Machali anavyomchana Kafulila

Machali anavyomchana Kafulila

Mbona haikai vizury akilini...huo ndo uandishi wa barua bila shaka kuna harufu ya uzushi
 
Sina hakika na authentisity ya nyaraka hizi,lakini haya ndiyo machali anayoyafichua huku Mwanza,kama ni kweli daaa kafulila hakuwa amejipanga

machali mambo yake yamemushinda anachana ya wengine
ona haya yanayotesa watu wake
mosi rushwa ya waziwazi ya tanesco kuweka nguzo mpaka utoe hongo
aacha imebaki ni kazi ya wananchi wake wa kafurila chama kilishafanya maamuzi wananchi watatoa yao woga wote wa nini?
 
Kwa mujibu wa Machali, Kafulila ndiye aliyeshinikiza James Mbatia afungue kesi dhidi ya Halima Mdee halafu sasa anageuka
 
Chigwiye na Wana JF,
Hizi ni Siasa za kinafiki, pande zote 2 zina mapungufu, ni busara tu ndio ingetakiwa kuchukua na Maslahi ya Taifa kuwekwa mbele.
Nawakilisha



Sina hakika na authentisity ya nyaraka hizi,lakini haya ndiyo machali anayoyafichua huku Mwanza,kama ni kweli daaa kafulila hakuwa amejipanga
 
Huyo Machali huenda 2015 hatagombea tena huko Kigoma ambako NCCR haitakiwi tena. Huenda kwenye mabadiliko ya katiba kutakuwa na vitu maalum kwa wanaume pia. Atasubiri Mbatia amteue, zaidi ya hapo na yeye asubiri kichapo cha kura.
 
Wanachokifanya NCCR Mageuzi ni upuuzi mtupu, niliwafuatilia vizuri akina machali star tv lakini nikagundua migogoro yote ni sababu ya chuki binafsi, na tamaa ya madaraka.Kama kweli kafulila aliwaomba msamaha kama vimemo vyao vinavyoonyesha walishindwa nini kumsamehe mbona hata Mungu anatusamehe.Walichokifanya kinawaua kisiasa wenyewe 100%.Mimi kama mtanzania halisi sipendelei vyama vyenye migogoro.Pia kama mliombana msamaha hiyo ni siri yenu na chama chenu si vyema kuja kutuonyesha mambo yenu ya ndani.Ukimuacha mke au Mme si busara kuanika udhaifu wake wa ndani mpaka mlivyoombana msamaha hadharani, kwa kufanya hivyo nadhani hata wewe mhusika utakuwa na matatizo makubwa kifikra na kimawazo.
 
mmmhhh..... Mie haya siyawezi. Hivi mwenzako akikuudhi ni vizuri kumwambia ndo maana ulitemwa na demu wako au ndo maana mke wako alimegwa na mchungaji?. machali akili yake ni ya jinsia ya upande wa pili.
 


KATIBU Mwenezi wa NCCR Mageuzi Taifa Mbunge wa Kasulu mjini mh. Moses Machali amesema kuwa kuendelea kuwepo kwa mbunge aliyetimuliwa uanachama hivi karibuni David Kafulila ndani ya NCCR Mageuzi ni sawa na kuilea kansa .

Machali ameyasema hayo jana katika mkutano wa NCCR Mageuzi uliofanyika katika uwanja wa Sahara jijini Mwanza uliokuwa na lengo la kuimarisha chama hicho.

Katibu huyo mwenezi wa NCCR Mageuzi amemtaja David Kafulila kuwa ni 'mpuuzi na kigeugeu' kwani ndiye aliye mshauri Mwenyekiti wa Chama hicho James Mbatia kufungua kesi dhidi ya Mbunge wa jimbo la Kawe Halima Mdee aliyemtolea maneno ya kashfa kipindi cha mchakato wa uchaguzi na ndiye aliye mshutumu Mbatia kwa kufungua kesi hiyo dhidi ya Halima Mdee.

Akithibitisha kuwa Mbatia hakuwa na nia mbaya kufungua kesi kama inavyotajwa na Kafulila, Machali alisema kuwa kabla ya kufungua kesi hiyo Mbatia alimwambia Mdee "ukiniomba radhi na kunisafisha kwenye vyombo vya habari sina tatizo na wewe, Halima Mdee akajibu kuwa ukienda mahakamani nitakwenda kukuvua nguo huko huko.

