Maaskofu na fedha ya ESCROW

Maaskofu na fedha ya ESCROW

Msiingize dini ye2 kwenye upuuzi uuuu
Dini ye2 ni safi kabixa
Xema aoo mbuz wala luswa wachomwe moto
 
Askofu ni mtu kama wengine.Wala kanisa haliwezi kuhukumiwa kwa kosa la Askofu au muumini
 
Ili padri apewe daraja la uaskofu sharti apewe jimbo. Hivyo askofu ni askofu wa jimbo fulani a.k.a jimbo mahalia.

Askofu Kilaini ni askofu msaidizi wa kanisa katoliki jimbo la Bukoba.

Ukitaka kutoa msaada wako wa fedha au vifaa, unatoa kwa kanisa katoliki jimbo la Bukoba. Kama ni hundi au Telegraphic Transfer a.k.a TT inatumwa kwenye akaunti ya kanisa katoliki jimbo la Bukoba au kama ni jimbo la Dar Es Salaam basi unatuma huko.

Na hata kama unataka kutoa sadaka ya kiwanja, lazima itafanyika transfer kutoka kwenye jina lako na kuwekwa kwenye jina la kanisa. Hauwezi toa sadaka yako kwenda kwa askofu Kilaini au askofu fulani. Huo ndiyo utaratibu wa kanisa katoliki.

Bunge katika mjadala wake, litamke waziwazi kwamba hawa maaskofu wafunguliwe mashtaka ya jinai. Kufanya hivyo siyo kuingilia mhimili wa mahakama kama Mheshimiwa Makinda anavyodai. Tunaona kwamba ni innocent ila tunawapeleka mahakamani ili mahakama either iwa exonerate au iwa convict.

Jambo lingine nikwamba, kanisa langu katoliki Tanzania, halina tena usafi tena wa kuinyoshea kidole serikali sababu watumishi wa serikali wasio waaminifu wanashirikiana na maaskofu wasio waaminifu kuhujumu mali ya umma. Zile pesa za Escrow ni za umma. Kama siyo za umma, kwanini kampuni binafsi inawagawia fedha viongozi wa umma? Ni ujira kwa kazi gani?

Huko nyuma Kilaini aliwahi kupelekwa nje kutibiwa kwa pesa za kiongozi wa serikali. Je kanisa katoliki lilikosa pesa ya kumtibia askofu huyu. Kanisa lijichungeze. Je nikwanini maaskofu hawa waliopokea pesa za ESCROW wote ni wale tu wasaidizi wa Pengo? Japo Kilaini kahamishwa lakini katokea kwa Pengo. Huyu mwingine ni msaidizi wa Pengo. Je Pengo kwanini anapendekeza wasaidizi wenye kasoro kimaadili?

Kanisa katoliki Tanzania tumechafuka


Unasema kanisa katoliki limechafuka? kwani limewahi kuwa safi?..mafisadi wao wauza unga wao, na bado mengi yanakuja hasa dili zenu za unga!
 
Hela waliyopewa maaskofu ni takribani milioni 160. Hiyo ni hela ndogo sana ambayo pengine hata wakiambiwa watairudisha hapo hapo. Tukumbuke Singasinga amechota bilioni 306
Mwizi ni Mwizi tu bila kujali kaiba Kiasi gani.
Na, hapa kanisa kama taasisi makini linawajibu wa Kutoa maelezo.
Kikubwa Si kurudisha walichoiba tu, bali pamoja na kuburuzwa mahakamani.
 
Hela waliyopewa maaskofu ni takribani milioni 160. Hiyo ni hela ndogo sana ambayo pengine hata wakiambiwa watairudisha hapo hapo. Tukumbuke Singasinga amechota bilioni 306

kwa hiyo unataka ku justify kitu gani? walistahili kuchukua? na hiyo pesa ya kurudisha hapo hapo wataitoa wapi? kwenye fungu la sadaka za waumini?.. tumia akili uchangiapo sensitive issues
 
Ili mtu afunguliwe mashtaka ya jinai, lazima kuwepo kosa la jinai. Ni vyema ukaisaidia mahakama kuonyesha kosa la jinai lililofanyika hapo.
Halafu wait a minute, hivi JK hawezi kukabidhiwa hela aifikishe kwenye taasisi fulani, say ya watoto yatima, bila kulazimika kuweka hela kwenye akaunti ya kituo hicho?

Rahisi tu; Huwezi,Haipo,Hiwezekani kumkabidhi kibubusa namna hiyo,
Na kama unao ushahidi kwa mfano mzuri wa raisi kama uliotupa tupe ushahidi ni lini na wapi imewahi kutokea kwa huyohuyo JK akawekewa kwenye akaunti yake?

Na kwa tafsiri ya kawaida akaunti binafsi ni mali ya mtu binafsi.
Hivyo ni wazi unapoweka pesa unamuwekea mwenye akaunti husika.
Kama kiongozi alipaswa kulijua hili.

Lakini twende mbele kidogo, Wakatoliki waliowengi wanakiri kuwa utaratibu wa sadaka ni kuitoa kanisani ili ipate kubarikiwa.
Je, Unataka kutuaminisha kuwa kuiweka kwenye akaunti ya maaskofu/viongozi hawa pesa ilishabarikiwa(automatically)?

Pili, Hizi taasisi wanazoziongoza viongozi hawa zimekasimu hawa viongozi kuwa ndio watunza fedha wao?
Au hazina akaunti zao za taasisi?

Mashaka makubwa na inaelekea kuwa huu ni mchezo wao na mengi yataibuka zaidi we subiri.
 
Nimekua makini kufuatilia ila mpaka mwisho nimegundua kitu kimoja tu ambacho huenda kinaleta mkanganyiko kidogo. Hivi bungeni kuna sehemu umeona wanasema pesa za Rugemalira ni haramu?
Zaidi wengine wameishia kumpongeza kwa jinsi alivyolipa kodi na mengineyo. Kwa njia hiyo pesa yake haina tatizo lolote zaidi ya sisi wananchi kupiga kelele tu. Na mpaka hapo kama ni skendo limwangukia singasinga ambaye najua serikali haiwezi kumfanya lolote.

Sasa kinachonipa utata kama pesa za Rugemalira ni halali na hazina tatizo lolote inakuwaje waliopewa pesa na tajiri huyo waingie hatiani? Nisaidieni ufafanuzi kidogo.

Hapa naona mwenye kosa zaidi ni Bank ya Mkombozi kufanya miamala mikubwa kinyume na sheria. Kwani sheria iko wazi hauruhusiwi kutoa cash ya kuanzia milion 10 na kuendelea.
pesa ya ruge haiwezi kuwa halali kama imetoka kwa singasinga ambaye tunamsema alijipatia fedha isivyo halali.
 
Naomba ukabatizwe kwanza ndiyo ujiite Mkatoliki, ukisha batizwa nenda katafute na kusoma kitabu hiki" How Cotholics Live. Virtues and Vices , pg 7.
Ili padri apewe daraja la uaskofu sharti apewe jimbo. Hivyo askofu ni askofu wa jimbo fulani a.k.a jimbo mahalia.

Askofu Kilaini ni askofu msaidizi wa kanisa katoliki jimbo la Bukoba.

Ukitaka kutoa msaada wako wa fedha au vifaa, unatoa kwa kanisa katoliki jimbo la Bukoba. Kama ni hundi au Telegraphic Transfer a.k.a TT inatumwa kwenye akaunti ya kanisa katoliki jimbo la Bukoba au kama ni jimbo la Dar Es Salaam basi unatuma huko.

Na hata kama unataka kutoa sadaka ya kiwanja, lazima itafanyika transfer kutoka kwenye jina lako na kuwekwa kwenye jina la kanisa. Hauwezi toa sadaka yako kwenda kwa askofu Kilaini au askofu fulani. Huo ndiyo utaratibu wa kanisa katoliki.

Bunge katika mjadala wake, litamke waziwazi kwamba hawa maaskofu wafunguliwe mashtaka ya jinai. Kufanya hivyo siyo kuingilia mhimili wa mahakama kama Mheshimiwa Makinda anavyodai. Tunaona kwamba ni innocent ila tunawapeleka mahakamani ili mahakama either iwa exonerate au iwa convict.

