raybse
Senior Member
- Oct 22, 2010
- 104
- 14
Lile sakata la Madaktari na Serikali Limefikia Madaktari Kuamua Uamuzi Mgumu wa Kuamua Kugoma rasmi kuanzia Kesho hii ni kutokana na Mikutano waliyoianza toka jumatano ya wiki iliyopita ya kujaribu kutafuta suluhu ya matatizo yao na Sekta ya Afya kwa Ujumla,Juhudi hizo hazikuzaa matunda kutoka kwa Serikali kuanzia ngazi ya Wizara ya Afya mpaka ofisi ya Waziri Mkuu ambapo.
Madaktari hao wana madai kadhaa ikiwemo Kuboresha Huduma za Afya nchini na Maslahi Duni kwa watumishi wa sekta ya afya ikiwa ni pamoja na kufanya Kazi katika Mazingira Magumu, Lingine ni Kuondolewa kwa Katibu mkuu wa wizara ya afya Bi.Blandina Nyoni.
Maamuzi hayo magumu yamefikiwa katika Mkutano wa leo uliofanyika Don Bosco Upanga DSM ikiwa ni mwendelezo wa Mikutano isiyokoma iliyoanza Toka jumatano ya Wiki iliyopita.
Madaktari hao wana madai kadhaa ikiwemo Kuboresha Huduma za Afya nchini na Maslahi Duni kwa watumishi wa sekta ya afya ikiwa ni pamoja na kufanya Kazi katika Mazingira Magumu, Lingine ni Kuondolewa kwa Katibu mkuu wa wizara ya afya Bi.Blandina Nyoni.
Maamuzi hayo magumu yamefikiwa katika Mkutano wa leo uliofanyika Don Bosco Upanga DSM ikiwa ni mwendelezo wa Mikutano isiyokoma iliyoanza Toka jumatano ya Wiki iliyopita.