viongozi wa kanisa wana wajibu wa kuwaelimisha waumini wao kimwili na kiroho...ndo maana makanisa yaliyokamilika yanajenga na mashule na mahospital pia, vinginevo yangejikita kujenga makanisa tu yasingepata mafanikio yalionayo kiroho. sioni shida kwa viongozi wetu kutupa mwanga katika tusiyoyajuaKweli umeamua kushikilia msimamo wako,lakini unapaswa ujue kanisani sio sehemu sahihi kwa hiyo mijadala,hayo jadilini mitaani kwenu.Kanisa ni Universal institution, sio taasisi ya kitaifa,ndio maana aihitaji kuwa raia ili uwe mshirika kama ilivyo kwa vyama vya siasa
Mimi ni Roman Catholic lakini hawa maaskofu wamenifanya niufikirie mara mbili mbili huu ukatoliki wangu.
Kwanini hawa maaskofu watudharau kwa kiasi hiki? Yani wametuona sisi ni ma-Robot tusioelewa chochote hadi tuelekezwe cha kufanya?
Hawa maaskofu kwa akili zao wanadhani Mungu alishindwa kutufanya ma-Robot tufanye anayoyataka yeye tuepukane na haya mateso ya hii Dunia?
Wamenikera sana hao maaskofu.
Mimi ni Roman Catholic lakini hawa maaskofu wamenifanya niufikirie mara mbili mbili huu ukatoliki wangu.
Kwanini hawa maaskofu watudharau kwa kiasi hiki? Yani wametuona sisi ni ma-Robot tusioelewa chochote hadi tuelekezwe cha kufanya?
Hawa maaskofu kwa akili zao wanadhani Mungu alishindwa kutufanya ma-Robot tufanye anayoyataka yeye tuepukane na haya mateso ya hii Dunia?
Wamenikera sana hao maaskofu.
Tatizo Lako Mkuu Bado Hujamuelewa Vizur MUSAMI Kwa Ufupi ilitakiwa Maaskofu Wakae Pamoja Na Mashekhe
:shocked:
Wajadil Msimamo Wao Ndo Wautoe Hadharani. Lakin Kusema Maadhimio Ya Maaskofu Tz Ni ... Juu Ya Katiba. Swali, Je Masheikh Nao Wakija Na Msimamo Wao Kinyume Na Maaskofu Huoni Kama Itatokea Balaa Kubwa?.
Mbona Viongozi wa Serikali walitoa wito tupige kura za NDIO? Hao hawajakukera?
Kwa hiyo wewe unakubali serikali inavyoipigia debe katiba? Serikali yenyewe ina ajenda gani inapowaambia watu wapige kura ya NDIYO? Kwa nini serikali wasitoe tu uhamasishaji wa kusoma katiba wakawaacha watu kuamua wenyewe? Mifano halisi ninayo. Waziri Mh Mary Nagu juzi kati alikuwa na wamasai akawaambia hii katiba ni nzuri wapige kura ya NDIYO (Hiyo ni kampeni ya serikali) Makamu wa pili wa rais kule Zanzibar naye hivi majuzi kule Zanzibar aliwaambia wananchi kuwa wapige kura ya NDIYO. (Pia hiyo ni kampeni ya serikali)
Sasa inakuwaje vibaya Maaskofu kuwaambia waumini wao wapige kura ya HAPANA wanapoona inatakiwa kuwa hivyo? Jamii forum ni ya watu wenye akili wanaoweza kuchambua mambo lakini nasikitika kuona watu wengi wanashindwa kuielewa vizuri hii nchi yetu. Tukubaline hapa kama Maaskofu wamekosea basi na serikali ishakosea zamani na hakuna wa kumlaumu mwenzie..