Madhara ya kutokujua historia yako

sambeke

JF-Expert Member
Nov 26, 2014
713
652
Ulishawahi kujiuliza kaanini Nchi za Kiafrika kwa maana ya viongozi pamoja na watu wake wengi wamegubikwa na ubinafsi, uchoyo na ubaya uliokithiri dhidi ya waafrika we wenzao?

Lipo jambo moja ambalo nataka sote tulitafakari kama sehemu ya tafakuri zetu za mchana labda tutaweza kuona sababu na hivyo kutufanya kuwa chachu ya mabadiliko!

1. Kwanza kabisa Historia ya Bara la Afrika imepotezwa! Kwa kupachikwa historia ya uwongo au sehemu nyingine kuachwa kama hakuna chochote cha kuongelea kuhusu eneo hilo na hivyo kufanya kama vile hakuna lolote lililowahi kutokea mahali hapo!

Sasa hii madhara yake ni nini? Madhara yake ni kwamba pale mtu anapokupndolea historia yako anakupoteza (He makes you NO BODY) kwa sababu historia inakuthibitisha (History makes you SOMEBODY)

utaniuliza kivipi?

Nitatoa mfano:- Moja ya sifa kubwa ambayo watu hujivunia ni pamoja na UKOO anaotoka! (Clan) zipo koo zinazotokana na #UCHIFU, #MSHILI = :kwa wenzetu kule Meru" #MANGI = kwa wachaga n.k! Na sababu kuu ya jina la ukoo kuwa la Muhimu ni kwasababu lenyewe ndilo linalobeba Historia yako! Jina la ukoo ndilo linalobeba #thamani yako! Na thamani hii huimarishwa na #historia ya ukoo wenyewe! Bila historia leo hii tusingekua na heshima tunayojivunia katika familia zetu!

Sasa nini kilifanyika? Walipokuja wazungu kututawala, walihakikisha kwanza wanatuondolea heshima yetu ambayo ni historia yetu na kutupandia historia yao! Wakatuondolea majina yetu ambayo yalikua na maana kuungana na historia zetu kila mmoja na kutubatiza kwa majina yao ambayo wengine hata maana zake hatujui! Haya yote yalifanikiwa kwa kupitia dini walizozileta hulu wakituogofya kwa jehanamu ijayo kama hatakubali kugeuzwa (converted) namnawaliyotaka wao na iliyowatukuza wao!

Kwa kuogopa jehanam tukakubali kupoteza utu wetu, historia yetu, imani yetu ya asili (natural) na kuanza kuishi maisha ya hofu na mashaka wakati wote na mwisho wake ni kufupisha uhai wa maisha! Sote tutakubaliana kwamba wazee wetu waliishi miaka mingi na moja ya siri ni kwamba waliishi maisha yasiyo na hofu za kupandikizwa wala pasipo na mashaka ya mambo ambayo kiuhalisia ni nadharia tu na wala sio chochote hivyo tukapoteza jinsi ya kuwaza, (reasoning) tukapoteza fahari yetu (our pride) na historia kwa jumla.

Haya yote yametuacha kuwa utupu; (NO BODY) leo hii angalia historia zinazofundishwa mashuleni! Zote zimejaa utukufu wa wakoloni kama vile nchi hizi hazikuwahi kukaliwa na watu kabla ya wakoloni hawa!

Dunia hii inasemekana imeishi miaka zaidi ya Mamilioni iliyopita! Lakini angalia historia ya nchi zetu yote inaanzia miaka sio zaidi ya mia mbili iliyopita na historia inayoenda mbali zaidi ya hapo inajaribu kufutwa kwa kutoizungumzia sana maana haijabeba fahari ya wakoloni bali ya mashujaa babu zetu waliokua watu wakuu sana na wenye kutukuka!

