Madiwani Manispaa ya Moshi-Kipindupindu kinanukia

MPAMBANAJI.COM

JF-Expert Member
Mar 2, 2011
712
331
Salam wapendwa, naamini wahusika hata mbunge atasoma na au ataelezwa kero yetu hii,

ni zaidi ya mwezi sasa huduma ya ubebaji taka imesitishwa ndani ya mji wa moshi. Hali ya uchafu ni ya kutisha maeneo ya kata ndani ya mji huu wa moshi ajabu uso wa stand ni msafi na wakuvutia. Raia wamejitahidi kukodi wazoa taka ila hali bado siyo ukizingatia makazi ya watu wa hapa yamepangika na maeneo ya kutupa taka hakuna.

Wananchi tunaomba kujua
- Kuna mikakati gani katika ufuatiliaji wa suala hili?
- Je kwanini msiweke matetenki ya uchafu katika maeneo mbalimbali ya kata ili kurahisha utupaji na uzoaji taka?
- Je ni dhambi gani mtapata iwapo mtatupa mirejesho ya mikakati ya afya na mazingira kwa sisi raia?
-Je usafi wa marigira na afya bora sio sehemu ya haki za binadamu

Asanteni,
my take, wananchi tumefunguka na kura zetu mtazipata tuu kulingana na umahiri wenu katika uwajibikaji kwa niaba yetu
 
Mkuu huku maeneo ya kwetu dar street ni mwezi wa pili gari la halijaonekana watu wameweka taka mpaka zimekua shida ukipitia maeneo ya mkulima bar dar street watu wamechoka wamezeweka taka barabarabi kuna inzi na harafu mbaya kwa kweli hali ni mbaya
 
Sio kwa sasa ilikua zamani sema jambo kubwa huku ni utamaduni wa watu kuhifazi taka mfano kila mtu anahifadhi taka zake gari ikipita ndio wanatoa na hiyo ndio iliyokua inaupa huu mji sifa ya usafi sasa watu wametunza taka gari haipiti kuchukua miezi miwili kwa hali ya kawaida hakuna mtu anaweza kuvumilia harufu ya taka na kweli wasipofanya jitahada za haraka mitaro na makorongo yote yatajaa taka
 
Back
Top Bottom