Wewe PakaJimmy, is this Monday, a Blue Monday to you? Mbona leo umemiss point? Serikali, ndiyo agents of the Devil, wao ndiyo wana wa kuzimu! Serikali, ndiyo accountable, kwa vifo vitakavyotokea!
Kumbe, unajua, na Serikali inajua kwamba Madaktari wakiacha kazi siku moja tu, watakufa watu wengi! Kama ni hivyo, ebu sasa tujadili!
Unajua kwamba Mbunge Sumari tangu achaguliwe na watu wa Jimbo lake, huko Arumeru, hakuweza kufanya lolote huko, kwa sababu ya ugonjwa? Je, ni watu wangapi walikufa katika Jimbo lake, kutokana na kukosa huduma ya Mbunge wao?
Vivyo hivyo, ni nani amekufa katika Wizara ya Maji, kutokana na kukosa huduma ya Waziri wa Maji, Profesa Mwandosya, ambaye hajaweza kufanya kazi, kwa miezi mingi? Kwa zaidi ya mwaka mmoja, wilaya nyingi, hazina Wakuu wa Wilaya. Nani amekufa, kwa kukosa huduma za Wakuu hao wa Wilaya?
Kama Jibu ni HAKUNA, basi Tanzania tujifunze kuwaheshimu Madaktari, kama wanavyowaheshimu, nchi nyingine. Serikali iache kutoa mishahara na posho nzuri, kwa wanasiasa wapiga porojo; na kupuuza maslahi ya Madaktari. Madaktari huko Marekani, wanalipwa kati ya 60 - 100$ kwa saa moja, kulingana na fani zao! Sawa, sisi hatuwezi kulipa mishahara hiyo; lakini Serikali iwalipe vizuri zaidi, kuliko wanasiasa. Madaktari msirudi nyuma katika mgomo wenu. Nchi hii, haki haitolewi katika kisahani, bila fight!
acha pumba wewe,,,umeng`ang`ania kodi....kodi...kodi.....hakuna mtanzania asiyelipa kodi,,, huo mshahara daktari hapati bure hata kama ni kodi yako analipwa kutokana na cheti cha elimu yake na kazi aliyofanya hapewi zawadi ya bure... Na yeye analipa kodi tena yenye risiti kila mwezi....... Hakuna aliyeletwa duniani kuja kukuhangaikia wewe bila malipo ya stahili yake.......kumwambia mtu eti sababu alichagua kazi fulani ndo aishi maisha ya chini si jibu la kuondoa tatizo ni ujinga wa ufupi wa mawazo,... Hakuna anayetaka kutajirika kupitia mshahara,,,, watu tunataka mazingira mazuri ya kazi,, na hata huo mshahara uongezwe kiasi kwamba mtu apate mahitaji yake.......udaktari tabibu ni noble profession na mgomo ni upuuzi ukizingatia wamekula kiapo kwa mungu. Serikali imewasomesha buree wakati watanzania wengine wanalipa kila kukicha. Hizo ni kodi za watanzania. Walipe fadhila kwanza. Waache upuuzi. Kama wanataka maisha ya hollywood wabadilishe fani and it is too late now!! Hii ni ndoa na wanatakiwa kuitumikia kwa uadiilifu. Kama ni mgomo ungepaswa sis walipa kodi. Hadi hiyo mishahara yao ni kodi zetu. Na hata maboresho ya huduma ni kodi zetu pia. Sasa tutawasaidia mpaka lini. Acheni upumbaf fanyeni kazi ya ujenzi wa taifa hadi pesa zipatikane tutawaangalia mbeleni.
kumbe si mimi pekee nimwonavyo hivyo....... Kweli lipunguani hili...inawezekana akili yako haina akili ndugu
kada zingine za afya ni waoga kupindukia sababu ya idadi yao ndogo..... Kama wewe ni kada wa afya bila kigwangala na wenzake wa inten kugoma we usingekuwa unalipwa huo msahara wako wa sasa...... chunga domo lako kama si mkono wako. ...Walikimbia kazi baada ya kuona ufirauni unaofanyika na waliobaki ni kwamba wamekosa pa kwenda.....sekta ya afya haiongozwi na madaktari tu ni upuuzi wa madaktari kutusemea sisi watumishi wa kada zingize za afya ambao hatujashiriki mikutano yao kifupi wamechumka na kesho watafanya kazi tu hao ni wababaishaji wanadanganywa na madaktari waliokimbia kazi zao kama kingwangala na mpiga domo wa clouds fm maroo
hiyo ndo ngao ya wanasiasa,,,, innocent tanzanians???????kieleweke at the cost of lives of innocent tanzanians?
hebu eleza ni mazungumzo yapi yaliwahi kuleta suluhu ya shida za wafanyakazi wa umma tanzania bila harakati kama hizi?........mipango hii inaendelezwa na wasioitakia mema tz kwa kuwashawishi watumishi wote wa sekta za huduma za jamii zigome ili kuichanganya serikali na kutotaka kutumia utaratibu uliomo kwenye sheria pamoja. Mazungumzo yanafaa zaidi lakini wahusika wanalipwa kukataa kila aina ya suluhu toka serikalini. Mafisadi wakuu wana mkono katika migomo hii kila sekta!!
Kieleweke at the cost of lives of innocent Tanzanians?
Hivi serikali ipo wapi jamani ???usalama wa taifa hamuwashauri viongozi kumaliza migogoro kama hiyo?hamjui kuwa ndio chanzo cha usalama wa taifa zima kuwa mashakani??au nyie mnasubiri kusindikiza viongozi tu!??washauri wote na vyombo dola mnaogopa kutekeeleza wajibu wenu kushauri viongozi....PM ameshindwa kwenda na Katibu Mkuu kuongea nao hadi watu wafe waunde tume?mlikimbilia nini ikulu kama mnaogopa vivuli vyenu??
Ndugu inaelekea huna historia kamili kuhusu migomo,mwaka 1995 madaktari na wauguzi wote nchini waligoma kwa siku tatu na aliyekuwa waziri wa afya wakati huo Bi Zakia Meghji aliachia ngazi na ilibidi mh. Rais Mwinyi wakati huo awafuate kwenda kuwasihi warudi kazini na mara moja maslahi yao yalishughulikiwa yote kama walivyotaka, maiti zilinuka mawodini kulikuwa hakufai usifanye mzaha na migomo yao!
migomo sio njia nzuri ya kudai haki.
Unataka kusema sekta ya afya in wajinga?Madhara ya serikali legelege ndiyo hii imeonekana wazi.
Ngoja sasa ndg zetu waliolazwa mahosptalini wakose huduma hata ya drip hala wizara husika ijisikie vizuri!
Sekta lengwa ni Wajinga wakubwa sana!