Inaonekana wana usalama wetu wako kwa ajili ya kuwalinda vigogo na sio wananchi wa kawaida. Kama kwenye ufunguzi wa kanisa lililolipuliwa Rais angekua anakuja, watu wangepekua kila kona kabla mheshimiwa hajaingia na macho yangekua kazini muda wote akiwa hapo kwenye tukio, kwa bahati mbaya hakuwepo..maisha yamepotea, watu wamepata vilema vya maisha just because watu hawajali.
Usalama wa Taifa na polisi mna damu mikononi mwenu, kwa yaliyotokea leo hamuwezi kuepuka lawama. Wananchi maskini wanauwawa kwa jambo ambalo mngeweza kulizuia kama mngekua makini na kazi zenu, kwa kuwa leo ni jumapili- priority ilikuwa ni bia na nyama choma na wengine mlipoamkia mnajua wenyewe. Kwa matukio mabaya machache tu ambayo yametokea recently kwa waumini wa kikristo, hata mwanangu aliyepo nursery sasa hivi angejua nini kinapaswa kufanyika kabla tukio la ufunguzi wa kanisa lile haujaanza na wakati shughuli nzima inaendelea.
Raisi wangu JK, kama unaijali nchi katisha ziara ya huko ulipo urudi nyumbani sasa hivi! Najua hutafanya hivi kwa kuwa hujali na utalala usingizi mnono huko ulipo as if nothing has happened.....prove me wrong on this! Anyway, kazi ya kwanza ninayokuomba uifanye utakapojiskia kurudi ni kuwapiga chini wakuu wa jeshi la polisi na mwenzie wa usalama wa taifa kwa kuwaangusha watanzania kwa mara nyingine tena. Wakristo wamekuwa wavumilivu sana na waelewa kwa yote mabaya wanayotendewa, itakua ni kosa kubwa tuki assume kuwa wataendelea kuwa wavumilivu, vita ya waislamu na wakristo inanukia, nimeskia watu wakianza kusema 'enough is enough', taifa linaelekea kubaya..Can you imagine kama msikiti ndio ungekua umepigwa bomu leo ingekuwaje?