Maamuzi ya CHADEMA Asilia

Maamuzi ya CHADEMA Asilia

Babeli

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2015
Posts
6,700
Reaction score
3,276
JF,

Kutokana na wimbi kubwa ambalo lilitukumba na hasa baada ya Mbowe na wenzake kuamua kukaribisha mafisadi CHADEMA, na kumfanye kamanda wetu Dr. Slaa kutimua.

Tumeamua kwa kauli moja wote na hasa baada ya hotuba nyeti ya kamanda wetu Dr Slaa, KUMPA KURA ZETU ZOTE DR. JOHN POMBE MAGUFULI ili sasa CHADEMA wote tujifunze kutokana na makosa makubwa tuliyofanya kwa utashi binafsi tu bila hata ya kushirikisha wanachama.

Tuna uhakika wapo wabunge wengi wako pamoja nasi ila wapo kimya kwa usalama wao.

KURA ZETU KWA MAGUFULI.

CHADEMA ASILIA WOTE TUSIMAMIE HILI

Cc. Dr. Slaa
 
Ni heri kukaa kimya kuliko kutoa hizo propaganda zako zilizokufa kabla hata hazijatolewa, ushindwe na ulegee!!!
 
Chadema asilia wakoje humu ndani? Njoo na account yako halisi kama mimi ili tuamini wewe ni Chadema asilia na kura yako ni kwa magufuli.
 
Si kuna Wilbard Slaa anagombea ubunge Karatu (CCM) kule kule kwa SLAA? Nendeni mkampe kura huyo mpunguze machungu!
 
wote wenye fikra kama zako hamkujua maana ya mabadiliko watanzania tunayoyataka.mabadiliko yanayotakiwa hapa si ya watu bali ni ya mfumo.

mfumo mbovu wa ccm ndo umezalisha richmond, eppa, escrow. hivyo hata aingie nani,katika mfumo mbovu wa ccm hakuna atakalo fanya.

jitambue mambo unayoshabikia usipelekwe na hisia tumia fikra kijana.magufuli na lowasa wanamaana kama mifumo watakayotumia itakuwa ni imara
 
Huwezi kutugawa kwa mtindo huo.Treni liko kwenye spidi kali Sana huwezi kulisimamisha

We unashabikia treni lipi spidi kali sana kulekea shimoni. Yaani unawahi kujizika mwenyewe.

Sio mimi ninae gawa wanachama ila hayo ni maamuzi ya Chadema asilia wote na ipo hivyo. Maadam tumedharauliwa kwa kuletewa kundi la mafisadi na Dr Slaa kuonekana hana maana tena kwa nguvu zake zote alizozitoa na hata kupata kilema kwa ajili ya chama chetu hatuna budi na sisi kuonyesha msimamo wetu.

Wengi wetu tulikuja chadema kwa kuvutiwa na Dr Slaaa na misimamo yake na wala sio Mbowe wala Lissu. Sasa ameondoka ni lazima tuwe nae bega kwa bega popote pale.
 
We unashabikia treni lipi spidi kali sana kulekea shimoni. Yaani unawahi kujizika mwenyewe. Sio mimi ninae gawa wanachama ila hayo ni maamuzi ya Chadema asilia wote na ipo hivyo. Maadam tumedharauliwa kwa kuletewa kundi la mafisadi na Dr Slaa kuonekana hana maana tena kwa nguvu zake zote alizozitoa na hata kupata kilema kwa ajili ya chama chetu hatuna budi na sisi kuonyesha msimamo wetu.
Wengi wetu tulikuja chadema kwa kuvutiwa na Dr Slaaa na misimamo yake na wala sio Mbowe wala Lissu.
Sasa ameondoka ni lazima tuwe nae bega kwa bega popote pale.

Ndani ya Chadema Asilia ndiyo iliko hekima ya kesho. Hili linajulikana hata na malaika mbinguni
 
JF,

Kutokana na wimbi kubwa ambalo lilitukumba na hasa baada ya Mbowe na wenzake kuamua kukaribisha mafisadi CHADEMA, na kumfanye kamanda wetu Dr Slaa kutimua.

Tumeamua kwa kauli moja wote na hasa baada ya hotuba nyeti ya kamanda wetu Dr Slaa KUMPA KURA ZETU ZOOTE DR JOHN POMBE MAGUFULI ili sasa chadema wote tujifunze kutokana na makosa makubwa tuliyofanya kwa utashi binafsi tu bila hata ya kushirikisha wanachama.

Tuna uhakika wapo wabunge wengi wako pamoja nasi ila wapo kimya kwa usalama wao.

KURA ZETU KWA MAGUFULI.

CHADEMA ASILIA WOTE TUSIMAMIE HILI

Cc. Dr Slaa

Ninyi vijana wa juzi bana mna shida sana. Wewe kamata chako, tambaa! Siku utakapoanza kulipa bills katika maisha yako, ndiyo itaingia na kukaa vema. Sasa hakuna unachojua; ati wewe leo ndiyo mtetezi wa Dr.W.Slaa!!! What a joke...

Hata ku-tag hujua ngoja tukusaidie ili huyo #Sellout mwenzenu akusome.

Cc: Dr.W.Slaa
 
Last edited by a moderator:
wote wenye fikra kama zako hamkujua maana ya mabadiliko watanzania tunayoyataka.mabadiliko yanayotakiwa hapa si ya watu bali ni ya mfumo.mfumo mbovu wa ccm ndo umezalisha richmond,eppa,escrow.hivyo hata aingie nani,katika mfumo mbovu wa ccm hakuna atakalo fanya.jitambue mambo unayoshabikia usipelekwe na hisia tumia fikra kijana.magufuli na lowasa wanamaana kama mifumo watakayotumia itakuwa ni imara
We unazungumIa mfumo upi ambao unadhani ukawa tunao? Tumia akili kidogo
1) kama Richmond ndio hiyo Lowasa ndio masternind
2) kama uuzwaji wa nyumba za serikali Sumaye ndio kinara wake.
3) kama mfumo wa uteuzi wa mgombea urais ukawa umekwenda kimabavu bila utaratibu uliopangwa
4) kama uteuzi wa mgombea mmoja wa ukawa kila jimbo hilo limeshindikana, chadema tumedharau Mbowe kasema tunaangalia mgombea mwenye nguvu utaratibu wa kila chama kwa mgao haukufuatwa kama mkataba ukivyokuwa.
5) kama miaka yote tulikuwa tunapambana na ufisadi na mafisadi leo ajenda hiyo imekufa kibudu. Sasa tunaenda ikulu kufanya nini. Tuna faida gani
6) vinara wa mfumo wa ccm ndio hao tumewachukua. Wanakwenda kuhamishia limfumo hilo huku kwetu. This is rubbish!
 
Ninyi vijana wa juzi bana mna shida sana. Wewe kamata chako, tambaa! Siku utakapoanza kulipa bills katika maisha yako, ndiyo itaingia na kukaa vema. Sasa hakuna unachojua; ati wewe leo ndiyo mtetezi wa Dr.W.Slaa!!! What a joke...

Hata ku-tag hujua ngoja tukusaidie ili huyo #Sellout mwenzenu akusome.

Cc: Dr.W.Slaa

Nimekupenda bure mkuu Nyunyu,heshima kwako.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom