Maana ya Ushirikina na aina zake

Maana ya Ushirikina na aina zake

Katika Miongoni mwa aina za Ushirikina




فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَانْحَرْ

“Basi swali kwa ajili ya Mola wako na chinja kwa ajili Yake.”[2]

Endapo mtu atafanya ´ibaadah akamfanyia asiyekuwa Allaah atahesabika amemfanyia ´ibaadah asiyekuwa Allaah. Kwa hiyo anakuwa mshirikina. Mtu akilichinjia jini au akamchinjia aliyemo ndani ya kaburi amefanya shirki. Kadhalika akilichinjia kaburi, nyota au walii anakuwa mshirikina. Mfano mwingine ni du´aa. Akimuomba asiyekuwa Allaah, kwa mfano mtu akamuomba uokozi asiyekuwa Allaah katika mambo yasiyoweza yeyote isipokuwa Allaah, mtu akaomba ponyo kutoka kwa asiyekuwa Allaah, mtu akaomba kuyaondosha matatizo kutoka kwa asiyekuwa Allaah, mtu akaomba msaada kutoka kwa asiyekuwa Allaah katika mambo yasiyoweza yeyote isipokuwa Allaah, mtu akaomba kinga kutoka kwa asiyekuwa Allaah katika mambo yasiyoweza yeyote isipokuwa Allaah au mtu akaomba uokozi kutoka kwa asiyekuwa Allaah katika mambo yasiyoweza yeyote isipokuwa Allaah. Yote haya ni shirki.
 
Katika miongoni mwa Shirki kubwa ni
Kuhalalisha aliloliharamisha Allah au kuharamisha alilolihalalisha Allah

Allah anasema ndani ya Quraan


أَمْ لَهُمْ شُرَكَاءُ شَرَعُوا لَهُم مِّنَ الدِّينِ مَا لَمْ يَأْذَن بِهِ اللَّـهُ

“Je, wanao washirika waliowaekea shiria katika Dini(yao)lile ambalo,Allah hajaliidhinisha kwayo”[3]
 
Kiujumla

Shirki ndio Dhambi kubwa zaidi,kuliko dhambi zote



Ni dhambi inayowatafuna watu weeeengi,ima kwa kujua au kutokujua

Wanaojiita Waislam ma wasiokuwa Waislam,wanaogelea katika hili


Tunamuomba Allah atuepushe na janga hili sisi na vizazi vyetu

Tunamuomba Allah atupe mwisho mwema
 
Ushirikina ni kufanya Ibada kwa asiyekuwa Allah, au kumchanganya Allah na kiumbe katika Ibada

ZINGATIO
Ibada ni nini?!
IBADA,ni jina lenye kukusanya,kila anachokipenda Allah na kukiridhia,katika kauli na matendo ya dhahiri au ya siri

Turudi katika mada
Uislam ndio Dini pekee inayopiga Vita Ushirikina na aina zake Allah anasema katika suratul Luqmaan akisimulia kisa cha mja mwema,pale akimuasa mwanae anasema Kumbuka aliposema Luqmaan kumwambia mwanae,ilihali akimpa nasaha,''Ewe mwanangu, usimshirikishe Allah,Hakika ya Shirki,ni dhulma kubwa''

AINA ZA USHIRIKINA
Ushirikina umegawanyika sehemu kuu mbili
1)USHIRIKINA MKUBWA
2)USHIRIKINA MDOGO


USHIRIKINA MKUBWA
Ni kufanya Ibada kwa asiekuwa Allah au kumchanganya Allah na kiumbe mfano Kuabudu Majini,Mizimu,Miti nk

Aina hii ya ushirikina inamtoa mtu katika Uislam

USHIRIKINA MDOGO
Shirki ndogo,ni sawa na riyaa(kufanya jambo kwa kujionyesha) Jambo hili,Halimtoi mtu katika Uislam,Bali lile tendo alilolifanya kisha akalichanganya na ushirikina mdogo,ndio tendo pekee litakalokataliwa kwamaana halitapokelewa na kukubaliwa kisheria

Tunamuomba Allah atuepushe na shirki na mfano wake
Amin
 
SABABU YA MSINGI YA KUUMBWA MWANA WA ADAMU

Ni Kumtambua Muumba wake na kumuabudu yeye pekee,bila ya mshirika


Allah anasema ndani ya Quraan
وما خلقت الجن والإنس إلا ليعبدون
Na sikuumba Majini na Watu,isipokuwa waniabudu mimi tu(pekee)

Tunaona katika aya hii tukufu
Sababu kuu ya kuumbwa viumbe hawa wawili,Majini na Wanaadam,ni kuja na kutekeleza maamrisho kamili ya Mola wao

Na neno IBADA,maana yake kamili ni

NI JINA LENYE KUKUSANYA,KILA ALIPENDALO ALLAH NA KULIRIDHIA,KATIKA MANENO AU MATENDO,YAWE YA WAZI AU YA SIRI


Hii ndio maana kamili na halisi ya Ibada
Tukiangalia maana ya Ibada tunapata yafuatayo

Kwanza kabisa
Neno au tendo ulifanyalo,liwe limeridhiwa na Mola wako na kupendwa

Tendo hili lenye mbawa mbili kuu
Kuridhiwa
Kupendwa
Ndio hubeba maana kamili ya Ibada

Kadhalika
Katika Ibada,kuna mgawanyiko
nao upo sehemu kuu mbili

1)IBADA ZA SIRI
2)IBADA ZA DHAHIRI/WAZI

Hizi zote,zitakuwa ni Ibada sahihi,ikiwa Allah anazipenda na kuziridhia

Baada ya kuona kwa ufupi maana ya Ibada

Tuangalie umuhimu wake katika maisha ya Binaadam
Allah anasema

ولقد بعثنا في كل أمة رسولا أن اعبدوا الله واجتنبوا الطاغوت

Na hakika tulipeleka katika kila Umma Mtume,(kauli kuu ya kila Mtume wa Allah ni kuwaambia watu)Muabuduni Allah,na jiepusheni na Twaaghuut

Ni nini maana ya Twaaghuut?!!
Twaaghuut maana yake kisheria

KILA KIUMBE MWENYE KUABUDIWA AKIWA RADHI,
Na Matwaaghuut wapo wengi sana,ila vinara wao ni watano(5)
1)Shetani/Ibliis
2)Kiumbe mwenye kuabudiwa akiwa radhi
3)Na mwenye kudai kujua mambo yajayo(mambo yaliyofichikamana)
4)Mtu mwenye kuwaita watu,katika kuabudiwa yeye tu
5)na mwenye kuhukumu pasi na sheria za Allah

Hawa watano,ndio vinara wa Matwaaghuut

Twaaghuut katika Lugha ya Kiarabu,maana yake

YULE MWENYE KUPETUKA/KUCHUPA MIPAKA ALIYOWEKEWA NA MOLA WAKE

Baada ya kuona haya machache
tunaona ya kwamba,Mola wetu Mlezi,Hakuna Nabii katika Manabii wake au Mtume katika Mitume yake,ila kauli kuu ili

AABUDIWE MOLA MMOJA TU
asie na mshirika

Ndg zangu

IBADA,ndio sababu kuu ya kuletwa Duniani na Mola wetu aliejuu

Basi turudini kwa Mola wetu aliejuu
Tumuabudu yeye tu pekee
Ni yeye tu,alie na sifa kamilifu,ni yeye tu
MOLA MMOJA
MWENYE KUTEGEMEWA NA VIUMBE WAKE WOTE
ASIE ZAA WALA KUZALIWA
ASIE NA MFANO NA YEYOTE

Nawatakia usiku mwema na maisha ya mafanikio
 
السلام عليكم ورحمة الله

Ndg zangu
Nataraji mpo salama pamoja na familia zenu

Kwa siku ya leo,in sha Allah nitapenda tuendelee kidogo na darsa yetu fupi
nayo
UBAYA WA USHIRIKINA

Tuangalie aya tatu(3)zilizopo ndani ya Quraan
AYA YA KWANZA
Allah anasema
وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا
Na amehukumu/amepitisha Mola wako,kwamba msimuabudu yeyote isipokuwa yeye tu,na ni juu kuwafanyie wema wazazi wawili

AYA YA PILI
Allah anasema
وَاعْبُدُوا اللَّهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا
Na muabuduni Allah na wala msimshirikishe na kitu chochote,na kwa ni juu kuwafanyia wema wazazi wawili

AYA YA TATU
Allah anasema
قُلْ تَعَالَوْا أَتْلُ مَا حَرَّمَ رَبُّكُمْ عَلَيْكُمْ ۖ أَلَّا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا
Sema,Njooni niwasomee yale aliyowaharamishia/aliyowakataza Mola wenu juu yenu
Msimshirikishe na kitu chochote,na juu yenu kuwafanyia wema wazazi wawili


Hizi aya tatu(3)
Zote zinakataza kushirikishwa Mola na kitu cha aina yoyote
na kutuamrisha Kumuabudu yeye tu wa pekee
Kadhalika,tunalazimishwa kuwafanyie wema wazazi wawili(Baba na Mama)

Ndg zang
Ushirikina ni mbaya mno kuliko dhambi ya aina yoyote ile
Tujihadhari sana na kila aina ya shirki

Tunamuomba Allah atupe mwisho mwema sisi na vizazi vyetu
 
Back
Top Bottom