Maamuzi magumu

Status
Not open for further replies.

Aigle

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2020
Posts
1,539
Reaction score
7,985
Duniani huku ukiwa masikini ni mateso tu, na kudharauliwa, lakini siamini ya kwamba tumeletwa duniani kuteseka au kudharauliwa sababu ya kutokuwa na pesa.

Sina kazi, nimefukuzwa nyumba ya kupanga, nalazimika kuomba hela ya vocha ili nije kupaza sauti yangu huku kwenye mitandao ya kijamii kama huu, pengine ntapata usaidizi. Sitakubali kunyanyasika hivi, hivyo basi wadau.

Kama kuna yeyote atakuja kuniunganisha na mtaalam wa ndagu za utajiri nitamshukuru sana, nimedhamiria na nipo tayari. Haya maamuzi hayajaja leo bali ni ya muda sasa, hadi kusema hivi ni maji yamefikia shingoni.

______________

Update

 
Duuh
 
Ngoja waje.
 
Naona mizimu ya ukoo wenu inakuambia rudi nyumbani kumenoga

Mkuu angalia tu usije tututoa kafara tusio na hatia maana maisha yenyewe mafupi usije tufupishia zaidi.. nikutakie kazi njema..
umenichekesha mkuu japo nina machungu yangu makubwa ila asante japo kwa kunifanya nicheke tu, ila maamuzi nishayapigia mstari hata sirudi nyuma.
 
"Kama kuna yeyote atakuja kuniunganisha na mtaalam wa ndagu za utajiri nitamshukuru sana,"

Kwa mawazo haya, utabaki kuwa masikini hivyohivyo . Badili fikra zako mapema.
hainibadilishi hii kauli, wengi mnaosema hivi hua ndio masikini zaidi
 
Utajiri wa kurithi hauna, utajiri wa zali la mentali kama betting au kuokota Tanzanite nao umeukosa.

Sasa cha msingi piga kazi sana piga kazi mno na uwe smart utatoboa.

Hakunaga utajiri wa "wataalam"
wewe wasema!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…