Madalali: Houses, Apartments, Shop frames na Office spaces

Madalali: Houses, Apartments, Shop frames na Office spaces

makohnstruct

Member
Joined
May 8, 2015
Posts
28
Reaction score
7
Habari wana JF na wote mlioamua kutumia muda wenu kupitia uzi huu.

Sisi ni wakala ambao kwa sasa tunapatikana jijini Dar es Salaam.
Katika awamu ya kwanza, tunafanya shughuli zetu katika maeneo ya Kinondoni, Upanga, Kariakoo na mjini kati. Na kwa kiasi fulani tumejitanua kuelekea mikoa ya Pwani na Morogoro. Kazi zetu tunafanya kwa ueledi na umakini wa hali ya juu.
Zaidi ya hapo tunamsikiliza mteja na kumjali yeye, muda wake, pesa na mali yake.

Tuna nyumba, apatimenti, ofisi, na fremu za maduka zilizo wazi na zinahitaji wapangaji na wanunuzi, katika maeneo tajwa hapo juu, pia maghala sehemu mbalimbali za jiji, bila kusahau viwanja na mashamba. Isitoshe tunapokea oda kwa wahitaji wa mali.
Pia tunakaribisha wamiliki wenye mali tajwa hapo juu katika maeneo tajwa hapo juu au mengineyo kuingia makubaliano na sisi ili tuwatafutie wateja kwani tunatumia teknolojia ya mawasiliano rahisi na ya kisasa kuweza kuzitangaza mali zao na hatimaye kupata wateja.

Kwa yeyote mwenye uhitaji asisite kupiga simu/whatsapp namba +255786157788.
Wote mnakaribishwa. Asanteni.
 
Labda nikufahamishe jambo. Dalali hamiliki mali kwamba anahitaji mteja na wala si muhitaji wa mali.
Mara nyingi kinachotokea, ni dalalali kupokea taarifa zisizo sahihi bila kufahamu kuwa taarifa hizo si sahihi na kuanza kuzinadi upande wa pili katika hali ya usahihi na kuaminika. Pindi biashara inapokuwa imefanyika na ikabainika haikuwa sahihi, mtu wa kwanza kuhusishwa ni dalali. Mpikaji wa tukio ambaye anaweza kuwa mmiliki, ndugu au jamaa wa karibu wa mmiliki huwa hawatazamwi kwa jicho baya kama ilivyo kwa dalali.

Karibu sana gambagumu na pole kama yalikufika.
Nina miaka mitatu katika kazi hii na sijawahi kumkwaza mteja wangu yeyote mpaka sasa ninavyoelekea kukamilisha usajili wa kampuni yangu ya udalali.
 
Nahitaji fremu nzuri sana na kubwa ambayo ipo sehemu nzuri na yenye mchanganyiko wa watu je unazo na kama unazo je ni wapi hasa??
 
Udalali bongo ni utapeli kamili

GAMBAGUMU sio kweli mimi ni dalali nanunua viwanja na kuuza pia nawasaidia watu wengine kuuza viwanja kwa kufanya utafiti kuhusu umiliki na uhalali kabla ya kununua na kuuza,lakini nimeajiriwa ajira ya kudumu ya serikali,mtumishi wa umma,kwa upande wangu udalali sio utapeli
 
Studio apartment upanga kwa 500k inapatkana? Na kkoo ya lak3 kushuka chin? Isiwe zaidi ya ghorofa ya Tatu kama hakuna lift.
 
Studio apartment upanga kwa 500k inapatkana? Na kkoo ya lak3 kushuka chin? Isiwe zaidi ya ghorofa ya Tatu kama hakuna lift.

Kwa sasa iliyopo ni yenye fenicha, Upanga. Hii inataka dola 750 kwa mwezi. Pia isiyokuwa na fenicha, Kariakoo. Hii ni 400k kwa mwezi.

Kwa ofa uliyoitoa bado inapelea hata kukiwa hakuna fenicha, hasa hiyo ya Kariakoo.
Pamoja na hivyo ntaendelea kutembeza msako, huenda nikabahatika kupata.
 
Kwa sasa iliyopo ni yenye fenicha, Upanga. Hii inataka dola 750 kwa mwezi. Pia isiyokuwa na fenicha, Kariakoo. Hii ni 400k kwa mwezi.

Kwa ofa uliyoitoa bado inapelea hata kukiwa hakuna fenicha, hasa hiyo ya Kariakoo.
Pamoja na hivyo ntaendelea kutembeza msako, huenda nikabahatika kupata.

nataka isiyo na furniture mkuu, chumba kimoja (hata viwili) cha kulala, sebule jiko, parking hata kama ya kulipia.
 
Natafuta frame/ofisi kubwa na isizidi laki tatu kwa mwezi.... eneo lolote kati ya hizo ulizo taja isipokua kko.
 
Back
Top Bottom