Maarifa ya kutengeneza na Kurusha Bomu Watz wameyapata wapi?

Maarifa ya kutengeneza na Kurusha Bomu Watz wameyapata wapi?

Inanambo

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2011
Posts
4,063
Reaction score
2,873
Habari za kulipuka bomu katika kanisa huko arusha zimenisikitisha na kunitia hofu. Najiuliza mabomu huwa yanauzwa dukani kama Bastola au hutengenezwa kienyeji? Nilifuatilia sana ile habari ya Bomu uko Boston marekani nikajifunza kuwa lilitengenezwa kutokana na Sufuria ( Pressure Cooker).

Je elimu hii ya kutengeneza mabomu hutolewa shuleni? Japo nilisoma Chemistry kidogo ya O Level sikuwahi kukutana na elimu hii. Naomba serikali itafute kwa makini haya mabomu hutoka wapi ili tusiendelee kuumizana na kuuana. Kama kuna kiwanda kisakwe na kufungwa kabisa.
 
Hawa wameba bodaboda sio magaidi ni njaa tu magaidi ni wale waliotoka Saudi na falme za kiarabu kwasababu ya kuuwa waumini wa kitatoliki. Vijana wa bodaboda wenye miaka 18 na 20 inawezekana hata hawajajua walikuwa wanafanya nini!! hivyo sio Watanzania bali ni wageni
 
Mkuu hilo sio swali tena, ukweli ni kwamba watanzania tunatengeneza mabomu. Hivi ninavyoandika hapa sijalala usiku kucha nimeenda kwenye shughuli flani maeneo ya kimara king'ongo, jioni tukiwa na wenyeji wangu wakaniambia kutokea kwa majambazi ambayo yanatega bomu 'labda' linalotengenezwa kienyeji lakini mlipuko wake ni kishindo kikuu, jamaa ndani ya wiki moja wamepiga nyumba mbili eneo moja, wanachofanya wanatega hilo bomu kwenye makufuli ya geti halafu wanalipua then wanaingia ndani cha kushangaza kazi yote hiyo wanachukua hela, pete za ndoa, tv deki na vitu vidogovidogo.

Kwakuwa ni mshindo mkuu watu hawawezi kutoka mda huohuo so wanafanikiwa kutoroka. Sasa leo saa tisa na dakika arobaini na tisa alfajiri tukiwa tunapiga story tukasikia kishindo tena, of coz kila mtu alitafuta ustaarabu wake kwanza then ndo filimbi na wananchi tukatoka, nimeshuhudia live jinsi bomu lilivyosambaratisha grill, jamaa wakaingia ndani wakawatite, wakakomba hela tv na deki, mlango wa mninga na geti lake nyang'anyang'a.

Ni punde tu hapa imetokea. Enyi wanasiasa wetu acheni kufuja pesa, wawezesheni polisi watulinde, hali ni mbaya. naambiwa baruti zitumikazo zinapatikana kwa wingi na kirahisi kabisa, watu wa machimbo ya pale tegeta na kwingineko wanalitambua hili sasa sembuse arusha ambako mererani inapatikana na tanzanite inachimbwa underground? I think it is a very simple technology na ndo maana watu wanatengeneza mabomu ya kwenda kuibia TV wakati tv siku hizi sio dili tena. Inasikitisha mkuu, halafu naambiwa wagenini/wavamizi wa kinyarwanda nk huku ndo maeneo yao ya makazi
 
Watoe semina za ujasiriamali za kutengeneza mabomu
 
ugumu wa maisha na tamaa na mafanikio ya muda mfupi ndio yanafanya watu kufanya hayo mambo mkuu..
 
watanzania tunaelekea wp? Tanzania ni aman ndio maana uhur we2 tupata bila kumwaga damu. Inakueje bomu leo hii? Ujanja ujanja wa wa2 fulan ambao hataki aman ya nchi ye2 tunaomba walaniwe kwa mawazo hayo mabaya.
 
Back
Top Bottom