Tumefanywa sio kitu (NO BODY) Tumeondolewa uhalisia wetu na hivyo kujikuta tunaishi maisha yasiyo halisi (an artificial life) ambayo ni ya kuchanganya sana (very stressful) na hii kazi yake ni kutufupishia siku zetu za kuishi (life span) kwa ujumla!.

Kuna tofauti kubwa sana kati ya Imani kwa Mungu na #DINI, babu zetu walikua na imani kwa Mungu bila dini! Hawakufundishwa na mtu yeyote maana Mungu huishi ndani yetu na sisi ndani yake hivyo unapozaliwa unazaliwa na uungu ndani yako na huo ndio uliowaongoza babu zetu kuabudu! Walifanya ibada kwa Mungu asiyeonekana! (Invisible God) na huyo ndiye Mungu halisi! Mungu ambaye hakua na dini! Mungu ambaye hakua na sura! Hivyo kutufanya sote tujione wamoja bila kubaguana maana wote walijiona wanatoka kwa Mungu mmoja, asiyeonekana na asiye na sura!

Sasa walipokuja watawala hawa, wakatuletea mpaka sura ya Mungu!

Matokeo yake ni nini?Matokeo yake kukatokea kugaqanyika! wakatokea waliosema Mungu hana sura na wale waliokubali mafundisho ya Mungu mwenye sura na umbo fulani kwa hofu ya jehanam (ambayo uhalisia wake nao haupo) wakajitenga! Ndani ya waliojitenga nako kukawa na tofauti zilizopelekea kuwepo kwa msururu wa dini ambazo kila mmoja akijaribu kujiaminisha kwa Mungu mmoja ambaye mwanzo walimwabudu wote kwa pamoja!

Unaweza kuona athari za kuifuta historia ya jambo au ya mahali au ya nchi au ya Dunia kwa ujumla! Athari ni kubwa sana! Leo hii mwanadamu amekua kiumbe hatari sana kwa mwanadamu mwenzake na sababu ni moja tu! Amepotezewa kumbukumbu ya historia yake! Hakumbuki tena kama sote sisi tunatoka kwa mtu mmoja #MUNGU. Na kama ni hivyo sisi sote bila kujali rangi, Kabila, Utaifa, dini, na lugha, sisi sote tunatoka kwa mmoja. Na ndiyo maana pamoja na yote haya sisi sote tunao mwisho mmoja!! Kama tulikua hatuna mwanzo mmoja basi tusingekua na mwisho mmoja!

Turudi tulikoanguka tukaanze upya, naamini hatujachelewa, tupendane tukianza na familia zetu mpaka nchi na ulinwengu kwa ujumla. Hiyo ndiyo familia aloijenga Mungu! Kama vile ambavyo hakuna baba anaetaka familia yake ifarakane kadhalika Mungu anatutaka tuwe wamoja.

Waliotuletea dini hizi wao wameachana nazo! Lakini angalia walivyo na umoja! Wote wanapendana bila kujali nchi wanazotoka akimuona yeyote mwenye rangi kama yakwake humpa msaada na kumuhudumia kidugu bila kujali utaifa wake!

Sisi waafrika ni wakati wetu sasa kuamka! Tuondoe dhana ya ukoloni ndani yetu na tutambue sisi sote ni wamoja! Tunatoka kwa baba mmoja.

Jumapili njema kwenu nyote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuanzie kwa viongozi wetu wa nchi wanaohubiri uzalendo, amani na mshikamano huku wao wakiwa wabinafsi, wezi na wasio na utu.

Mmoja aliwahi kusema hakuleta tetemeko kisa tu hataka kusaidia ila upande wa 2 akatoa msaada. Unaweza kuona hii roho ya ubinafsi inaanzia wapi.

Laiti kama hawa wanaojiita viongozi wangetawaliwa na uzalendo, hekima na busara jamii nzima ingefuata misingi ya umoja, mshkamano na uzalendo ila wao wametawaliwa na roho za uroho wa madaraka na ubinafsi.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ulishawahi kujiuliza kaanini Nchi za Kiafrika kwa maana ya viongozi pamoja na watu wake wengi wamegubikwa na ubinafsi, uchoyo na ubaya uliokithiri dhidi ya waafrika we wenzao?

