Madhara au mateso yatokanayo na kubadili mfumo kutoka mfumo usio sahihi kwenda mfumo halali

Mc2nyi

Senior Member
Nov 5, 2013
190
185
Copied somewhere.

Credited below.

TAFADHALI SOMA UJUMBE WOTE UELEWE

GOVERNMENT SWITCHING COST: Madhara au mateso yatokanayo na kubadili mfumo kutoka mfumo usio sahihi kwenda mfumo halali,

Katika nchi ya Tanzania kumekuwepo na watu kuish kwa ujanja ujanja bila kufuata taratibu husika,
Short cut zilizojaa rushwa zilikithiri mpaka watu wakazoea kuish maisha ya ujanja ujanja, bila kufuata taratibu husika,
Ndiyo maana malalamiko ya ugumu wa maisha hasa kwa wajanja wajanja yameshamili.

Sasa katika nia ya dhati ya kubadili kutoka mfumo ujanja kuja uhalali,

Lazima waguswe wakwepa kodi, wauza pembejeo kwa upendeleo, wahujumu uchumi, wahujum hela ya mikopo ya elimu ya juu,

Kwa tathmin ya haraka inaonesha kuanzia mwaka 2007-2016 asilimia 74 ya watanzania waliishi maisha ya ujanja ujanja wa kukwepa kodi, au utapeli, au kujipa malipo yasiyo halali,

Asilimia 30% ya wachumi tanzania yaan wakubwa walikwepa kodi sana na kutokana na ukwepaji kodi wa hao watu ulinufanisha 90% ya watanzania kwa kupata bidhaa kwa bei ya chini kwa kuwa haikulipa kodi,

40% ya maliasili za Tanzania zilipelekwa bila kurekodiwa mahali popote ama kupitia njia ya anga , majini au ardhi, kubana maeneo haya kumesababisha tu sikilizie madhara ya Ku switch (kuhama) kutoka mfumo wa ujanja kwenda mfumo halali,

48% ya hela ya kwenye mzunguko haikuwa halali hii ilitokana na kutolewa mikopo ya biashara kutoka taasisi za serikali kwenda watu wasiostahili wasio na sifa stahiki,
Mishahara hewa ambayo iliwaendea watu ambao hawana sifa ya kuipata na saa Nyingine walipokea malipo zaid ya kazi walofanya, ilifanya mzunguko wa hela kuwa sivyo hela ilionekana kuwepo lakin baada ya kubanwa wakaumia wasio na nia njema na Tanzania, na madhara yake ni makubwa sana,

70% ya waliokuwa wanapata ajira hawakuwa na sifa stahiki, kigezo kilichotumika ni rushwa ,kujuana, na kupendeleana tu , wakati watu wenye sifa stahiki wanabaki,

60% ya bajet ya nchi ilitegemeam misaada bila kujua madhara yake,

UJIO WA MAGUFULI
Ujio wa bwana mkubwa huyu umesababisha hela yote hiyo kukauka maana haikuwa halali, madhara haya yakawa makubwa maana hakuna hela mtaani ni kwasababu hatujazoea kupata kipato halali, ni upigaji tu hivyo inakuwa ngumu kwa sasa kuendana na mfumo huu, na ajira za ngono ,kujuana , kupendelea hakuna tena hii imedababisha watu kusema hata hakuna ajira,

MUDA WA MADHARA
Muda wa madhara haya utaendelea kuwepo mpaka mwaka 2018 may ndipo watanzania watakuwa wemezoea kujipatia kipato halali, ndipo watanzania watakuwa tiyari wamezoea kuwa ajira so kujuana ni vigezo,

Ndipo watanzania watakuwa washajua kuwa ni lazima wawe na vigezo na kuimarisha vigezo vya kupata pesa toka taasisi husika, maana taasisi zilisitisha kwa muda kwa kuhofia wale wauza madawa ya kulevya, au wanaojilipa malimbikizo yasiyo na tija na kujipatia mikopo kama watapata fursa tena,

MAISHA KUWA MATAMU

Maisha ya watanzania yatakuwa mazuri kuanzia July 2018, maana watazoea mfumo na watakuwa wamesharudi kwenye msitari husika,

Vijana wengi watakuwa wameshajua kuwa siyo jukumu la serikali kuwapa ajira wahitimu wote,watakuwa wameshapata njia mbadala,

Huduma za jamii zitaimarika zaidi kutokana na vipaumbele vya bwana mkubwa kujikita kwenye Huduma za jamii kwa ujumla kuliko MTU mmoja mmoja,

