MADAKTARI Ungeni MKONO MABADILIKO YA UONGOZI KISIASA sio kudai mishahara kila siku(think bigger)

fikirikwanza

JF-Expert Member
Jan 25, 2012
7,452
3,065
Mgomo wa madaktari,tatizo hili ni kubwa mno hapa Tz. Hivi unaweza kueleza kitu gani watu wakakuelewa juu ya madakatari kuomba waongezewe mishahara, huu ni usaliti tena mkubwa. Tuko kwenye mapambano ya ukombozi harafu kundi moja la wasomi wanaomba mafao kwa ajili yao pekee yao??? aibu kwako.

Ushauri wangu madaktari waache kufanya haziwatoshi, waungane na kada zingine kuendeleza mapambano ya kuiondoka CCM madarakani, sio kuomba mishahara mikubwa. Kwa hali ilivyo sasa kuomba kuongezewa mishahara na CCM ni usaliti, rushwa na vitu vya aina hiyo.

Madaktari gomeeni CCM iondoke madarakani sio mafao yenu peke yenu huku waliowafundisha wako hoi, wanaolima kile mnachokula wako hoi, wanajenga hizo hospitals zenu wako hoi, wanaolinda na kuwalinda nyinyi usalama wa raia wako hoi, wavuvi wako hoi, wafugaji ambao ndo mwala nyama wako hoi, wanatengeza/repair tools za kufanyika kazi zenu wako hoi, think bigger please, tudaini CCM iende OUT of power kwanza, mishahara baadae itanyoka, ni kama kansa dawa ni kukata sehemu iliyoathirika sana ili mgonjwa apate tiba, sasa nyinyi wakubwa mnafanyaje hivyo??? Mbona kinyume kabisa na concept ya kansa iliyokomaa, au bado mnadhani CCM inaweza kuboresha maisha yenu??

Nitashangaa kama jibu ni ndio!!!


Nawasilisha.
 
Back
Top Bottom