Lipo jambo moja ambalo nataka sote tulitafakari kama sehemu ya tafakuri zetu za mchana labda tutaweza kuona sababu na hivyo kutufanya kuwa chachu ya mabadiliko!

1. Kwanza kabisa Historia ya Bara la Afrika imepotezwa! Kwa kupachikwa historia ya uwongo au sehemu nyingine kuachwa kama hakuna chochote cha kuongelea kuhusu eneo hilo na hivyo kufanya kama vile hakuna lolote lililowahi kutokea mahali hapo!

Sasa hii madhara yake ni nini? Madhara yake ni kwamba pale mtu anapokupndolea historia yako anakupoteza (He makes you NO BODY) kwa sababu historia inakuthibitisha (History makes you SOMEBODY)

utaniuliza kivipi?

Nitatoa mfano:- Moja ya sifa kubwa ambayo watu hujivunia ni pamoja na UKOO anaotoka! (Clan) zipo koo zinazotokana na #UCHIFU, #MSHILI = :kwa wenzetu kule Meru" #MANGI = kwa wachaga n.k! Na sababu kuu ya jina la ukoo kuwa la Muhimu ni kwasababu lenyewe ndilo linalobeba Historia yako! Jina la ukoo ndilo linalobeba #thamani yako! Na thamani hii huimarishwa na #historia ya ukoo wenyewe! Bila historia leo hii tusingekua na heshima tunayojivunia katika familia zetu!

Sasa nini kilifanyika? Walipokuja wazungu kututawala, walihakikisha kwanza wanatuondolea heshima yetu ambayo ni historia yetu na kutupandia historia yao! Wakatuondolea majina yetu ambayo yalikua na maana kuungana na historia zetu kila mmoja na kutubatiza kwa majina yao ambayo wengine hata maana zake hatujui! Haya yote yalifanikiwa kwa kupitia dini walizozileta hulu wakituogofya kwa jehanamu ijayo kama hatakubali kugeuzwa (converted) namnawaliyotaka wao na iliyowatukuza wao!

Kwa kuogopa jehanam tukakubali kupoteza utu wetu, historia yetu, imani yetu ya asili (natural) na kuanza kuishi maisha ya hofu na mashaka wakati wote na mwisho wake ni kufupisha uhai wa maisha! Sote tutakubaliana kwamba wazee wetu waliishi miaka mingi na moja ya siri ni kwamba waliishi maisha yasiyo na hofu za kupandikizwa wala pasipo na mashaka ya mambo ambayo kiuhalisia ni nadharia tu na wala sio chochote hivyo tukapoteza jinsi ya kuwaza, (reasoning) tukapoteza fahari yetu (our pride) na historia kwa jumla.

Haya yote yametuacha kuwa utupu; (NO BODY) leo hii angalia historia zinazofundishwa mashuleni! Zote zimejaa utukufu wa wakoloni kama vile nchi hizi hazikuwahi kukaliwa na watu kabla ya wakoloni hawa!

Dunia hii inasemekana imeishi miaka zaidi ya Mamilioni iliyopita! Lakini angalia historia ya nchi zetu yote inaanzia miaka sio zaidi ya mia mbili iliyopita na historia inayoenda mbali zaidi ya hapo inajaribu kufutwa kwa kutoizungumzia sana maana haijabeba fahari ya wakoloni bali ya mashujaa babu zetu waliokua watu wakuu sana na wenye kutukuka!

Tumefanywa sio kitu (NO BODY) Tumeondolewa uhalisia wetu na hivyo kujikuta tunaishi maisha yasiyo halisi (an artificial life) ambayo ni ya kuchanganya sana (very stressful) na hii kazi yake ni kutufupishia siku zetu za kuishi (life span) kwa ujumla!.