YAPI YANGEKUWA MADHARA KAMA MAGUFULI ASINGEBADILI MFUMO?
1. Tanzania ingefilisika kwa kudaiwa kila sehem maana tungeshindwa hata kulipa madeni wanayotusaidia kujazia bajeti,

2. Tanzania ingekuwa mikononi mwa wagen zaid,kama kuwalipa fidia ya madeni wanayotupa kujazia bajeti, au kupitia misaada yenye mashart magumu, baadhi ya taasisi nyeti zingepaswa kuwekwa rehani,

3. Wizi au utapeli wa kimataifa miongoni mwa vijana wanaosoma na kupata elimu ya juu alafu nafasi zao zinachukuliwa na wasio na vigezo, maana hao ma IT na wana mitandao wangecheza na taasisi za fedha na miamala isiyo halali, na pia ingesababisha wenye akili mbadala.wengi mtaani,

4. Makundi ya vijana waliochoka maisha wangejitokeza na kuanza uarifu hadharani, na kusababisha uaribifu,

SIFA ZA WANAOMCHUKIA MAGUFULI

kama unamchukia Magufuli utakuwa katika kundi mojawapo hapa

1. Wakwepa kodi
2. Wahujumu uchumi
3. Wafanya biashara haramu,
4. Wajanja wajanja wasiopenda kufanya kazi,
5. Chuki binafsi tu
6. Wapinzani wanaotafta huruma ya wananchi , maana ni lazima wapinge,

Hayo ndo madhara ya SWITCHING,

TUVUMILIE NEEMA YAJA,

By
Raia Mpenda Haki
 
Unaujua mfumo sahihi wewe?? Mfumo sahihi wa kukwapua pesa wa wahanga?? Mfumo sahihi wa vitisho na ukandamizaji??

Mfumo sahihi wa kusema hakuna njaa wakati njaa inaonekana?? Mfumo sahihi wa kusema serikali haitoi chakula wakati chakula kimenunuliwa kwa kodi za wananchi!??? Mfumo sahihi wa kuwa na viongozi vigeugeu (refer ishu ya ewura)???

Mfumo sahihi unaoacha wananchi walipishwe madeni ya iptl na escrow??? Mfumo sahihi ambao kiongozi anasema hawezi fukua makaburi???

Narudia tena mfumo sahihi upi unao ongelea wewe kijana???

NB: mfumo sahihi hautokaa uletwe na viongozi wanaovaa nguo za kijani!!
 
Mimi ni nanacho amini hakuna mfumo hakuna mfumo haramu ilimradi wananchi wananufakia.
Tatizo Kubwa hapa ni mitazamo ya watu na fikra na jinsi kundesha mambo mbali mbali ya kiuchumi.
Kuna nchi ambazo wananchi na wawekezaji hawatozwi kodi ovyo na zinamaendeleo.

Kwahiyo serikali hii isitumie uchochoro huu kujitetea.
 
Katika haya nipe asilimia ya watanzania ambao wanafanya kazi na wanaotakiwa kulipa kodi

Kwa tathmin ya haraka inaonesha kuanzia mwaka 2007-2016 asilimia 74 ya watanzania waliishi maisha ya ujanja ujanja wa kukwepa kodi, au utapeli, au kujipa malipo yasiyo halali,
Hiyo asilimia hao fikiria marambili. Zaidi ya asilimia 50 wanafanya kazi katika sekta zisizo rasmi,wewe umeipata wapi hiyo?


Kati ya hawa uliowataja hapa na wananchi wa kawaida wapi wanaolalamikia maisha magumu?


1. Wakwepa kodi
2. Wahujumu uchumi
3. Wafanya biashara haramu,
4. Wajanja wajanja wasiopenda kufanya kazi,
5. Chuki binafsi tu
6. Wapinzani wanaotafta huruma ya wananchi , maana ni lazima wapinge,
 
Copied somewhere.

Credited below.

TAFADHALI SOMA UJUMBE WOTE UELEWE

GOVERNMENT SWITCHING COST: Madhara au mateso yatokanayo na kubadili mfumo kutoka mfumo usio sahihi kwenda mfumo halali,

Katika nchi ya Tanzania kumekuwepo na watu kuish kwa ujanja ujanja bila kufuata taratibu husika,
Short cut zilizojaa rushwa zilikithiri mpaka watu wakazoea kuish maisha ya ujanja ujanja, bila kufuata taratibu husika,
Ndiyo maana malalamiko ya ugumu wa maisha hasa kwa wajanja wajanja yameshamili.

