Madaraka CCM, Uongozi CDM

Jazzie

Member
Jan 30, 2008
73
35
Hata siku moja sikudhani nitashuhudia haya yanayotokea Tanzania – kwamba kuna watu wako madarakani lakini si viongozi.

Kilichotokea bungeni hivi karibuni, ni hitimisho ya kile ambacho kilikuwa kimeanza kujitokeza, kwamba CCM wana mamlaka ya kuongoza nchi, lakini wameishiwa haki ya uongozi. Uongozi, ninavyoelewa mimi ni kuwa mstari wa mbele katika kujielekeza mwenyewe, kundi fulani, au jamii nzima kuelekea mahali ambapo pameainishwa wazi (leadership is directional, with a clear definition of a desired destion). Kwa Tanzania, safari yetu ni kuelekea katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Sehemu ya uongozi, kwa maana hiyo, ni kuwa mstari wa mbele katika uhodari, mawazo mapya, maono, mikakati, kutia moyo (inspiration) na kadhalika. Kinachotokea sasa hivi ni CCM kusubiri CDM waongoze nchi. Kama hiyo si kweli, ni lini (hasa siku za karibuni), umesikia wazo jipya limetoka ndani ya CCM? Ni lini, siku za karibuni, umetiwa moyo na CCM kama Mtanzania?
 
Hata siku moja sikudhani nitashuhudia haya yanayotokea Tanzania – kwamba kuna watu wako madarakani lakini si viongozi.

Kilichotokea bungeni hivi karibuni, ni hitimisho ya kile ambacho kilikuwa kimeanza kujitokeza, kwamba CCM wana mamlaka ya kuongoza nchi, lakini wameishiwa haki ya uongozi. Uongozi, ninavyoelewa mimi ni kuwa mstari wa mbele katika kujielekeza mwenyewe, kundi fulani, au jamii nzima kuelekea mahali ambapo pameainishwa wazi (leadership is directional, with a clear definition of a desired destion). Kwa Tanzania, safari yetu ni kuelekea katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Sehemu ya uongozi, kwa maana hiyo, ni kuwa mstari wa mbele katika uhodari, mawazo mapya, maono, mikakati, kutia moyo (inspiration) na kadhalika. Kinachotokea sasa hivi ni CCM kusubiri CDM waongoze nchi. Kama hiyo si kweli, ni lini (hasa siku za karibuni), umesikia wazo jipya limetoka ndani ya CCM? Ni lini, siku za karibuni, umetiwa moyo na CCM kama Mtanzania?
Punguza ndumu na ganja!!
 
Back
Top Bottom