Kuna tofauti kubwa sana kati ya Imani kwa Mungu na #DINI, babu zetu walikua na imani kwa Mungu bila dini! Hawakufundishwa na mtu yeyote maana Mungu huishi ndani yetu na sisi ndani yake hivyo unapozaliwa unazaliwa na uungu ndani yako na huo ndio uliowaongoza babu zetu kuabudu! Walifanya ibada kwa Mungu asiyeonekana! (Invisible God) na huyo ndiye Mungu halisi! Mungu ambaye hakua na dini! Mungu ambaye hakua na sura! Hivyo kutufanya sote tujione wamoja bila kubaguana maana wote walijiona wanatoka kwa Mungu mmoja, asiyeonekana na asiye na sura!

Sasa walipokuja watawala hawa, wakatuletea mpaka sura ya Mungu!

Matokeo yake ni nini?Matokeo yake kukatokea kugaqanyika! wakatokea waliosema Mungu hana sura na wale waliokubali mafundisho ya Mungu mwenye sura na umbo fulani kwa hofu ya jehanam (ambayo uhalisia wake nao haupo) wakajitenga! Ndani ya waliojitenga nako kukawa na tofauti zilizopelekea kuwepo kwa msururu wa dini ambazo kila mmoja akijaribu kujiaminisha kwa Mungu mmoja ambaye mwanzo walimwabudu wote kwa pamoja!

Unaweza kuona athari za kuifuta historia ya jambo au ya mahali au ya nchi au ya Dunia kwa ujumla! Athari ni kubwa sana! Leo hii mwanadamu amekua kiumbe hatari sana kwa mwanadamu mwenzake na sababu ni moja tu! Amepotezewa kumbukumbu ya historia yake! Hakumbuki tena kama sote sisi tunatoka kwa mtu mmoja #MUNGU. Na kama ni hivyo sisi sote bila kujali rangi, Kabila, Utaifa, dini, na lugha, sisi sote tunatoka kwa mmoja. Na ndiyo maana pamoja na yote haya sisi sote tunao mwisho mmoja!! Kama tulikua hatuna mwanzo mmoja basi tusingekua na mwisho mmoja!

Turudi tulikoanguka tukaanze upya, naamini hatujachelewa, tupendane tukianza na familia zetu mpaka nchi na ulinwengu kwa ujumla. Hiyo ndiyo familia aloijenga Mungu! Kama vile ambavyo hakuna baba anaetaka familia yake ifarakane kadhalika Mungu anatutaka tuwe wamoja.

Waliotuletea dini hizi wao wameachana nazo! Lakini angalia walivyo na umoja! Wote wanapendana bila kujali nchi wanazotoka akimuona yeyote mwenye rangi kama yakwake humpa msaada na kumuhudumia kidugu bila kujali utaifa wake!

Sisi waafrika ni wakati wetu sasa kuamka! Tuondoe dhana ya ukoloni ndani yetu na tutambue sisi sote ni wamoja! Tunatoka kwa baba mmoja.

Jumapili njema kwenu nyote.

Sent using Jamii Forums mobile app
Waafrika hawajawahi kuwa na umoja usidanganye watu.

Ukoloni na dini zao una mambo Mengi Mazuri sana ukilinganisha na yaliyokuwepo kwa waafrika.

Waafrika ni kizazi kilichojawa na Ubinafsi ,chuki na Fitina, Kama waafrika wangekua na umoja wasingetawaliwa na huyo Mkoloni.
Mkoloni hakuja Afrika kwa Mitutu ya Bunduki Bali kwa kutumia maneno yaliyojaa hekima na maarifa.
Wakoloni walikuja kama kundi dogo sana.
Waliokuja kuleta dini hawakuwa wabinafsi mana waliacha kwao penye ndugu zao na familia zao na Mali zao wakaja huku kulikokua hakuna ndugu zao wala hapakua na starehe walizoziacha kwao.
Walifanya kama bahati nasibu tu kuja mana hawakujua wangekutana na watu wa namna gani. Wengine waliuawa ba wanyama wakali ,wengine na watu waliowaona kama viumbe vya ajabu ,wangine waliwaona kama albino ambao kwa mila potofu walihesabiwa kama watu wenye kuleta mabalaa kwenye nchi.

