakisha na sasa hautasubiri mwezi mtukufu uishe na mda wowote kuanzia sasa wataitisha mkutano wa waandishi wa habari,ama watarudisha kadi kwenye mkutano wa hadhara unaoandaliwa na CCM Dodoma ,mkutano utakaofanyika mda wowote kuanzia sasa na wamependekeza Jk awepo.
Kwa mujibu wa chanzo cha taarifa hii kilichopo miongoni mwa waratibu wa mpango huo muovu dhidi ya CDM,kinadokeza vikao vya awali vilifanyikia katika mikoa ya Daressalam,Morogoro na sasa waratibu wa mpango huo, wapo mkoani Dodoma wakiendelea na uratibu huo kikao kilichoandsliwa kufanyikia Dodoma Hotel,
Mpango huu unaratibiwa na Samwel Malichela (Mtoto wa John Samwel Malichela ambaye anaungwa mkono na viongozi wa CCM jimbo la Mtera na Dodoma katika jitihada zake za kuhakikisha mbunge wa sasa jimbo la Mtera Livingstone Lusinde"kibajaji"anang'olewa kwenye kiti cha ubunge uchaguzi ujao) kwa kushirikiana na viongozi wa CCM mkoa Dodoma kupitia kwa katibu mwenezi wa mkoa, katibu mkuu wa CCM mkoa wa Dodoma bwana Mgumba ambaye mpaka sasa ndiye alieidhinisha malipo ya kugharamia nauli ya kuwaleta madiwani wa CDM kutoka jimboni Mtera,gharama za ukumbi, malazi jumla ya fedha hiyo ni shili Laki 4 na elfu 70(470,000)
Na miongoni mwa magari yaliyotumiwa katika safari za kuratibu shughuli zote hizo za kutaka kuihujumu CDM ni gari namba T 645 CUG aina ya NADIA, Nyaraka zinaonesha mmliki wa Gari hilo ni bwana Kyamani Elpidius, ambaye hadi sasa haijulikani anajishughulisha na nini, Hata hivyo, mtoa taarifa anaendelea kupasha kuwa CCM hadi sasa wameingizwa mkenge kwani mpango uliopo ni kuwa, madiwani hao watajiunga na CCM kwa muda tu, baadae watarudi kujiunga na Chama kipya cha ACT wakati wa uzinduzi wake mwezi wa 9 mwaka huu.
Na mwisho wa siku wameahidiwa kupewa pesa yote ambayo wangelipwa kama madiwani kwa kipindi cha kuanzia siku watakayojiudhuru mpaka mwakani,pia katika sakata hili kuna mtu mmoja anatajwa kwa majina ya Gwakisa Burton anatajwa kuwa nyuma ya mpango huu.
- :angry: