Madini haya hapa tena

OSOKONI

JF-Expert Member
Oct 20, 2011
10,965
5,336
'Ungeni mkono uchimbaji Urani' Serikali Send to a friend
Monday, 24 October 2011 09:27
0diggsdigg

Mwandishi Wetu
SERIKALI imewataka Watanzania na wadau mbalimbali wa madini kuunga mkono uchimbaji wa madini ya Urani unaotarajiwa kuanza hivi karibuni chini ya Kampuni ya Madini ya Mantra Resources Limited.

Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Tarishi Kibenga akizungumza katika semina kwa wadau wa madini ikiwahusisha wajumbe wa Kamati ya Bunge Maliasili na Utalii alisema Serikali itahakikisha uchimbaji wa madini hayo unakuwa na manufaa kwa Watanzania.

Katika semina hiyo mada mbalimbali ziliwasilishwa ambapo pamoja na mambo mengine ni mada za sheria ya madini, uhifadhi wa mazingira na athari zake, taarifa ya mradi wa madini ya Urani wa Mto Mkuju wa Namtumbo na athari za mionzi ya madini ya Urani.

Alisema tayari kampuni ya Mantra ipo katika mchakato wa upembuzi yakinifu kuhusiana na uchimbaji huo katika Mkoa wa Ruvuma Wilaya ya Namtumbo na kwamba hatua hizo zipo mwishoni kumalizika.

Aliwataka Watanzania na wadau wengine ndani ya sekta hiyo kuunga mkono hatua za utekelezaji wa kufanikisha mradi huo ambao anaamini utakuwa na manufaa makubwa kwa Watanzania na taifa kwa ujumla.

"Serikali tayari tumetoa idhini kwa Kampuni ya Mantra kufanya tathimini na upembuzi katika kuelekea uchimbaji hivyo tunatakiwa kuunga mkono hatua hii ambayo Serikali inaamini itakuwa na manufaa makubwa kwetu sote," alisema Kibenga.

Kwa upande wao wajumbe wa Kamati ya Bunge Maliasili na Utalii pia walionyesha kuunga mkono uchimbaji huo lakini wakitahadharisha juu ya umakini katika kuchukuliwa tahadhari za athari za madini hayo.

James Lembeli, Mbunge wa Kahama ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati hiyo alisema hakuna haja ya kuwa na wasiwasi juu ya mradi huo na kwamba jambo la muhimu ni kuhakikisha madini hayo yanawanufaisha Watanzania.

Alisema kamati hiyo imepata nafasi ya kutembelea eneo la mradi wa Mto Mkuju wa Namtumbo na kujionea hali halisi ambapo madini husika yakionyesha kuwepo kwa kiasi kikubwa katika ardhi ya Namtumbo.

Mbunge wa Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema Serikali inapaswa kuwa makini kuhakikisha mikataba ya madini husika inatekelezwa hususani upande wa tahadhari kuhusiana na madhara ya madini hayo kwa wakazi wa maeneo husika.

Alisema walitembelea eneo la mradi na kupata maelezo kutoka kampuni husika yakionyesha tahadhari kubwa zinachukuliwa katika kuhakikisha uchimbaji wa madini hayo hauleti madhara kwa wahusika na unakuwa na tija kwa taifa.

source: Mwananchi


 
Ruksa tunachohitaji ni maendeleo, ila chondechonde uhifadhi wa mazingira katika eneo husika usingatiwe.
 
Mikataba yote inayosainiwa na hii serikal yetu haikosi 10%! kwanini sehemu zote za migodi wananchi waliopo maeneo hayo hawanufaiki na huo uwekezaji? pia najiuliza mjomba anataka auze vitu vyo kabla ya kuondo kwny uongozi, kwa ushauri wangu asibinafsishe kwanza asubirie katiba mpya.
 
2015 vijana wenzangu tusifanye makosa, tumuingize Sata wa bongo aka Dr. Slaa, atupe somo watanzania.
 

Aliwataka Watanzania na wadau wengine ndani ya sekta hiyo kuunga mkono hatua za utekelezaji wa kufanikisha mradi huo ambao anaamini utakuwa na manufaa makubwa kwa Watanzania na taifa kwa ujumla.

Mpaka sasa hayo madini ambayo wameshachimba yameleta manufaa gani kwa watanzania na taifa kwa ujumla..., au hizi faida zitaanzia kwenye huu mradi.?
 
Watanzania tusiunge mkono uchimbaji wa madini ya Uranium. Kwani ni manufaa ya wachache wa serikali ya Ccm na maafa makubwa kwa
Watanzania na Dunia nzima, Hawa mafisadi wapo katika mwelekeo wa kuliangamiza Taifa letu la Tanzania.
 
Hayo ya Namtumbo mbona yashaanza kuchimbwa na kuchukuliwa na hao manta siku nyingi? au sielewi anachomaanisha?
 
Watueleze tumefaidiki nini toka kwenye hiyo migodi mingine kwanza kabla ya kutulazimisha tuukubali huu wa Ruvuma
 
Tatizo la watawala wa ccm wanachosema hawakitekelezi na wanachokitekeleza hawakisemi, sasa unaweza kuta uchimbaji wa uranium wakatutia changa la macho,mimi siwaamini kabisa hoa wanaharamu wakubwa, wana mipango mingi ya siri ambayo ndani yake imejaa uovu. Mungu atusaidie sana.Tunateswa sana watz, Mungu alitujalia madini mengi lakini mafirauni wachache wanafaidi, angalia barrick na wengineo wanavyochua madini ya malofa matz. Kweli bongo lala.
 
Wanaosema maendeleo yataletwa na Uranium, nawasihi wakumbuke kuwa kuna madini ya aina nyingi hapa Tz lakini hayawahi kuleta maendeleo yenye tija kwa walala hoi. Pia waulize tone za madini mbalimbali yanayouzwa nje, jamani tusirusu uchimbaji wa madini haya kwa sasa maana bado hata hayo mengine wakoloni mamboleo hawajayamaliza, tusubiri angalau wamalize hayo mengine, mbona walafi hawa wanataka kumaliza vyote kwa wakati mmoja? Tukiwaruhusu imekula kwetu, faida kwao madhara kwetu ni ya milele.
 
Ruksa tunachohitaji ni maendeleo, ila chondechonde uhifadhi wa mazingira katika eneo husika usingatiwe.
Wasiruhusiwe kuchimba, kwanza tutafakari manufaa ya Dhahabu kwa Watanzania. Tz ni ya tatu kwa uzalishaji Dhahabu lakini wakati mwingine inapata taabu hata kulipa mishahara ya Watumishi wake.
 
Kwa hili Siungi mkono. Kwamza ni mapema mno kuanza kuchimba madini hatari (yenye mionzi hatari) kama haya; kwani hata kukontroo kwake ni kugumu, hebu angalia japan pamoja na ujanja wake wa kiteknolojia lakini vinu vyake vilipopigwa dhoruba ilikuwa ni tatizo kwa nchi yao, vipi kama ingekuwa TZ. Lakini pili, bado vitega uchumi vyetu vikuu kama vile madini (hasa dhahabu na tanzanite), mbuga pamoja vingine havijaonekana vikiwa na manufaa sana kwa wanchi zaidi ya madini yetu pamoja na wanyanyama kuchukuliwa bure na kupelekwa ulaya. Tatu tuna viongozi uchwara wanaotengeneza mikataba isiyokuwa na manufaa kwa mtanznia ila manufaa kidogo kwa baadhi ya vigogo na yenye neema kwa wale wanaoitwa wawekezazi, tena si ajabu ikikubalika kwa hili mkata ukatangenezwa bomu kuliko ule wa richmond/dowans na ukasainiwa hotelinihuko ulaya.

Kwa ujumla sina imani na viongozi wakuu wa nchi kama wanaweza kutengeza mkataba wowote wenye kuwanufaisha watz.
 
Mimi siungi mkono kabisa!!! Kwanza Serikali itueleze tunanufaika vipi na madini ambayo yanachimbwa sasa hivi na hao waporaji kabla ya kuingiza waporaji wengine!!!! Madini yenyewe wanataka kuchimba katika pori la akiba la Selous!!!!... Yaani Serikali hii bwana!!!!...
 

Monday, 24 October 2011 09:27
0diggsdigg

Aliwataka Watanzania na wadau wengine ndani ya sekta hiyo kuunga mkono hatua za utekelezaji wa kufanikisha mradi huo ambao anaamini utakuwa na manufaa makubwa kwa Watanzania na taifa kwa ujumla.

/QUOTE]

Huyu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Tarishi Kibenga vipi? Atwambie kwanza Taifa linapata mgao wa asilimia ngapi? Akina Mzindakaya kwenye ubinafsishaji wa makaa ya mawe walisema wazi tunapata 10%. Huyu ni sawa na Jairo tu, atamke tunapata asilimia ngapi ndo aseme upuuzi wake!
 
Back
Top Bottom