Vurugu kubwa ziliibuka katika kikao cha Baraza la Madiwani la Manispaa ya Kinondoni, jana baada ya madiwani wa Chadema kuhoji matumizi ya sh. 44 milioni zilizodaiwa kutengwa kwa ajili ya Ilani ya Uchaguzi wa CCM.
Vurugu hizo ziliibuka mwishoni mwa kikao baada ya madiwani wa Chadema kuhoji na kutaka kubadilishwa matumizi ya fedha katika Bajeti ya Halmashauri ya mwaka 2011/12 walizodai kuwa zimepangwa kwa ajili ya kuandaa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.
Kauli ya madiwani hao iliyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Kawe, Halima Mdee na madiwani wa CCM wakiwa na jazba walikuja juu na kutaka mjadala ufungwe.
Wakati mzozo ukiendelea Diwani mmoja wa CCM alisimama na kusema "CCM oyeee!" na kuitikiwa "Oyeeeeee!"
Diwani wa Chadema naye akasimama na kusema "peoples!" na kuitikiwa "power!!!"
NAWAKILISHA!!!!!!!
Vurugu hizo ziliibuka mwishoni mwa kikao baada ya madiwani wa Chadema kuhoji na kutaka kubadilishwa matumizi ya fedha katika Bajeti ya Halmashauri ya mwaka 2011/12 walizodai kuwa zimepangwa kwa ajili ya kuandaa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.
Kauli ya madiwani hao iliyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Kawe, Halima Mdee na madiwani wa CCM wakiwa na jazba walikuja juu na kutaka mjadala ufungwe.
Wakati mzozo ukiendelea Diwani mmoja wa CCM alisimama na kusema "CCM oyeee!" na kuitikiwa "Oyeeeeee!"
Diwani wa Chadema naye akasimama na kusema "peoples!" na kuitikiwa "power!!!"
NAWAKILISHA!!!!!!!