Maazimio ya Kamati Kuu CHADEMA

Maazimio ya Kamati Kuu CHADEMA

Dar es Salaam. Kamati Kuu ya Chadema imesema tathmini yao kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Desemba 14,mwaka huu imebaini kuwa ulihujumiwa.

Pia, kimewataka Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Hawa Ghasia kujitathmini na kuchukua hatua za kuwajibika kwa kujiuzulu kutokana na kushindwa kusimamia ipasavyo uchaguzi huo.
 
Vyama vya upinzani haswa UKAWA vilishughulika saana na kutizama nani agombee wapi,badala ya kufikiria nini waatakiwa wafanye nini ili wasiache mwanya uchaguzi kuhujumiwa,kama kweli umehujumiwa. Kwa mwendo huu watabaki katika kila chaguzi kusema tumehujumiwa au tumeibiwa.
 
Kamati kuu niliwaomba kwenye maazimio yenu kwamba kuanzia sasa wananchi waanze kuchukua majina na picha za polisi wanaoshirikiana na ccm kuhujumu demokrasia, huko mbele ya safari chochote kikitokea watatumika kama sehemu ya ushahidi. Inaonekana polisi wanatumika kwa maslahi yao na ccm kwani wote wanalihujumu taifa kwa njia ya rushwa. Wanajua wakiwatetea ccm bado wataachia mwanya wa kula rushwa. Kwa mfano huku Arusha kuna jambazi sugu anayefahamika kwa jina la Jumanne mjusi anakata wapinzani mapanga kwa kutumwa na ccm huku polisi wakijua na kumuona lakini hawachukui hatua.
 
Back
Top Bottom