Maaskofu waipinga CHADEMA...

Wana bahati sana wangeongoza kipindi cha agano la kale sijui kama wange-survive . Manake kipindi kile ukileta unafiki au kosa dogo tu kama alilofanya Musa basi adhabu pale pale. Na pia washukuru mno watz tuko poa sana wanatunyanyasa lkn aa tunamwachia Mungu. Tena na hawa viongozi wa dini wanaongoza kwa ufisadi unadhani ukikosa ada ya mtoto shule wanakusaidia hawa . Wanasahau kua kila jpili unatoaga sh 200 wewe na familia yako yote na bado michango ya jumuia . Tumewanyamazia tu wanadhani hatuelewi/ hatujui kama wanatunyonya na wameanzisha mara fungu la kumi n.k. Viongozi wa dini acheni siasa fanyeni kazi mliyoitiwa na kama mnataka kutetea wananchi basi simamieni haki
 
Askofu si nabii na si malaika kama wako neutral angemaliza kutoa maoni yake kuhusu huundwaji wa red briegad ya cdm angeshutumu hata green guard iliyoazishwa na chama cha ccm angeeleweka sana
 
Mmmh......kama kujilinda dhambi basi hiyo kali.Kwanini tunafunga milango tunapolala?.......nataka kujiunga jamani na hicho kikundi cha kujilinda.
 
..watanzania ni raia wapole na wavumilivu sana...na ndio maana wanaonewa kwenye kila nyanja ya maisha yao....wamebaki kumwachia Mungu tu mambo.....utawasikia hata baadhi ya raia wadai haki siku hizi wanaposhindwa wanabaki kusema wanamwachia Mungu... maana wakisema wanaambiwa watapigwa....na wanapigwa haswa...inauma.....
 
Mmmh......kama kujilinda dhambi basi hiyo kali.Kwanini tunafunga milango tunapolala?.......nataka kujiunga jamani na hicho kikundi cha kujilinda.
..hao viongozi wa dini wenyewe kwenye taasisi zao na majumbani kwao wamejiwekea ulinzi mkali......tena siku hizi ambazo wao nao wanapigwa mabomu ndio kabisa.....leo wanakuja na kauli hizi za kinafiki....utawaelewaje hawa viongozi....kama si minafiki mikubwa.....
 

Si ndo hapo sasa.......
 
Tena bola na wao wanapigwa pengine watapata akili. Yaani mimi wamenitoka sijui ndio ujeuri umenizidi yaani hata niwaonapo siwanyenyekei kama zamani sanasana wananitia hasira tu
 
Askofu si nabii na si malaika kama wako neutral angemaliza kutoa maoni yake kuhusu huundwaji wa red briegad ya cdm angeshutumu hata green guard iliyoazishwa na chama cha ccm angeeleweka sana
Yap hata mimi ningemuona wa maana lkn yuko biased hivi ndio inayotia hasira
 
Gamba huyu Askofu!! Leo hii ndio anaona vikundi vya ulinzi vinahatarisha AMANI alikuwa wapi kutoa kauli iyo wakati CCM walipoanzisha GREEN GUARD?
 
Wakati green guard inapigiwa kelele mbona hamkusema?nawasifu sana Chadema,yaani mtego wao unazidi kunasa wanafiki wengi!
 
Mimi ni mkristo na ni muumini wa KKKT na ninasali usharika wa Arusha Mjini Kati lakini kwa maneno ya askofu huyu yananifanya niamini moja kwa moja askofu huyu katoka nje ya maagizo na maneno ya vitabu vitakatifu na kutekeleza mashinikizo ya wanasiasa ikiwamo ccm kwa maslahi binafsi.

Ombi langu kwa askofu huyu ni ajitathmini kwa mara nyingine na afanye toba ya kweli aepeke hukumu ya dhambi hii kubwa aliyoifanya ya kupotosha kondoo wa Mungu.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Exoud mamuya poleni na deni la ciridor spring mkuu. Maaskofu wengine ndio tabu ya watanzania
 
kwa moshi na arusha ni hao red brigade ni makundi ya majambazi wataongozwa magenge ya uhalifu ya uwizi wa magari na mauaji ya Lema yaliyokuwa yanatikisa miji hiyo
Askofu alisema nini
kuhusu haya nayo. Nauliza hivi kwa kuwa inaonekana umeandika kwa mlengo
fulani ambao una upendeleo. Nimeshindwa kujua kama hiyo Slant ni ya
Askofu? au ni ya Mwandishi. Kasema lipikuhusu Haya
 

Mkuu sijui malengo yako lakini huwatendei haki "Maaskofu"! Hii uliyotoa hapa ni kauli binafsi ya "Askofu Amon Kinyunyu" na hujaonesha popote kwamba yeye ni "msemaji wa maaskofu"!!!
 


vip babako yupo? Tunataka mlinzi wa ofis za cdm,huku zinavunjwa na nyaraka kuibwa! Huna aibu mjinga wewe,twende polis tuombe ulinz wa ofis? Chambua alichosema mbowe,red brigade ipo inaimarishwa kukabiliana na hila zenu.
 
kanisa lilianzishwa kabla ya green guard. walipaswa kukemea green guard kwanza. inashangaza maaskofu kutoa matamko yenye harufu zote kuwa wamepewa mlungula na kuambiwa 'semeni hivi'

Mimi naamini huu ni mwendelezo wa propaganda za wahuni - CCM!
Haiingii kabisa akilini huyo askofu akemee uanzishwaji wa vikundi vya kujihami dhidi ya hujuma zinazofanywa na CCM na washirika wao dhidi ya CHADEMA.
Hivi askofu huyo anaishi hapa nchini au ughaibuni? Ni kweli kabisa hafahamu CCM Ina Jeshi la kuteka, kutesa na kuua wote wenye mawazo tofauti na wao?
Hapa ndipo ninapoungana na mchangiaji mmoja aliyesema inawezekana Askofu huyo amehongwa na vibakauchumi hawa CCM ili kutoa tamko la namna hiyo, tamko linalofhalilisha hadhi yake.
Kama ni kukemea angefanya hivyo kwa CCM ambayo kwa miango kadhaa sasa ina Jeshi la kulinda uhalifu wao.
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1374268635.322842.jpg
    81.6 KB · Views: 57
  • ImageUploadedByJamiiForums1374268674.807263.jpg
    56.7 KB · Views: 51
  • ImageUploadedByJamiiForums1374268709.677697.jpg
    57.6 KB · Views: 54
  • ImageUploadedByJamiiForums1374268741.688941.jpg
    19.8 KB · Views: 50
  • ImageUploadedByJamiiForums1374268764.771291.jpg
    34.1 KB · Views: 42
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…