Sasa katika nia ya dhati ya kubadili kutoka mfumo ujanja kuja uhalali,

Lazima waguswe wakwepa kodi, wauza pembejeo kwa upendeleo, wahujumu uchumi, wahujum hela ya mikopo ya elimu ya juu,

Kwa tathmin ya haraka inaonesha kuanzia mwaka 2007-2016 asilimia 74 ya watanzania waliishi maisha ya ujanja ujanja wa kukwepa kodi, au utapeli, au kujipa malipo yasiyo halali,

Asilimia 30% ya wachumi tanzania yaan wakubwa walikwepa kodi sana na kutokana na ukwepaji kodi wa hao watu ulinufanisha 90% ya watanzania kwa kupata bidhaa kwa bei ya chini kwa kuwa haikulipa kodi,

40% ya maliasili za Tanzania zilipelekwa bila kurekodiwa mahali popote ama kupitia njia ya anga , majini au ardhi, kubana maeneo haya kumesababisha tu sikilizie madhara ya Ku switch (kuhama) kutoka mfumo wa ujanja kwenda mfumo halali,

48% ya hela ya kwenye mzunguko haikuwa halali hii ilitokana na kutolewa mikopo ya biashara kutoka taasisi za serikali kwenda watu wasiostahili wasio na sifa stahiki,
Mishahara hewa ambayo iliwaendea watu ambao hawana sifa ya kuipata na saa Nyingine walipokea malipo zaid ya kazi walofanya, ilifanya mzunguko wa hela kuwa sivyo hela ilionekana kuwepo lakin baada ya kubanwa wakaumia wasio na nia njema na Tanzania, na madhara yake ni makubwa sana,

70% ya waliokuwa wanapata ajira hawakuwa na sifa stahiki, kigezo kilichotumika ni rushwa ,kujuana, na kupendeleana tu , wakati watu wenye sifa stahiki wanabaki,

60% ya bajet ya nchi ilitegemeam misaada bila kujua madhara yake,

UJIO WA MAGUFULI
Ujio wa bwana mkubwa huyu umesababisha hela yote hiyo kukauka maana haikuwa halali, madhara haya yakawa makubwa maana hakuna hela mtaani ni kwasababu hatujazoea kupata kipato halali, ni upigaji tu hivyo inakuwa ngumu kwa sasa kuendana na mfumo huu, na ajira za ngono ,kujuana , kupendelea hakuna tena hii imedababisha watu kusema hata hakuna ajira,

MUDA WA MADHARA
Muda wa madhara haya utaendelea kuwepo mpaka mwaka 2018 may ndipo watanzania watakuwa wemezoea kujipatia kipato halali, ndipo watanzania watakuwa tiyari wamezoea kuwa ajira so kujuana ni vigezo,

Ndipo watanzania watakuwa washajua kuwa ni lazima wawe na vigezo na kuimarisha vigezo vya kupata pesa toka taasisi husika, maana taasisi zilisitisha kwa muda kwa kuhofia wale wauza madawa ya kulevya, au wanaojilipa malimbikizo yasiyo na tija na kujipatia mikopo kama watapata fursa tena,

MAISHA KUWA MATAMU

Maisha ya watanzania yatakuwa mazuri kuanzia July 2018, maana watazoea mfumo na watakuwa wamesharudi kwenye msitari husika,

Vijana wengi watakuwa wameshajua kuwa siyo jukumu la serikali kuwapa ajira wahitimu wote,watakuwa wameshapata njia mbadala,

Huduma za jamii zitaimarika zaidi kutokana na vipaumbele vya bwana mkubwa kujikita kwenye Huduma za jamii kwa ujumla kuliko MTU mmoja mmoja,

YAPI YANGEKUWA MADHARA KAMA MAGUFULI ASINGEBADILI MFUMO?
1. Tanzania ingefilisika kwa kudaiwa kila sehem maana tungeshindwa hata kulipa madeni wanayotusaidia kujazia bajeti,

2. Tanzania ingekuwa mikononi mwa wagen zaid,kama kuwalipa fidia ya madeni wanayotupa kujazia bajeti, au kupitia misaada yenye mashart magumu, baadhi ya taasisi nyeti zingepaswa kuwekwa rehani,

3. Wizi au utapeli wa kimataifa miongoni mwa vijana wanaosoma na kupata elimu ya juu alafu nafasi zao zinachukuliwa na wasio na vigezo, maana hao ma IT na wana mitandao wangecheza na taasisi za fedha na miamala isiyo halali, na pia ingesababisha wenye akili mbadala.wengi mtaani,

4. Makundi ya vijana waliochoka maisha wangejitokeza na kuanza uarifu hadharani, na kusababisha uaribifu,

SIFA ZA WANAOMCHUKIA MAGUFULI

kama unamchukia Magufuli utakuwa katika kundi mojawapo hapa

1. Wakwepa kodi
2. Wahujumu uchumi
3. Wafanya biashara haramu,
4. Wajanja wajanja wasiopenda kufanya kazi,
5. Chuki binafsi tu
6. Wapinzani wanaotafta huruma ya wananchi , maana ni lazima wapinge,

Hayo ndo madhara ya SWITCHING,

TUVUMILIE NEEMA YAJA,

By
Raia Mpenda Haki
Acha mawazo mgando na finyu, umetumwa? Unataka kusema wote wanaolalamika ni wakwepa kodi, mafsadi au wajanja wajanja? Sahv kila sehemu wanalalamika unataka sema wote wapga dili? Bukoba 95% wanalia na mfumo huu nao wapga dili? Toeni siasa zenu za kijinga,

Sio kila mtu mwanasiasa, je huyo Aloktma umsifie anaongoza kwa kufata katba na sheria ilivyo? Je kuongeza mshahara kila July 1 ilikua mfumo mbovu? Ajira unasema hazikufata taratb je yy ameajiri lini kwa kufata taratb?

Kuna watu wengn kaz yao kusifia tu, IPO siku mtatiwa dole gumba msifie pia kuwa ndo mfumo mpya!
 
Hata Mfumo uwe mbaya namna gani lazima wawepo wanufaika na waathirika................Pia Hata Mfumo uwe Mzuri namna gani watakuwepo watakaoathirika na kunufaika......hapa Busara inatakiwa kuangalia wangapi(wengi) wananufaika hata kama Mfumo ni Mbovu......
 
Unaujua mfumo sahihi wewe?? Mfumo sahihi wa kukwapua pesa wa wahanga?? Mfumo sahihi wa vitisho na ukandamizaji??

Mfumo sahihi wa kusema hakuna njaa wakati njaa inaonekana?? Mfumo sahihi wa kusema serikali haitoi chakula wakati chakula kimenunuliwa kwa kodi za wananchi!??? Mfumo sahihi wa kuwa na viongozi vigeugeu (refer ishu ya ewura)???

Mfumo sahihi unaoacha wananchi walipishwe madeni ya iptl na escrow??? Mfumo sahihi ambao kiongozi anasema hawezi fukua makaburi???

Narudia tena mfumo sahihi upi unao ongelea wewe kijana???

NB: mfumo sahihi hautokaa uletwe na viongozi wanaovaa nguo za kijani!!
Kafe mbele huko l.o.f.a!
 
Acha mawazo mgando na finyu, umetumwa? Unataka kusema wote wanaolalamika ni wakwepa kodi, mafsadi au wajanja wajanja? Sahv kila sehemu wanalalamika unataka sema wote wapga dili? Bukoba 95% wanalia na mfumo huu nao wapga dili? Toeni siasa zenu za kijinga,

Sio kila mtu mwanasiasa, je huyo Aloktma umsifie anaongoza kwa kufata katba na sheria ilivyo? Je kuongeza mshahara kila July 1 ilikua mfumo mbovu? Ajira unasema hazikufata taratb je yy ameajiri lini kwa kufata taratb?

Kuna watu wengn kaz yao kusifia tu, IPO siku mtatiwa dole gumba msifie pia kuwa ndo mfumo mpya!
No 5 inakuhusu!
 
Hata Mfumo uwe mbaya namna gani lazima wawepo wanufaika na waathirika................Pia Hata Mfumo uwe Mzuri namna gani watakuwepo watakaoathirika na kunufaika......hapa Busara inatakiwa kuangalia wangapi(wengi) wananufaika hata kama Mfumo ni Mbovu......
No 2 inakuhusu!
 
Teh!

Eti maisha ya Watanzania yataanza kuwa mazuri kuanzia May 2018.

Nimegundua kitu kila serikali inayoingia madarakani inajaribu kutengeneza "uwongo" kupitia makosa ya serikali iliyopita ili kujitetea kwa wananchi wasioweza kuchanganua mambo.

Watu hawana maono yoyote kuhusu maisha yao kudanganya wengine kwao ni ushujaa. Lakini ni upuuzi tu mwisho wa siku


Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom