Madereva wasiowajibika watawaharibia SuperFeo

Madereva wasiowajibika watawaharibia SuperFeo

chakii

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2013
Posts
21,367
Reaction score
27,773
Habari wana JamiiForums

Kama inavyojulikana hapa Jamvini kwamba mimi ni mteja mzuri wa SuperFeo kwa route ya Dar Songea basi sitokaa kimya kuona wazembe wachache wasiowajibika katika majukumu yao hasa madereva wanaopakia roho za watu

Ni mwezi tu mmoja uliopita nikitokea Dar kuelekea Songea na basi la SuperFeo ambalo namba zake ninazo katika tiketi niliyosafiria kwa wahusika nitawapatia kwa hatua zaidi za kinidhamu

Kama inavyofahamika safari ya Dar kwenda Songea siyo safari fupi nikimaanisha inahitaji dereva zaidi ya mmoja ukizingatia ni basi la abiria ili waweze kusaidiana pale mmoja wao anapochoka

Katika hali inayoshangaza ni kwamba tangu Dar mpaka Songea alikuwa akiendesha dereva mmoja tu na mwenzake alikuwa akimpigisha stori tu na kulala

Hakika huku ni kuziweka roho za watu rehani kwani dereva hutokea kuchoka na hivyo kushindwa kulimiliki gari na hatimaye kupelekea ajali

Namshukuru Mungu tulifika salama lakini pia nisingependa hali hii itokee tena kwani ni hatari

Naamini wawakilishi wa Superfeo mpo humu Jamiiforum fanyieni kazi hili tafadhali
 
Naaamini ujumbe huu wameupata.hatari sana
 
Ebana dar songea ni mbali sana sasa kinachoniuma ni spidi kali hata kwenye miteremko..unaweza ukasali mpaka ukaonekana chizi
 
Tunaishi kwa mazoea, we nenda katupe tu hiyo tiketi kwasababu hakuna atakayeitaka kumuwajibisha dereva.

Wadosi wameshika ikulu.
 
Tunaishi kwa mazoea, we nenda katupe tu hiyo tiketi kwasababu hakuna atakayeitaka kumuwajibisha dereva.

Wadosi wameshika ikulu.

mkuu hii ni alert na siyo kwamba hakuna mabasi mengine yanafanya safari katika route hii

Endapo hali hii itatokea tena wawe tayari kupoteza wateja kwani hakuna mtu asiyejali roho yake
 
mkuu hii ni alert na siyo kwamba hakuna mabasi mengine yanafanya safari katika route hii

Endapo hali hii itatokea tena wawe tayari kupoteza wateja kwani hakuna mtu asiyejali roho yake

Sijakataa mkuu ila ninachojaribu kusema hata ukemee vipi serikali imelala usingizi wa pono. Wameshashikwa kila sehemu.
 
Kampuni inaendeshwa kiswahili. madereva wamejaa jeuri na dharau. kampuni inalangua sana nauli ya mizigo na parcel. management hamna pale.
 
Dar-Songea siku moja tu madereva wawili!!! Na keshoyake tena Songea-Dar tuamke wote tena? Tutapumzika lini sasa? Huoni kama namna hiyo ndo hatutapata muda wa kupumzika (na familia zetu pia) na tutasababisha ajali nyingi kwa kufikiria familia zetu badala ya kuconcetrate na kazi! Taratibu zetu: siku moja barabarani, siku moja off.
 
Wezi sana wa mida ya magari mengine na sumatra wanalijua hilo wapo kimya wamewekwa mfukoni.Magari yao mengi hayana timetable halali huku makampuni mengine madogo kwa njombe songea yakibanwa mbavu na hawa wanyonyaji
 
Back
Top Bottom