Jambo lingine nikwamba, kanisa langu katoliki Tanzania, halina tena usafi tena wa kuinyoshea kidole serikali sababu watumishi wa serikali wasio waaminifu wanashirikiana na maaskofu wasio waaminifu kuhujumu mali ya umma. Zile pesa za Escrow ni za umma. Kama siyo za umma, kwanini kampuni binafsi inawagawia fedha viongozi wa umma? Ni ujira kwa kazi gani?

Huko nyuma Kilaini aliwahi kupelekwa nje kutibiwa kwa pesa za kiongozi wa serikali. Je kanisa katoliki lilikosa pesa ya kumtibia askofu huyu. Kanisa lijichungeze. Je nikwanini maaskofu hawa waliopokea pesa za ESCROW wote ni wale tu wasaidizi wa Pengo? Japo Kilaini kahamishwa lakini katokea kwa Pengo. Huyu mwingine ni msaidizi wa Pengo. Je Pengo kwanini anapendekeza wasaidizi wenye kasoro kimaadili?

Kanisa katoliki Tanzania tumechafuka
 
Naona umehama kutoka kwenye mada na kuanza kulishambulia kanisa. pole sana ref: Yesu akasema "Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. Nami nitakupa wewe funguo za ufalme; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo loteutakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni. (Mathayo 16:18-19)


Wakatolik bwana kwa kuish kwa dhehebu hawajmbo
 
MKOMBOZI BANK nayo ifutiwe usajili ni DESI mpya.
Hii benki ipo kisheria kabisa. sama hii taarifa hapa

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU AKAUNTI YA VIP ENGINEERING AND MARKETING ILIYOPO KATIKA BENKI YA BIASHARA YA MKOMBOZI

Utangulizi


Taarifa hii inatolewa kwa umma kutokana na ripoti mbalimbali zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari mitandao ya kijamii na taarifa iliyotolewa kwenye mjadala katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

1. Ufunguzi wa akaunti ya VIP engineering and Marketing (VIP)


Kampuni ya VIP engineering and Marketing ni kampuni ambayo imesajiliwa kwa mujibu wa sheria za Tanzania. Kampuni hii ilifungua akaunti katika benki ya biashara ya Mkombozi na hivyo kuwa moja kati ya wateja wa benki. Benki ilijiridhisha na ilizingatia taratibu zote za ufunguzi wa akaunti husika kwa kuzingatia sheria za nchi na kanuni zinazozitaka benki kupata nyaraka muhimu kutoka kwa mteja wakati wa ufunguzi wa akaunti hiyo.

Nyaraka hizo ni pamoja na kuwepo kwa cheti cha usajili wa kampuni, kanuni za kampuni, idhinisho la kampuni kumruhusu moja kati ya wanahisa wake kuendesha akaunti pamoja na picha na hati ya kusafiria ya mhusika wa kuendesha akaunti hiyo.

2.0 Mauzo ya hisa za VIP

Kampuni ya VIP ilileta mkataba kwenye benki ya Mkombozi wa mauziano ya hisa za asilimia 30 baina ya VIP na kampuni ya Pan Africa Power Solutions (PAP) ambazo inamiliki katika kampuni ya IPTL. Mkataba huo ulisainiwa tarehe 19 Ogasti, 2013. Bei ya asilimia 30 ya hisa hizo ilikuwa ni dola za Marekani milioni 75. Katika kifungu namba 2.4 cha mkataba wao kinaelekeza fedha za mauzo ya hisa zilipwe kwenye akaunti ya VIP iliyopo benki ya Mkombozi. Mkataba huo wa mauziano ya hisa baina ya kampuni hizi mbili ulitambuliwa na hukumu ya Mahakama Kuu ya Tanzania iliyotolewa na Jaji J.H.K Utamwa tarehe 5 Septemba, 2013.

