Maaskofu ndio wasaliti

Huna point. Na kama ulikuwa hujui kiongozi wa Kanisa Katoliki hapa nchini ni Askofu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) na ye ni Ngalalekumtwa aliyesaini waraka huo wa maaskofu. Kama unajua umuhimu wa dini waachie wakristo wameamua kupitia maaskofu wao hawataki deal bovu la kupanga kusimika mahakama ya Kadhi (mahakama ya dini) katika nchi isiyokuwa na mlengo wa kidini.
 

Mimi nimemuelewa mkuu,isipokuwa mimi ninachokijua ni kwamba Maaskofu wana msimamo wao wakati Masheikh nao wana msimamo wao,sasa kwamba Maaskofu na Masheikh wawe na Msimamo mmoja hiyo ni ngumu sana kumbuka hao hawana common interest kutokana na kutofautiana ktk misingi mikuu ya Kiimani,ndiyo maana Maaskofu wanaona bora wawaelekeze Waumini wao vivyo hivyo na Masheikh nao wanawaelekeza waumini wao;

Halafu tambua kuwa si viongozi wa wakristu pekee ndio wanaowaelekeza waumini wao kuhusu Katiba bali hata wale viongozi wa Waislamu hufanya hivyo tofauti ni kwamba wao wanafanya kwa siri kubwa,ndio maana baadhi ya watu wanahisi Maaskofu wamekosea sana lakini mimi nasema wapo sawa.
 

mkuu umenena.
 
Kama Ni Wakiristu au Wakiristo hebu tujuzeni Kati ya hao ni yupi wa Msalaba tu na yupi wa Bibilia. Banjo atapinga hili;

MATHAYO 5:25. PATANA NA MSHITAKI WAKO UPESI, WAKATI UWAPO PAMOJA NAYE NJIANI, YULE MSHITAKI ASIJE AKAKUPELEKA KWA KADHI,
NA KADHI AKAKUPELEKA KWA ASKARI, UKATUPWA GEREZANI.

KADHI WA KIISLAMU HAMPELEKI MTU GEREZANI ILA YEYE NI KUTOA MAAMUZI YA HAQI TU BASI. MAASKOFU NA WACHUNGAJI TUSOMA KWELI YA MUNGU, TUSIPOTOSHE WATU!!
 
Mathayo 5;26
amin, nakuambia,
hutoki humo kamwe hata uishie kulipa sent ya mwisho.
Sasa tafakuru hayo maagizo ya mungu, tupende ya mungu ya bin adamu yatatumwaga damu.
Uwepo wa kadhi ni maagizo ya mungu.
 
sheckman

Kwa hiyo una maana kwa Maaskofu kupinga mahakama ya Kadhi wanapingana na biblia? Hiyo Mathayo 5:25. Nafikiri kuna tofauti kati ya kadhi aliyezungumzwa hapo na huyu anayedaiwa na waislamu
 
Last edited by a moderator:
Wa MATHAYO 5;25:
KADHI huyu anao Askari wakukutupa GEREZANI.
Lakin KADHI mkuu KTK Iman ya Kiislam, hana Magereza na wala hana Askari, yeye kufungisha Ndoa, Mali za Waqfu, Mirathi na kulinda Ndoa zadi ya Watu laghai.
Mambo ya Kijinai ni KTK Mahakama za Jamuhuri.
 
MATHAYO 5;25 ndivyo ilivyo sasa Askof anatafsiri.
Kama upo karibu naye muulize tu!!! Atakujibu, mm siwezi kusema anaikubali ama anaikataa,
Shukrani.
 

Serikali inaongozwa na Chama Ccm inasema kura ya Ndio afuCdm/ukawa kura ya Hapana sasa hawa maaskofu wanasimama wapi hawaon kama wanatuchanganya waumini hapo
 
wao ni viongozi wa dini,kwa nafasi yao wametushauri wauumini tupinge katiba mbovu.wewe unaanza kuhoji.kanisani unafuata nini?zaidi ya yote akili za kuambiwa changanya na zako.say no to fake constitution.wajulishe na wenzio
 
wao ni viongozi wa dini,kwa nafasi yao wametushauri wauumini tupinge katiba mbovu.wewe unaanza kuhoji.kanisani unafuata nini?zaidi ya yote akili za kuambiwa changanya na zako.say no to fake constitution.wajulishe na wenzio

Kanisani sio sehemu ya kujadiliana katiba ya nchi,bali ni sehemu mahususi kwa ajili ya kumuabudu Mungu,sababu ni kwamba kwa ulimwengu wa leo ni kawaida kukuta watu wa mataifa mbalimbali ndani ya kanisa,sasa mkianza kuleta mijadala ya katiba yenu kwenye ibada wewe unaona litakuwa jambo la hekima?Hawa wageni watafaidikaje na mijadala yenu?
 
