Waandishi habari Tanzania walikwisha goma siku nyingi zilizopita,na ndio maana hatupati habari makini,bali habari baada ya bahasha.
Hivi kwa nini tusijulize maswali haya kabla ya kulaumu au kuunga mkono maandamano hayo.
1:Je mwandishi wa habari analipwa mshahara?
2:kama analipwa ni nini mafao yake awapo nje ya kituo chake cha kazi?
3:Kama anataka kupokea malipo toka kwa chanzo cha habari,je habari yenyewe itakuwa halisi?
4:kama ni mwandishi wa kujitegemea.nini mkataba wake na wale anaowapelekea habari?
Waandishi wa habari mkoani Iringa wamefanya maandamano yao kuelekea kwa MKUU wa MKOA kwa lengo la kulalamikia kunyanyaswa na Ofisa Habari wa Mkoa huo. Moja ya malalamiko yao ni kunyimwa posho wakati wa safari za viongozi mbalimbali mkoani humo. Nawaleteeni picha soon. TAFAKARI, CHUKUA HATUA!
Mkuu
Maswali ya msingi sana hayo. Hili sio suala la kujadiliwa kishabiki, linahusu objectivity katika journalism. Watamkasirikiaje RC ambaye ni sehemu ya source na kumwacha mwajiri wao.
Watakuwaje huru iwapo nao watakuwa sehemu ya mfumo!
Katika hili siwaungi mkono, wangetoa tamko la kugomea kazi za serikali yao ya mkoa hata wanene wajapo hapo ningewaelewa.
Watakuwa wanalilia posho za bahasha hawa
habari nilizopokea ni kuwa veta na green resource ya mufindi waliwalipa ila walitaka zaidi
Mkuu hiyo signature yako inakuondolea uhalali wa kuwa great thinker. Jitahidi uibadilishe tafadhali.Lipia tangazo ya blog yako!!!
Waandishi wa habari mkoani Iringa wamefanya maandamano yao kuelekea kwa MKUU wa MKOA kwa lengo la kulalamikia kunyanyaswa na Ofisa Habari wa Mkoa huo. Moja ya malalamiko yao ni kunyimwa posho wakati wa safari za viongozi mbalimbali mkoani humo. Nawaleteeni picha soon. TAFAKARI, CHUKUA HATUA!