Maaskofu na fedha ya ESCROW

Maaskofu na fedha ya ESCROW

pesa nyingi hivo za kubebwa kwenye magunia...kuna maana gani kubeba mzigo wote huo wakati mabank yapo na kutransact haichukui hata nusu SAA
unazipush tu then unatembea mwepesiii...Fumbua macho kaka.
Milioni 40 sihitaji hata kubeba mfuko wa rambo, suruali tu inatosha
 
Rahisi tu; Huwezi,Haipo,Hiwezekani kumkabidhi kibubusa namna hiyo,
Na kama unao ushahidi kwa mfano mzuri wa raisi kama uliotupa tupe ushahidi ni lini na wapi imewahi kutokea kwa huyohuyo JK akawekewa kwenye akaunti yake?

Na kwa tafsiri ya kawaida akaunti binafsi ni mali ya mtu binafsi.
Hivyo ni wazi unapoweka pesa unamuwekea mwenye akaunti husika.
Kama kiongozi alipaswa kulijua hili.

Lakini twende mbele kidogo, Wakatoliki waliowengi wanakiri kuwa utaratibu wa sadaka ni kuitoa kanisani ili ipate kubarikiwa.
Je, Unataka kutuaminisha kuwa kuiweka kwenye akaunti ya maaskofu/viongozi hawa pesa ilishabarikiwa(automatically)?

Pili, Hizi taasisi wanazoziongoza viongozi hawa zimekasimu hawa viongozi kuwa ndio watunza fedha wao?
Au hazina akaunti zao za taasisi?

Mashaka makubwa na inaelekea kuwa huu ni mchezo wao na mengi yataibuka zaidi we subiri.
Mwizi Kilaini kaandika kwenye mitandao bila aibu kuwa hii si mara ya kwanza kupokea pesa kwa njia hizo. Achunguzwe critically.
 
Sharti alilotoa mfadhili wao (Ruge) ni kwamba kila aliyemuomba fedha awe ana akaunti Mkombozi Bank (kwa ajili ya urahisi wa kuhamisha fedha)
Si kweli hapa ni kwakuwa Mkombozi ndio vinara na wanaoujua huo umafya wa utakasishaji Pesa hii yenye element ya uharamu.
Si rahisi Jimbo la Bukoba likawa na akaunti Mkombozi bank, ukizingatia ina brances Dar na Mwanza tu
Aibu gani hii, Kwahiyo inachukuwa miaka kwa taasisi kufungua akaunti ndio maana wakaamua kuweka kwenye akaunti za viongozi hawa? Kwanini taasisi isingefungua akaunt na kisha wakawa wanahamisha kwenyenda kwenye akaunti za mabenki ambayo yana matawi jirani na jimbo lao? Ondoa upofu!.
Lakini viongozi na watumishi wa Kanisa waliopo na waliowahi kuwapo Dar wengi wao wana akaunti zao Mkombozi Bank. Nadhani hapo umenielewa nnataka kusema nini
Kwahiyo kiongozi akiwa anaanzisha taasisi basi asilazimike kufungua akaunti kuondoa usumbufu. Hueleweki, Na hutaeleweka.Mwenye kutetea Wizi tu ndie anaeweza kukuelewa- Kanisa linachakujibu hapa.
 
.
Aibu gani hii, Kwahiyo inachukuwa miaka kwa taasisi kufungua akaunti ndio maana wakaamua kuweka kwenye akaunti za viongozi hawa? Kwanini taasisi isingefungua akaunt na kisha wakawa wanahamisha kwenyenda kwenye akaunti za mabenki ambayo yana matawi jirani na jimbo lao? Ondoa upofu!. Kwahiyo kiongozi akiwa anaanzisha taasisi basi asilazimike kufungua akaunti kuondoa usumbufu. Hueleweki, Na hutaeleweka.Mwenye kutetea Wizi tu ndie anaeweza kukuelewa- Kanisa linachakujibu hapa.

Ipange vizuri, nitakujibu. Umechanganya quotes zangu na response zako
 
Huyo Gavana wa BoT aliyezitoa hizo fedha hajaguswa, nani ataguswa kwa kupokea?
Hilo ni somo na mjadal mwingine, Uliopo sasa waliopokea fedha kiutata na tunaowafahamu kwa ushahidi washughulikiwe, Period.
 
Mwizi Kilaini kaandika kwenye mitandao bila aibu kuwa hii si mara ya kwanza kupokea pesa kwa njia hizo. Achunguzwe critically.

Naomba niongezee apekenyuliwe, Kumbe ndio mchezo wao huu?
Hapa Kanisa linalo deni kubwa la maelezo kwa:
1.Waumini wa Kanisa Katoliki lenyewe, ingawa nasikia wanakawaida ya kutokuuliza na kuulizwa.
2.Waumini wa madhehebu mengine ya Kikristo
3.Waislam.
4.Wasiokuwa na dini wa jamii ya Wa-Tanzania.
5.Ulimwengu kwa ujumla kama wanataka watu wawe na imani nao.
 
Watanzania bwana. Mzizi mkuu umewashinda kuung'oa. Sasa mnaanza kuparamia kufyeka majani ya mti. Ng'oeni mzizi mkuu kwanza, hayo majani yatakauka tu automatically. Hebu mshughulikieni aliyegawa hizo pesa kwanza.