3. Mchakato wa kulipa kodi ya serikali


Benki ilitambua kwamba katika mauziano hayo ya hisa ni lazima kodi ya Serikali ilipwe na hivyo iliizishauri pande zote mbili kupeleka mkataba husika katika ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili kufanyiwa makadirio ya kodi husika. Tarehe 20 Januari, 2014 TRA iliiandikia barua kampuni ya VIP na nakala ya barua hiyo kuletwa kwenye benki ya Mkombozi. Katika barua hiyo TRA iliitaarifu kampuni ya VIP kuwa makadirio ya kodi yatokanayo na mauzo ya hisa ni shilingi 38,186,584,322.00 ikiwa ni kodi ya mauzo ya hisa ya asilimia 30 za mauzo ya hisa kutoka VIP kwenda kwa PAP.(Capital gains and stamp duty).

TRA pia iliiagiza benki ya Mkombozi kuhakikisha kuwa inalipa kodi hiyo kwa niaba ya VIP mara tu fedha zitakapoingia kwenye akaunti yake.

Malipo ya kodi ya shilingi 38,186,584,322.00 yalilipwa TRA kwenye akaunti 11120100 iliyopo katika Benki Kuu ya Tanzania na TRA ilikiri kupokea kodi hiyo kwa barua yake yenye kumbukumbu namba 3-4/100/100/223/4 ya tarehe 24 Januari, 2014.

4. Ufafanuzi wa mambo mbalimbali


4.1 Benki ya mkombozi kuhusika katika kusafisha fedha chafu

Fedha zote zilizoingizwa kwenye akaunti ya VIP iliyopo kwenye benki ya Mkombozi zilitokana na mauziano ya hisa kati ya VIP na PAP kwa mkataba uliotambuliwa na Mahakama Kuu ya Tanzania. Chanzo cha malipo hayo ni kuhamisha fedha kutoka kwenye akaunti ya PAP iliyopo katika benki ya Stanbic na kuingizwa kwenye akaunti ya VIP iliyopo katika benki ya Mkombozi.

Fedha hizo zilihamishwa katika mafungu mawili. Fungu la kwanza ilikuwa ni shilingi 73,573,500,000.00 zilihamishwa kwa njia ya TISS kwa kumbukumbu namba 000000050720 ya tarehe 23 Januari, 2014 na fungu la pili ni dola za Kimarekani 22,000,000.00 zilihamishwa kwa TISS kwa kumbukumbu namba000000050812 ya tarehe 23 Januari, 2014. Malipo mengine ya asilimia kumi ya mauzo ya hisa yalilipwa kwenye akaunti ya Mkombozi iliyopo Benki Kuu ya Tanzania. Kutokana na mchakato huo benki ya Mkombozi ilijiridhisha kuwa fedha hizo ni malipo halali na siyo fedha chafu.

Benki ya Mkombozi haijihusishi na utakasishaji wa fedha chafu na haramu katika uchumi wa Tanzania.

4.2 Malipo yatokanayo na akaunti ya VIP

Malipo toka kwenye akaunti ya mteja hufanywa kutokana na maelekezo ya mteja. Benki ikishajiridhisha kuwa fedha ya mteja ni halali na ipo kwa mujibu wa sheria na hamna zuio lolote toka katika mahakama hapa nchini hutekeleza malipo kwenye akaunti ya mteja kutokana na maelekezo yake.

Benki ilijiridhisha kuwa malipo yote yaliyofanywa kutoka kwenye akaunti ya VIP ni halali kwa kuwa chanzo cha pesa hizo ilikuwa ni halali kutokana na mauzo ya hisa na ulipwaji wa kodi ya Serikali kama ilinyoelezwa hapo juu. Kutokana na sababu hiyo benki haikuwa na shaka juu ya malipo hayo.

4.3 Malipo taslimu kwa wateja na kubeba fedha kwenye viroba, mifuko ya rambo na magunia

Benki inatoa tamko kuwa malipo yote yaliyofanywa katika akaunti ya VIP yalilipwa kupitia akaunti za walipwaji. Hakuna fedha zilizolipwa taslimu kwa wateja na kubebwa kwenye viroba au magunia kama ilivyoripotiwa Bungeni. Pesa iliyotoka kwenye akaunti ya VIP tarehe 6 Februari, 2014 kiasi cha shilingi 3,314,850,000.00 ililipwa kwenye akaunti nane za wateja tofauti na siyo kubebwa kwenye viroba au magunia.

Na zile zilizotoka toka benki ya Stanbic zilizotajwa hapo juu zilitumwa kwa njia ya TISS na siyo kubeba kwenye magunia au viroba.

4.4 Malipo kwa mfanyakazi wa benki ya Mkombozi

Gazeti la Mawio la tarehe 20-26, Novemba, 2014 tolea namba 0122 liliandika kuwa mwanasheria wa benki ya Mkombozi ajulikanaye kwa jina la Rweyengeza Alfred alipokea malipo toka akaunti ya VIP ya shilingi milioni 40.2.

Benki inatoa tamko kuwa haina mfanyakazi anayetambuliwa kwa jina hilo na wala hakuna mfanyakazi yeyote wa benki aliyelipwa fedha toka kwenye akaunti ya VIP.

Wito kwa umma

Benki ya Mkombozi inachukua fursa hii kuwatarifu wateja wake na umma kutopotoshwa na taarifa au tuhumma zilizofafanuliwa hapo juu na kuwataka wateja wake wote kutokuwa na hofu yeyote kwani benki ipo imara na inafanya kazi kwa kufuata misingi ya sheria, taratibu na kanuni zilizowekwa na Benki Kuu ya Tanzania. Benki inawataarifu wateja wake na Watanzania kwa ujumla kutoyumbishwa na tuhumma hizo ambazo hazina ukweli ndani yake na badala yake waitumie benki yao kwa shughuli za maendeleo ya nchi yetu.

Pamoja tunajenga nchi na uchumi wa nchi yetu.

Hitimisho

Benki ya biashara ya Mkombozi haijihusishi na haitajihusisha na utakasishaji wa fedha chafu.

Imetolewa na:

MKURUGENZI MTENDAJI BENKI YA BIASHARA YA MKOMBOZI
 
Mpendwa Kanisa katoliki ndiyo serekali? Yakaizari abaki nayo kaizari na ya Mungu yaachani kwa Mungu, kanisa halina ucharika wowote na serikali. kwanza naomba nikukumbushe serikalia haina dini.

Kanisa langu Katoliki limechafuka na kuonesha mifumo yake imefeli kutuondolea huu upuuzi.......tunasubiri hatua kali na si ujanja ujanja.......
 
Jambo lingine nikwamba, kanisa langu katoliki Tanzania, halina tena usafi tena wa kuinyoshea kidole serikali sababu watumishi wa serikali wasio waaminifu wanashirikiana na maaskofu wasio waaminifu kuhujumu manani za umma. Zile pesa za Escrow ni za umma. Kama siyo za umma, kwanini kampuni binafsi inawagawia fedha viongozi wa umma? Ni ujira kwa kazi gani?

Mi nadhani tuanzie hapa. Je walilipwa ujira gani? Hili hamna aliyetayari kujibu maana itatibua siasa na kuweka uhalisia. Ndiyo maana haisemwi alilipwa bali zito anasema waligawana. pia hawasemi account ni ya nani bali waliogawiwa hamna document inayotaja account name bali namba na majina ya wqnayoiservice. wenye ushahidi wa hili ni mabenki husika na wenye waliotajwa kugawiwa fedha.

Kuhusu kanisa nadhani ni swala la kujiuliza tu ni kanisa linaendeshwaje? Basi na si zaidi.

Swala la Kilaini kwenda kutibiwa sishangai kwani yeye ndiye kiongozi wa dini pekee kutubiwa kwa fedha za srrikali? Au kwasababu alisema JK ni chaguo la Mungu kwa mujibu wa maelezo ya humu? Swala la eskrow linaendeshwa kisiasa na litaisha kisiasa.




