KERO Mabasi ya Abood (Dar - Moro -Dar) yanajaza abiria kupitiliza kama Daladala za Mbagala, hii si sawa

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Abood.jpg
Machi 6, 2024 nikiwa natoka Morogoro kurudi Dar es Salaam nilikata tiketi vizuri tu katika Ofisi za Mabasi ya Abood, tumetoka Stendi Kuu siti zipo levo, lakini kufika vituo vya mbele wakaanza kusimama na kuendelea kubakia abiria.

Matukio hayo yalinishangaza sana, kwanza wahusika wa mabasi wenyewe wanaona kabisa basi limejaa lakini wanaendelea kuingiza abiria zaidi.

Pili abiria wenyewe wanaingia wanakuta hakuna siti iliyo wazi, kote kumejaa na bado hawalalamiki.

Yaani basi limejaza abiria kama vile mnaenda Daladala za Mbagala ama Gongo la Mboto kumbe ni safari ya masafa marefu, kilichonikera zaidi mtu anakuinamia kwenye siti yako, harufu ya jasho lake yaaani ni kero tupu,

Hakuna hata raha ya kupanda hili basi, hii sio mara ya kwanza, kwani nilijua ni ukitokea Moro tu lakini niliposiri tena kutoka Dar Kwenda Moro nikakutana na hali hiyohiyo.

Ukipanda Stendi Kuu kutoka Dar kila kitu kiko poa, subiri mfike kuanzia maeneo ya Kibamba ama Misugusugu kule Ubena Zomozi wanajaza abiria wa kusimama hasa nyakati za Alasiri kwenda jioni.

Huu utaratibu ni mbovu sana, nimeshaona pia katika mabasi ya kampuni kadhaa nyingine ambazo hazina umaarufu lakini kama Abood nao wameanza hii tabia, inamaanisha hatua zinatakiwa kuchukuliwa haraka, kwani mbali na kuwa kero pia sio salama kiafya na wanavunja utaratibu waliowekewa na mamlaka za usafirishaji.

Serikali inasisitiza mabasi yatumie Digitali katika kudhibiti mapato na kurahisisha mchakato wa ukataji tiketi, lakini hiki kinachofanyika inamaanisha kina baraka za wale Maafisa wanaosimamia vyombo vya moto barabarani kwa kuwa nina uhakika wanaona na hawachukui hatua kwasababu wanazozijua wao.

Kingine mrundikano wa Abiria unaweza kuchangia kuambukizana kwa magonjwa na hata ikitokea changamoto mfano hajali, wale walioongezeka hawatapata haki zao wanazostahili kwa kuwa hatakuwemo kwenye orodha.
 
Mkuu unawachoma wakati wenzako wanatafuta riziki kwa kujiongeza , pesa ile wanagawana Dereva na Konda.

Gari inakuwa imejaa kuna abiria wanakuwa na haraka na wengine wanashuka vituo vya jirani wanachukua buku 7 au nyingine yeyote kinyume na ile ya tiketi ..

Hawajazi kama Dalalada wanakuwa kidogo tu sio wengi kiasi Cha kuleta kero ,mbele wakiona hatari wanawashusha Kisha bodaboda wanawafaukisha kwenda kupanda sehemu nyingine baada ya kuvuka Dangerous zone.
 
Hiyo posho ya konda na dereva.

Watu wanaona bora wasimame kuliko kupanda Coaster za Dar Moro. Abiria wa Dar au Moro kwenda Chalinze,Mlandizi, Vigwaza wanaona bora wasimame ili wawahi kufika
 
Mkuu unawachoma wakati wenzako wanatafuta riziki kwa kujiongeza , pesa ile wanagawana Dereva na Konda.

Gari inakuwa imejaa kuna abiria wanakuwa na haraka na wengine wanashuka vituo vya jirani wanachukua buku 7 au nyingine yeyote kinyume na ile ya tiketi ..

Hawajazi kama Dalalada wanakuwa kidogo tu sio wengi kiasi Cha kuleta kero ,mbele wakiona hatari wanawashusha Kisha bodaboda wanawafaukisha kwenda kupanda sehemu nyingine baada ya kuvuka Dangerous zone.
Kwa expense ya abiria?

Basi waendeshe daladala.
 
Acheni kulia lia.
Kama Aboud anazingua panda BM au kampuni nyingine.
 
Ungelijua hayo mabasi ni ya nani hata usingeleta Uzi Abood ni nyapara tu na trafiki wa njia hiyo wanajua kuwa ni Mali ya awamu ya pili
 
Back
Top Bottom