OLS
JF-Expert Member
- Oct 12, 2019
- 457
- 773
Japo michoro ya mwilini(Tattoo) ni kitu kinachopendwa na watu wengi. Asilimia 40 ya vijana wana michoro hiyo mwilini walau picha moja
Hatua zenyewe za uchoraji kwanza huhitaji sindano ambayo kimsingi huiumiza ngozi ili kuweka michoro, sindano huweka matone ya rangi. Kama ngozi itapona vizuri ndio huacha mchoro mzuri kwenye ngozi ambayo huwa urembo
Madhara ya tattoo ni haya yafuatayo
1. Unaweza kukosa fursa mbalimbali
Mfano katika mashindano ya ulimbwende hayaruhusu mtu mwenye tattoo inayoonekana kushiriki katika kinyang’anyiro hicho.
Suala hilo liliwahi kudhihirika kwa Rachel George ambaye alikuwa akishiriki mashindano hayo ngazi ya wilaya jijini Dar es Salam. “Ilibaki kidogo nitolewe lakini nikawahi kuifuta na kwa sababu haikuwa kubwa sana kovu halikuleta shida na rangi ya ngozi yangu nyeusi ilisaidia katika kuficha uangavu wa kovu lile,”
Vijana wanaoiga kuchora tattoo za maisha wamekuwa wakikosa fursa walizozitamani na wengine wamekuwa wakiponea chupuchupu
Mh. Temba, alifanya kila awezalo na kufanikiwa kujiunga na mafunzo ya jeshi zaidi ya mara tatu, na mara zote alifanikiwa kuhitimu mafunzo, lakini mara nyingine kabla hajakabidhiwa ajira anajikuta anaachishwa au anaacha na kisha anarudia tena mafunzo
2. Maambukizi ya ngozi
Namna nzima ya kuchora michoro hiyo huipa michubuko ngozi yako, ambayo huimuzi tabaka la juu na la kati la ngozi.
Mtu huwa katika hatari ya kupata maambukizi kwa wiki mbili za mwanzo baada ya kujichora. Dalili zake huwa ni pamoja na wekundu kwenye ngozi, kuwashwa, au kutoa usaha.
Maambukizi hayo yakiendelea yanaweza kusababisha homa. Mara nyingi maambukizi hayo huwa sugu
3. Kuwa na aleji/mzio
Watu wengine huanza kuwa na aleji mara baada ya kujichora. Hii huhusianishwa sana na wino uliotumika kuchora, haswa kama wino ukiwa na plastiki. Mayo clinic wanasema rangi nyeundu, njano, buluu na kijanii huwa na uwezekano mkubwa wa kutengeneza aleji kwa aliyejichora
Madhara ya aleji huweza kutokea miaka kadhaa baada ya kujichora.
4. Matatizo kipindi cha kufanya kipimo cha MRI
Ikitokea daktari akisema inabidi kufanyiwa MRI Scan, mara nyingi tatuu huwa kikwazo. Na pia huvimbana kuwasha kisha kupotea yenyewe
Hatari huongezeka kama umetumia wino wa ubora wa chini au kama michoro ni ya muda mrefu
5. Saratani ya ngozi
Kwa kiasi kikubwa saratani ya ngozi inaweza kusababishwa na michoro hii na magnjwa mengine yanayohusika na ngozi. Kwa sababu unapotoboa layer ya juu ya ngozi ya binadamui na kuweka wino wenye kemikali huweza kuleta madhara tofauri kati ya mtu mmoja na mwingine.
6. Kushindwa kuchangia damu
Mtu mwenye michoro mwili hawezi kuchangia damu hata kama kundi la damu yake linafanana na mgonjwa, hali hii itafanya kupeteza watu ikiwa kuna mgonjwa anayehitaji damu kwa haraka
Watu waliochora tattoo hukosa pia fursa ya kuchangia damu hata ikiwa ni kwa dharula hiyo ni kutokana na uwepo wa hatari ya kusambaza ugonjwa kwenda kwa mtu mwingine,
Kutana na mkali mwenye tattoo nyingi duniani kwa mwaka 2019
Lucky Diamond Rich, ndiye mtu mwenye tattoo nyingi mwilini kwa rekodi ya mwaka 2019 alizaliwa New Zealand, akiwa anaitwa Gregory Paul McLaren, "Diamond limekuja kuwa jina langu kwa kuwa marafiki zangu wananiita Almasi chafu, na pia wameniita Rich(Tajiri) kwa kuwa mimi ni tajiri wa kiroho"...