100 mkuu
 
yani Rc Kwa Sasa Hamna Tofauti Na Ccm Askof Wenu Wezi Tena Wale Waliokaribu Na Kadinali Benk Yenu Imetumiwa Kutakatisha Fedha Chafu Mnakuja Apa Ooh Kanisa Letu Safi...Mnanukuu Vifungu Vya Bible Ili Viwape Unafuu Nyie Kubalini Kanisa Limepakwa Matope Ili Kulisafisha Kamateni Wezi Pelekeni Mahakamani Mkinyamaza Ccm Wakwanza Kwa Wizi Wapili Roman Catholic
 
yani Rc Kwa Sasa Hamna Tofauti Na Ccm Askof Wenu Wezi Tena Wale Waliokaribu Na Kadinali Benk Yenu Imetumiwa Kutakatisha Fedha Chafu Mnakuja Apa Ooh Kanisa Letu Safi...Mnanukuu Vifungu Vya Bible Ili Viwape Unafuu Nyie Kubalini Kanisa Limepakwa Matope Ili Kulisafisha Kamateni Wezi Pelekeni Mahakamani Mkinyamaza Ccm Wakwanza Kwa Wizi Wapili Roman Catholic

Kweli hawa wenye dhamana ya kuongoza waumini ndo wamekuwa mfano mbovu, maandiko yanasema wanafunzi wangu watajulikana kwa mfano na matendo yao mema. Inakuwaje kiongozi upewe fedha yote hiyo tena kinyemela! Kwa kifupi hawa ndo walounganisha fedha ile kutolewa ktk bank ya Mkombozi na walicholipwa ni mgao wao wa kufanikisha utoaji wa fedha hizo haramu. Na wala halihitaji akili ya juu sana kutambua hili. Mimi ni RC na zijapendezwa kabisa na suala hili.
 
Fisadi Lowasa huwa anatoa misaada in public tena kwa institutions japo huwa hasemi ni marafiki gani wamechanga.Ruge amuige Lowasa sio kutoa kimya kimya
 
[




QUOTE=Spina;11269237]Kosa la jinai la maaskofu hawa ni kukwepa kodi. Mapato yoyote apatayo mtu lazima yalipiwe income tax to the tine of 30%[/QUOTE]

Hivi tangu lini sadaka ikatozwa kodi?
 
Hakuna cha ajabu hapo..Mfumo kristo unafanya kazi.
 
mwizi ni mwizi tu bila kujali kaiba kiasi gani.
Na, hapa kanisa kama taasisi makini linawajibu wa kutoa maelezo.
Kikubwa si kurudisha walichoiba tu, bali pamoja na kuburuzwa mahakamani.

kwani hao maaskofu wameiba wapi hizo pesa mnazodai warudishe?
 
Mimi ni Mkatoliki wa kufa..ila kwa hili hawa Maaskofu lazima wachukuliwe hatua stahiki..

Hivi unadhani kwa taratiu za kanisa zilivyo Kilaini atapona? Kumbuka kupeleka Bukoba ilikuwa ni scandal ya kujishirikisha kwke kwenye ambo ya kisiasa kiasi cha kuikwaza serikali sembuse na hili!
 
Ili padri apewe daraja la uaskofu sharti apewe jimbo. Hivyo askofu ni askofu wa jimbo fulani a.k.a jimbo mahalia.

Askofu Kilaini ni askofu msaidizi wa kanisa katoliki jimbo la Bukoba.

Ukitaka kutoa msaada wako wa fedha au vifaa, unatoa kwa kanisa katoliki jimbo la Bukoba. Kama ni hundi au Telegraphic Transfer a.k.a TT inatumwa kwenye akaunti ya kanisa katoliki jimbo la Bukoba au kama ni jimbo la Dar Es Salaam basi unatuma huko.

Na hata kama unataka kutoa sadaka ya kiwanja, lazima itafanyika transfer kutoka kwenye jina lako na kuwekwa kwenye jina la kanisa. Hauwezi toa sadaka yako kwenda kwa askofu Kilaini au askofu fulani. Huo ndiyo utaratibu wa kanisa katoliki.

Bunge katika mjadala wake, litamke waziwazi kwamba hawa maaskofu wafunguliwe mashtaka ya jinai. Kufanya hivyo siyo kuingilia mhimili wa mahakama kama Mheshimiwa Makinda anavyodai. Tunaona kwamba ni innocent ila tunawapeleka mahakamani ili mahakama either iwa exonerate au iwa convict.

Jambo lingine nikwamba, kanisa langu katoliki Tanzania, halina tena usafi tena wa kuinyoshea kidole serikali sababu watumishi wa serikali wasio waaminifu wanashirikiana na maaskofu wasio waaminifu kuhujumu mali ya umma. Zile pesa za Escrow ni za umma. Kama siyo za umma, kwanini kampuni binafsi inawagawia fedha viongozi wa umma? Ni ujira kwa kazi gani?

Huko nyuma Kilaini aliwahi kupelekwa nje kutibiwa kwa pesa za kiongozi wa serikali. Je kanisa katoliki lilikosa pesa ya kumtibia askofu huyu. Kanisa lijichungeze. Je nikwanini maaskofu hawa waliopokea pesa za ESCROW wote ni wale tu wasaidizi wa Pengo? Japo Kilaini kahamishwa lakini katokea kwa Pengo. Huyu mwingine ni msaidizi wa Pengo. Je Pengo kwanini anapendekeza wasaidizi wenye kasoro kimaadili?

Kanisa katoliki Tanzania tumechafuka

Binafsi sina imani kabisa na kanisa katoliki...Bora kuabudu chini ya pango kuliko kanisani.
 
Binafsi sina imani kabisa na kanisa katoliki...Bora kuabudu chini ya pango kuliko kanisani.

Nawe ni punguani tuu..kuna uhusiano gani wa Imani na Kanisa lako kiasi cha kufanya usiende Kanisa angali ni watu wachache ambao wataubeba mzigo wao wenyewe...

Si dhani kama wewe ni Mkatoliki..
 
Back
Top Bottom