Mfano dini ya Ukristo haikuwa dini ya asili ya wazungu wote ,ilipelekwa na kuhuburiwa kama ilivyokuja Afrika .
Wala Uislam haikua dini ya asili ya waarabu wote Bali ilienezwa kote kama ilivyoenezwa Afrika.

Hakuna dini zilizokua na vitisho kama dini za asili za mwafrika.
Na wale waliokua na miujiza na nguvu kubwa waliogopwa badala ya kuwa msaada kwa jamii.

Usifikiri babu zetu walikua wajinga na wewe ambaye hukuwepo ndiye mjanja na mwenye akili. Babu zetu walijua sana mila zao lakini walikubali kupokea dini na mambo mazuri waliyokuja nayo wakoloni. Mengine waliyakubali kutokana na kuwa tangu wanazaliwa na waliishi miaka yote hawakiwahi kuona wala kusikia mambo kama waliyokuja nayo wazungu. Real and tangible things. Mtu hajawahi kusikia wala kuona simu au radio halafu anakuja MTU anamuonyesha simu na kupiga na kuongea na mtu aliyeko mbali kwa sekunde bila masharti kama ya wachawi na kificho. Lazima ataona kuna tofauti.

Na yale makabila waliokataa kupokea yale waliyokuja nayo wakoloni iwe waarabu au wazungu kama Wahazabe mpaka leo wanaishi porini na hatuoni Maendeleo yao.
Hatuoni wakifundisha elimu ya asili kwa wazi zaidi ya kificho. Wana uganga wa kupita mahali bila kuonekana lakini mpaka wanasiasa wakienda huko wanawapigia magoti kuomba nyama za nyani na chakula mana wana njaa balaa. Akili ya kufuga nyani wengi hawana. Hawana hata mwonekana na mambo mazuri ya kuushawishi ulimwengu ufuate mila zao za asili.

Asili ya binadamu ni moja dunia nzima, Mungu anapotaka kubadili ulimwengu anawatumia wale watu jasiri wenye nguvu; ama nguvu ya Kivita au Nguvu ya kiakili na maarifa.
Ni lazima babu zetu walikubali kufuata mambo mazuri na yenye kubadili maisha yao kuwa bora zaidi.
Mh.Rais wetu kama angebakia kwenye kazi yake ya kwanza ya ualimu bila shaka angekua anajiandaa tu kustaafu akiwa mtu wa kawaida na maisha ya kawaida ,kamwe asingekua amiri jeshi mkuu nchi nzima. Lakini aliamua kubadili gia angani na kuingia kwenye siasa ambayo ilikua ni chagua bora zaidi kwake na limemjengea heshima kubwa na mamlaka makubwa zaidi.

Kama dini za hao wazungu na elimu zao zimewafanya wao wakaendelea kwa nini sisi ni vipi tuzikatae wakati huko tulikotoka tumepasahau na hatuna namna ya kurejea .

Kama waafrika wangekua wamoja basi tusingekua na utitiri wa lugha ,makabila , dini ,mila na tawala tofauti zisizohusiana na mwingine.

Kama ungejua vizuri historia ya waafrika ungejua kuwa Afrika ni mahali ambapo vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya kabila moja na koo moja vilikua havikomi.

Vita za wenyewe kwa wenyewe ndizo zilizowapa nafasi wakoloni kuingia kirahisi Afrika. Kama ilivyo leo Pakiwa na kundi moja la watawala na marafiki zao au chama chao au kabila moja likiwanyanyasa Wengine inakua ni rahisi kwa adui kuja na kuahidi kumsaidia anayeonewa kumwangusha mwoneaji na kuungwa mkono.