Kazi kweli kweli, Kuhubiri Neno LA MUNGU, na kupropoganda Siasa, ni Upande UPI Una Rehema na Baraka tele?
Mtaalamu wa Neno answers kujiingiza ktkt Siasa? Ama ktk Siasa kunamanufaa zaidi ya Maeneo ya Ibada?
Sio Maaskofu tu hata Masheikh.
Siasa iwe Siasa na
Ibada iwe Ibada, Ushauri wa Bure.
 

Kwa kuwa huzijui ToR za wachungaji ninakushauri unyamaze au uulize uambiwe. Soma Biblia kama wewe ni Mkristo utaona manabii walivyokuwa wanawakemea wafalme. Kumbuka Eliya aliwahi kuizuilia mvua kunyesha. Najua wewe siyo Mkristo ndo maana hujui kazi za watumishi wa kweli walioitwa na Mungu.
 
.wao hawajajadili na waumini wao,wamewaambia wapige kura ya sio.wewe binafsi unaionaje rasmu hii?na ilivyopitishwa unaridhika?
 

Kanisa linahusisha watu kutoka mataifa mbalimbali ndio maana kuna makanisa hapa nchini yanaongozwa na raia wa kigeni,mfano kuna Wachungaji kutoka Kenya,Nigeria,Uganda n.k wanachunga makanisa hapa nchini,sababu ni kwamba Kanisa lipo kwa ajili ya kueneza ufalme wa Mungu na si wa dunia,Sasa kuleta mijadala ya katiba ndani ya kanisa ijadiliwe na watu kutoka mataifa mbalimbali ni ukengeufu.Tafakari
 

Sina cha kutafakari. Hao Wanigeria unaowazungumzia hata wakiwa kwao huwakemea watawala. Kama huna ToR za wachungaji endelea na imani yako.
 
kuna watu wanafikiri taasisi za kidini ni kufundisha mambo ya roho tu..., mbona hizi hizi taasisi za dini wanafundisha pia elimu dunia? wana hospitals? vituo vya kulelea yatima? kwa nini hayo wasingewaachia wenye serikali...wao waendelee na kupiga ishara za msalaba?
Kifupi ni kazi ya viongozi wa kidini kutulea kimwili na kiroho.
 
Sina cha kutafakari. Hao Wanigeria unaowazungumzia hata wakiwa kwao huwakemea watawala. Kama huna ToR za wachungaji endelea na imani yako.

Kweli umeamua kushikilia msimamo wako,lakini unapaswa ujue kanisani sio sehemu sahihi kwa hiyo mijadala,hayo jadilini mitaani kwenu.Kanisa ni Universal institution, sio taasisi ya kitaifa,ndio maana aihitaji kuwa raia ili uwe mshirika kama ilivyo kwa vyama vya siasa
 
na serkal inavosema uipigie kura ya ndiyo haijakukera? je wewe umeipata au hata kuisoma hiyo katiba pendekezwa??? umeielewa????? kwani kazi ya viongozi wa dini ni kuhubiri neno la Mungu tu? wao walichofanya ni kuelimisha uma na kwa kuwa wengi hatujasoma hiyo katiba, wao wamesoma na kuiona ina walakini ndo maana wametoa kama angalizo....but hujalazimishwa kupigia kura yoyote...wao wametoa angalizo ili yakikupata usimtafute mchawi
 

Ni wajibu wao kufanya hivyo, na wala sio dharau. Mbona kila siku unaenda kanisani kusikiliza mahubiri ya biblia wakati kuna biblia zimejaa kila kona, inamaana wewe ni robot usiejua kusoma? Au wanapokuhubiria kumcha Mungu na kuacha dhambi wakati kwenye kila moyo wa binadamu kumeandikwa jambo jema na baya. Ruhusu akili yako kuona mbali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…