Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Nikitazama milima ya kwetu eh eh
Machozi yanitoka kwa uchungu na mawazo,
Tulikuja wawili ninarudi peke yangu
Baba na mama wataniuliza mke wako yuko wapi eh eh eh
Ndugu jamaa wataniuliza mke wako yuko wapi eh eh heeee
Nitasema nini kwa mama mimi mwenzenu eeee
Nitasema nini kwa baba mimi najuta eeee
Harusi ilifanyika kwa sherehe kubwa sana ooooh watu alikunywa, kula na kusaza maaamama
Nikaenda kuishi na bibi yule mjini kazi yake ilikuwa ni vitukooooo eh
Alianza kuweka sukari kwenye mboga nikashindwa kula nialala na njaaa
Siku nyingine akaweka tui kwenye chai kulikuwa na wageni wakatoka bila kuagaaaa
Kuna siku alivunja kioo cha dirisha ili apate kuchungulia wapitao njiani .
Nilishindwa kumuuliza eh, sikutaka nimuudhi, sababu nilikuwa nampenda nampenda saaaaana .X 2
Kiitikio ..
Walesemaaa dalili ya mvua ni mawingu niliyempenda kanitoroka maaama
Kanitoroka masikini mimi .
Walesemaaa dalili ya mvua ni mawingu niliyempenda kanitoroka maaama
Vitukoo eh vituko vya bibi yule .Pole sana
Sitoweza kusahau mimi oooh Eddy eeeh
Sitoweza kusahau mimi oooh mama oooh
Alikuwa kama helikopta ndege isiyochagua mahali pa kutua eeeeh
Kila mtaa hapa mjini jamani tazameni oooh,
Nasononeka jamaaaa ..
Kiitikio ..
Walisemaaa dalili ya mvua ni mawingu niliyempenda kanitoroka maaama
Kanitoroka masikini mimi
Walesemaaa dalili ya mvua ni mawingu niliyependa kanitoroka maaama
Wimbo huu uliimbwa na bendi ya Super rainbow ---Eddy Sheggy
Huu wimbo nimeukumbuka sana leo.