Kabla ya mkoloni Mmanyema hajawahi kuwa chini ya mtawala mmoja na Mndengereko n.k. Kila mtu aliishi kwenye nchi yake na utawala wa kabila lake.
Huo ndio umoja unaosema!!!!

Kuna makabila yaligawanyika kabisa kabla ya kuja mkoloni Kwa mfano wachaga wa Kibosho na Machame walikua hawajengi hata nyumba zenye milango inayoelekeana kutokana na vita na uhasama. Ilikua ni mwiko kwa Mmachame kuoa mkibosho na kinyume chake.

Mpaka leo ukiondoa Polisi ya mkoloni kule Musoma Mjaluo na Mkuria hawawezi kuishi kwenye ardhi moja kamwe watauana mpaka waishe. Na sio kuwa wale wamshika sana dini za mkoloni la hasha wapo kiafrika zaidi.
Huo ndio umoja wa mwafrika unaosema!!!

Kabla ya mkoloni Wakurya na Wanyakyusa hawakuoana. Hapakua na hiari ya kufuata mila bali ilikua ni Lazima.
Usingeweza kusema kuwa sasa umeamua kuunda mila zako bila kufuata mila za mababu hata kama ni mbovu.
Watoto wengi waliuawa kwa sababu ya kuzaliwa wakiwa na utofauti Fulani kama alama nyeusi usoni,kuongea siku ya kuzaliwa ,kuanza kuota meno ya juu . Vidole sita kiganjani n.k. Wote waliuawa.
Hawa wengi ndio waliokua Magenus. Waliuawa na kutupwa porini.
Nakumbuka kuna Mzee mmoja aliwahi kunisimula kuwa kuna mzee mmoja alizaliwa akiwa na kialama kwenye sikio. Wakataka kumzamisha kwenye Kinu chenye maji cha kutwangia mahindi. Shangazi yake aliyetakiwa kufanya kazi hiyo akawa na wazo la kumficha.
Mtoto alipelekwa kwa mama yake kwa kificho na kuendelea kuishi.
Yule mtoto alipokua wakati huo wakoloni walikua wameingia alikua na akili na jasiri kuliko ndugu zake. Alianza kusoma akiwa na miaka zaidi ya 15 . Alisoma mpaka Darasa la Nane enzi hizo na kuwa Afsa wa kilimo kwenye mashamba ya Wazungu. Alimsaidia mama yake na ndugu zake. Ndiye pekee aliyesoma kwenye hiyo familia.
Tujiulize Mila zetu zilitumika kuua na kupoteza watu wangapi ambao leo wangekuwa ndio mwanga wa maendeleo ya Afrika na Dunia nzima.
Dunia nzima ilikua na mila za hovyo kabla ya kuja hizo unazoziita dini za ukoloni za Uislam na Ukristo.

Mkoloni hakumlazimisha mtu afuate dini yake bali dini hizo zilikua ni mahitaji ya wakati huo.

Sasa vipi dini za mkoloni! ziwe lazima wakati kila mmoja alifuata anayopenda mwenyewe?

Jeshi la mgambo dhaifu haliwezi kuteka ngome ya makomandoo.

Kama dini zetu zingekua bora zenye nguvu kubwa na imara tusingetawaliwa na kutekwa kirahisi ndani ya muda mfupi Afrika nzima ikagawanywa kama makundi ya kondoo wasio na mchungaji.

Unasema kuwa wale waliotuletea dini wameachana nazo .
Sina uhakika kama ni kweli mana nijuavyo Mimi ni kwamba dini ni matendo sio maneno tu. Siamini kuwa kuna sehemu yenye ukristu na mila zake kuliko Vatican au Uislam na mila zake kuliko Saudi Arabia.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom