Madawa ya Kulevya: Wazazi Ndiyo Chanzo Kikubwa cha....

Je unakubaliana na hoja

  • Yes

  • NO


Results are only viewable after voting.

Kessy Wa Kilimanjaro

JF-Expert Member
Jan 23, 2016
327
208
Kuelewa Addiction ni vigumu kwa watanzania kama Makonda, kwasababu wengi wenu hamjasomea Psychology Ya watumiaji madawa na sababu zao za kutumia.

Msomi wa Addiciton Dr. Gabor Mate, anasema sababu kubwa kuliko zote za utumiaji wa madawa ni CHILDHOOD TRAUMA au CHILD ABUSE, Yani maisha yako utotoni na kilichotokea ambacho kiliko kuthuru kiakili.


Fact 1. ADDICTION NI UGONJWA WA AKILI!

Fact 2. Hamna Nchi ambayo imeweza kupambana na madawa ya kulevya na ikamaliza hii vita kwa kutumia nguvu bila psychology.

Fact 3. Madawa ya kulevya siyo mwanzo wa tatizo bali ni matokeo ya tatizo kubwa zaidi ambalo ni wazazi wabaya. (BAD PARENTING)

Fact 4. Watumiaji madawa ni watu ambao tayari maisha yao hayana maana, na hawana muelekeo wa mafanikio kabla hata ya kuanza kutumia madawa.

Fact 5. Kila mtumiaji madawa au kila mtu mwenye ADDICTION yeyote ile iwe kazi, pesa, pombe, pornography, ngono, e.t.c akienda kwa psychologist inajulikana kwamba alikuwa na malezi mabaya au alifanyiwa uovu utotoni.



Hii video hapa juu ni documentary inayomfwata msichana ambaye alikuwa amebakwa na mtu ambaye alitakiwa kumlea na kumtunza. Huyu msichana akaishia kutumia madawa.



Hiyo video ni mfano mmoja ya watu wanaotumia madawa wanatoka kwenye maisha gani. Tunahitaji kuelewa kwamba hawa watu walikuwa watoto ambao walifanyiwa vitendo viovu utotoni au hawakupendwa na kulelewa kwa umakini na wazazi wao ndio wanaishia kwenye madawa.

KAMA TUNATAKA TUONDOE UTUMIAJI MADAWA TUNAHITAJI KUPIGANA VITA NA UZAZI NA ULEZI MBAYA.

TUSIPIGE WATOTO WETU BALI TUWALEE KWA HEKIMA.

TUWE WAANGALIFU JUU YA WATU AMBAO TUNAWAACHIA WATOTO WETU WAKAE NAO.

TUHAKIKISHE KWAMBA WAZAZI WOTE WAWILI, BABA NA MAMA WAPO NYUMBANI NA WANAMPENDA NA KUMLEA MTOTO KWA HEKIMA.
 
Back
Top Bottom