Watu wa aina yako ndio wanaosababisha vita na vurugu za kidini.
Kwa muda mrefu waislam hapa Tanzania wamekua wakilalamikia mfumo uliopa na kufikia mahali pa kuuta huu mfumo wowote wenye matokeo mabaya na ya dhulma kuwa ni mfumo Kristo. Leo hii pesa haramu zinagawanywa kwenye kanisa tena kwa kificho na kutumia benki ya kanisa kutakatisha pesa haram halafu hadala ya kukemea tunasapoti huo uovu na dhambi kubwa ya kufanya nyumba ya Mungu kuwa pango la wanyanganyi kisa tu mnataka kumtetea Pinda ambaye bila shaka ndiye aliyeshawishi benki ya kanisa lake ikubali kutumiwa na matapeli.
Tujiulize kama ni sadaka kwa nini mashehe hawakupewa?
Jibu ni rahisi wanatambua kuwa kwa dini ya kiislam ni mwiko kutoa hela haram sadaka.Na walijua wazi kuwa akigundulika wazi kiongozi wa kiislam kwamba amehongwa itakua ni mtiti.Sasa badala yake wanatumia mfumo muovu kuzidi kulichadua kanisa mbele ya dini ya kiislam inayolalamika siku zote kuhujumiwa na kunyimwa maendeleo kwa sababu ya wakristo wa kanisa moja la rumi wanaonufaika kwa kuhujumu uchumi wa nchi.
Hili litolewe ufafanuzi kwa kuwa litaondoa imani ya maaskofu wa makanisa kwa watanzania.

Kodi iliyotakiwa ikusanywe kwa ajili ya watanzania wote inatumika kuendesha shughuli za watu na taasisi binafsi ikiwemo kanisa katoliki na miradi yake ya kibenki kwa kuhonga maaskofu wake.
Tusizidi kuwapa waislam sababu ya kulalamika halafu tukawaona wabaya.
Serikali isitumie nguvu ya kanisa katoliki kutufarakanisha.Hii nchi ikichatuka kidini hata hao maaskofu mafisadi hawata kaa kwa amani.Watajifungia makanisani kwa kilio na kusaga meno kwa dhambi walizoshiriki dhidi ya uchumi wa watanzania maskini.
 
Naona umehama kutoka kwenye mada na kuanza kulishambulia kanisa. pole sana ref: Yesu akasema "Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. Nami nitakupa wewe funguo za ufalme; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo loteutakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni. (Mathayo 16:18-19)



Hiyo Mathayo 16:18-19 sijaona palipoandikwa kanisa la Kirumi.
Na alikua anaongea na Petro ambaye alikua Myahudi na sio Mrumi au mjerumani au Mpolandi.
Je,uliwahi kumsikia Papa Myahudi.

Kwa mitume wale wa Yesu akiwemo Petro ilikua ni dhambi na kosa kumwita mtu kiongozi wa kanisa au baba (papa) wa kanisa.Je,hayo yapo kwako?
Bila shaka hili kanisa lililojipachika jina jipya la Kanisa la Kirumi ni yale magugu yaliyopandwa na adui(shetani) wakati wa usiku na sasa tunalitambua kwa matendo yake maovu ya kuturahia viongozi wake kupewa sadaka gizani tena kwa siri kupitia biashara za pesa haramu.
Hakika nawaambieni wakristo safi wakinyamazia juu ya huu ufisadi basi waislam watapaza sauti.
 
... Au hazina akaunti zao za taasisi?
Sharti alilotoa mfadhili wao (Ruge) ni kwamba kila aliyemuomba fedha awe ana akaunti Mkombozi Bank (kwa ajili ya urahisi wa kuhamisha fedha). Si rahisi Jimbo la Bukoba likawa na akaunti Mkombozi bank, ukizingatia ina brances Dar na Mwanza tu. Lakini viongozi na watumishi wa Kanisa waliopo na waliowahi kuwapo Dar wengi wao wana akaunti zao Mkombozi Bank. Nadhani hapo umenielewa nnataka kusema nini
 
kwa hiyo unataka ku justify kitu gani? walistahili kuchukua? na hiyo pesa ya kurudisha hapo hapo wataitoa wapi? kwenye fungu la sadaka za waumini?.. tumia akili uchangiapo sensitive issues
Umejuaje kama wameitumia? Hela walizo nazo za matumizi ya kawaida sio shida kwa mapadre na maaskofu wa Katoliki kwani matumizi yao si makubwa
 
Back
Top Bottom