Jina lako lipo tofauti na unayosema, sisi wapiga kura tunataka wabunge wapinzani waongezeke halafu wewew unashauli wapungue!!!!Binafsi, nachukua fursa hii kumpongeza Mh. MACHALI kwa msimamo wake wa kuapa kujiuzuru ubunge na uanachama wa NCCR iwapo Kafulila atakuwa mwenekiti wa chama hicho, unajua watu wengi hamjui kafulila na tabia zake mbaya, wala huyu hana uzalendo hata kidogo
ni mr.misifa yaani hupenda kusema tu ili aonekane amesema lakini ukija katika suala la utekelezaji wa mipango yake ni ziro kabisa. Nawashauri kumuona kafulila sawa na matapeli wa kisiasa,si mfano wa kuigwa. Kwa upande wa machali aka JEMBE yaani mtu anayependa kusema ukweli daima aungwe mkono, huyu jamaa siyo mbabaishaji hata kidogo ni mtu anayependa kufuatilia mambo kuliko Kafulila, hebu anza tu kufuatilia sifa zao kitaaluma utabaini kuwa Kafulila alitoroka hata chuo,elimu yake mnaijua?muulizeni muone kama atawaambia labda anaweza akawaambia kwa sababu nimechokoza hilo,ni mbabaishaji tu na ndiyo maana anawakimbia hata watu wake jimboni,
hana uwezo wa kujadiliana ni mnafiki wa kupita kiasi.Zipo taarifa kuwa yeye na Hashimu Rungwe wamepata fedha za CCM ili kuhakikisha mbatia nang'oka kwenye uenyekiti eti kwa sababu mbatia kashitaki Benki ya moja inayotetewa na kampuni moja ya kiwakili ya watu wa CCM. Wasiyeyushe hoja, wahojini wamepata wapi hela za kununua wajumbe wa NEC ya nccr?
Aidha siku moja Mh. MACHALI alipata kudai kuwa tayari kafulila alikuwa amemwomba washirikiane kumng'oa Mbatia lakini kwa kuwa machali ni ANALYST wa mambo kitaaluma huwa hakurupuki, alimshauri kafulila haraka ya nini kutaka Mbatia aondoke kwa vurugu?una ajenda gani,Oooh!mimi nataka niwe m/kiti(kafulila huyo)halafu wanasiasa wengi watahamia kwetu na tutajenga chama na kwa hiyo kuna watu wengi wanatuunga mkono wakiwemo akina hashimu Rungwe nk. Kwa hiyo wewe niunge mkono.
MACHALI AKAMJIBU "SIWEZI KUWA CHIMBUKO LA VURUGU ZISIZOKUWA NA FACTS. Nenda katafute hoja nyingine na ukipata sababu za kutosha ndiyo uje", Kiukweli Machali anapaswa kuungwa mkono kwa msimamo wake, hatupaswi kumbeza kama anavyofanya Kafulila kwa kusema kuwa Machali ni mwoga na eti apambane akiwa humohumo nccr.
Kusema hivyo ina maana tunabariki wana ccm na wale wote waliowahi kuwa ccm warejee ccm wakendeleze kupambana humohumo ccm. Wazo la Kafulila limefulia kweli kama jina lake lilivyo, anataka kutushawishi na sisi wana harakati kuwa ccm siyo tatizo, Kimsingi KAFULILA awapelekee ndugu zake hiyo hoja ya kutaka, KAMANDA machali abaki nccr wakati kafulila au Rungwe akiwa mwenyekiti. NAKUBALIANA NA DR. SLAA KUMUITA kafulila SISIMIZI, hakika anfikiria kisisimizi sisimizi.
Ndio maana aliwahi kumsifia KIKWETE Kuwa ndiye Rais bora aliyewahi kuujali mkoa wa kigoma, anamsifia kikwete kwa mema yapi kwa wana kigoma. Kafulila CCM kwelikweli tena CCM "A",halafu huyu jamaa ndiye anayetaka kuwa Mwenyekiti wa NCCR, amefulia kwelikweli na hii ni aibu hata kwa wale wote wanaomfagilia kafulila huku wakijua kuwa ni mtu wa kuzungumza tu huku akiwa siyo mtendaji. Anafagilia CCM Kama hajui ccm NDIYE MCHAWI wa sis kuwa masikini katika hii miaka 50 ya uhuru.
Machali amenena sawasawa kuwa Kafulila na wafuasi wake wakifanikiwa kuingia kwa fujo kabla ya muda kufika ajiuzuru, hakika bravooooooooooooo kwa machali na hii itatoa mwanga na kuwakumbusha watu kuwa ni ujinga na upumbavu kukubali kufanya kazi chini ya mtu ambaye unajua kuwa hafai hata kidogo katika tasisi moja kama kafulila, Inawezekana ni kafulila kaandika hii post hapa JF na kujificha ili aone kama watu tutagilia, hatufagilii ujinga sisi, tunamshauri kafulila arudishe akili zake nyuma akatafakari juu ya yeye kuwa Bw. MITAFARUKU kila anapokwenda alipokuwa CHADEMA vurugu, NCCR vurugu.
Ametumwaa na ccm kuuua upinzani,hafai hata kuwa mkuu wa familia.
Huoni kuwa wakipungua NCCR itapoteza ruzuku na jimbo litakwenda CCM na Mbatia atapoteza nafasi ya Mwenyekiti!!!
Ndiyo maana nikasema tuwe wakweli kutoa Mawazo sio kukurupuka watu wanatufuatilia afya zetuni ili kupima uwezo wetu!!!???