James Mbatia kwa ushauri wa Kafulila akafungua kesi mahakamani lakini mara baada ya kufungua kesi Kafulila ndiye aliyekuwa wa kwanza kumshutumu Mbatia kufungua kesi dhidi ya mpinzani mwenzake na kumtaja kuwa ni kada wa Chama cha mapinduzi (CCM)"

Katibu huyo mwenezi alisema kuwa Kafulila alishamwambia nia yake ya kuukwaa uenyekiti wa NCCR Mageuzi na kwa kuwa alikuwa na ajenda hiyo alianza kumzushia mambo mbalimbali bwana James Mbatia, jambo la kwanza likiwa ni kumtaka mwenyekiti huyo kujiuzuru kwa kushindwa kukiendeleza chama hali inayokifanya kizidi kudidimia.




"Nikamwambia Bunge la 9 lililoishia mwaka 2010 NCCR ilikuwa haina hata mbunge mmoja bungeni leo tuna wabunge wanne chini ya uongozi wa Mbatia, nao wananchi wa Kigoma wamekuamini kwa kampeni na nguvu za huyo huyo Mbatia"
"NCCR ilikuwa na madiwani 19 nchi nzima leo tuna madiwani zaidi ya 40 je haya siyo maendeleo?" alisema Machali kisha akaongeza...
"Nikamwambia, NCCR ilikuwa ikipata ruzuku ya shilingi milioni 1.2 kwa mwezi lakini leo kutokana na idadi ya madiwani kuongezeka tunapata shilingi milioni 12 kwanini tusiige mfano wa wenzetu CHADEMA kwa sisi wabunge wanne tukafanya kazi ya kuaminika majimbo mbalimbali tukaongeza idadi ya majimbo wewe unaanzisha chokochoko zisizo na tija bali kukivuruga chama?"

"Akaniambia 'Ndugu yangu, kaka yangu machali shida yangu ni Uenyekiti' "
"Nikamwambia uenyekiti hautafutwi hivyo subiri 2013 tutakwenda kwenye uchaguzi wa chama wanachama wakikuamini watakupa nafasi"

"Akaniambia 'Achana na mimi' " na ndipo alipoanza kuwarubuni makamishina mbalimbali akiwaambia kuwa ANATAKA KUFANYA MAPINDUZI NDANI YA CHAMA....

Mh. Machali aliongeza kuwa zaidi ya mara 20 katika kipindi cha mwaka mzima 2011 chama hicho kimekuwa kwenye vikao kikijadili masuala ya Kafulila na mbunge huyo amekwisha onywa na kukiri mwenyewe kuwa amekosa na hatorudia kukivuruga chama lakini kila kiakao kinachoitishwa kimekuwa kikimzungumzia yeye.

"Chama kimeshindwa kufanya mambo mengi ya maendeleo kwa wananchi wake kwa kupoteza muda kumjadili mtu mmoja, tumekaa chini na kupima uwepo wake chamani na manufaa iwapo tutamtupa nje ya chama hivyo sote kwa pamoja tukasema TUMECHOKA" alisema kwa msisitizo katibu mwenezi huyo wa NCCR Mageuzi Mh. Moses Machali.

Akizianika nyaraka za Kafulila kuomba msamaha vikaoni.


Nyaraka za Kafulila kumuomba msamaha mwenyekiti wake James Mbatia kwenye baadhi ya vikao.




Wananchi wakiperuzi baadhi ya nyaraka zilizoanikwa kwenye hadhara hiyo alizoandika Kafulila kuomba msamaa kupitia vikao mbalimbali vya NCCR Mageuzi.


Hii kali zaidi....!!!!!!!!!!
 
Machali alifukuzwa kufanya mkutano jimboni kwake akakimbilia Mkoani Mwanza, sasa anajigongagonga kuhusu rufaha yake kwa Halima Mdee... NCCR - Mageuzi wanataka vyote

 
Licha ya makosa ya kafulila lakini huyu jamaa machali hana cv yoyote compared to kafulila,anatumia mda mwingi kumzungumzia mwanaume mwenziwe(kafulila) , machali nilikua namuamini sana lakini sasa natamani nimtemee mate..........................eti wana jf au ndo analipa fadhila za ukatibu mwenezi?
 
Kwa mujibu wa Machali, Kafulila ndiye aliyeshinikiza James Mbatia afungue kesi dhidi ya Halima Mdee halafu sasa anageuka


Sisi hatutaki kusikia hayo maneno yasiyokua na mashiko ya kua alishinikizwa na Kafulila kufungua kesi. Tunataka kusikia kauli ya NCCR kuhusian na huyu bwana kua kikwazo kwa wapinzani wenzake maana siyo mara ya kwanza kuwawekea pingamizi wapinzani wenzake.
 
Back
Top Bottom