======
Maoni ya wachangiaji
Kwa mtu wa Tanzania kutofahamu Tattoo ni kitu gani, ni kitu cha Kawaida sana .Kwa maana Tattoo wengi tunaziona kwa Watu maarufu ambao wengi wana maisha ya ajabu ajabu kama ya ha Wakina Irene
Lakini mtoa mada na wadau wengine nataka kukwambia kuwa Tattoo ni kitu muhimu sana kwa jamii tena za kiafrika kwani Tattoo ilikuwepo hata kabla ya Ukoloni.
Na Tattoo wakati huo hazikupakwa kama sehemu ya Urembo hapana, na haikuwa kwa ajili ya Watu maarufu pia.
Wakat huo tattoo ilikuwa ni kwa jamii nzima na ilikuwa ni sehemu ya Utamaduni. Kupitia Tattoo watu waliweza kuwasiliana na kupeana Utambulisho kwa mfano Kabila la Wamakonde
Lakini pia ukija huko Amerika hasa kwa Hao Watu weusi Tattoo zilikuwa sehemu ya Harakati za Ukombozi. Kwani ilikuwa kazi ngumu kusimama hadharani na kudai uhuru mbele ya Watu weupe uko Amerika.
Hivyo kupitia Tattoo watu walijichora na kuwalilisha Ujumbe kadri wawezavyo bila watu wengine kujua.
Hivyo ni asilimia kubwa sana ukiwa USA ukikutana na Watu wamechor tattoo watakwambia sababu za kuchora, na sababu zao zinafungamana na historia halisi ya maisha aidha ya mtu mmoja au ya jamii nzima. Na ndio maana huko unakuta mtu kachora Tattoo ya Rosa Park.
Lakini huku kwetu kwa kuwa tunaiga kupitia Video na kuona tu Wanawake wanaovaa vichupi na wanaume ambao ni Wasanii. Hudhani kuwa Tattoo ni kitu cha Starehe na hivyo ni kinyume na Dini zetu wa hapa Afrika.
Hapo hapo kuna mtu ambaye pengine yeye ni Mwislamu bado haelewi Tattoo ni kitu gani wakati huo huo kuna Wanamke kavaa ijabu na bado kapaka Ina. Ambayo kimsingi ni michiro ile ile na rangi ni zile zile. Na ina dhamira sawa na waliochora Tattoo.
️Hoja zangu hizi zinasimama kwa watu wanaoamini kuwa Tattoo ni Dhambi na wale wanadhani Tattoo ni Uhuni pia. Kwani kuna Watu wana Tattoo za Yesu, nao tunawaweka kwenye kundi gani??
Dhambi ya tattoo ni ipi? Kile ulichochora au tabia zako baada ya kuchora?
Leo hii Lil Wayne wa Cash Money akija Tanzania na kutaka kutoa ufadhiri wa ujenzi wa kanisa, kuna watu watamkataza kisa ana Tattoo mwilini?
Ni kweli kuna madhara yake lakini jamii pia lazima ifahami Tattoo ni kitu gani na sio tu kuwa majibu ya Kidini dini bila kujua historia kamili.
View attachment 1322625
️Hoja zangu hizi zinasimama kwa watu wanaoamini kuwa Tattoo ni Dhambi na wale wanadhani Tattoo ni Uhuni pia. Kwani kuna Watu wana Tattoo za Yesu, nao tunawaweka kwenye kundi gani??
kidogo umeweza kuweka sawa kwenye hili kimtazamo wangu nachojua kidogo kwenye tattoo ni kumbukumbu yakitu fulani mtu anaiweka kwenye mwili mfano Wayne zile tattoos ni kumbukumbu za vitu vyake sasa sijui hao wanaochora nao ni kwajili ya kumbukumbu pia.