Maamuzi magumu tunayashuhudia katika awamu ya 5 siyo yale ya Lowassa kujiuzulu Uwaziri Mkuu!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,961
141,956
Katika awamu iliyopita ilijengeka dhana kwamba kwa kitendo cha kujiuzulu uwaziri mkuu Lowassa alikuwa amefanya maamuzi magumu. Wapo waliodai kuwa Lowassa ni Waziri Mkuu wa kwanza kujiuzulu kwa hiyari hivyo wakamwita Mzee wa maamuzi magumu. Mimi binafsi niliuchukulia uamuzi ule kama jambo la kawaida kabisa katika kuonyesha uwajibikaji. Ila niwe mkweli katika awamu hii ya 5 chini ya Rais Magufuli nayashuhudia maamuzi magumu yakifikiwa na kutekelezwa na lililonifurahisha zaidi ni yale maandamano yaliyoratibiwa ughaibuni yalivyosambaratishwa. Nilimsikia Rais akiliambia taifa kuwa maandamano yale ni haramu na ole wake atakayethubutu kutia miguu yake barabarani kuandamana. Na jana tukashuhudia nchi ikiwa shwari na leo jamii nzima ya watanzania wakiwemo Chadema wamemkana Mange Kimambi. Mange amebakia mpweke akilia na kusaga meno huko America......haamini kilichotokea. Hayo ndio maamuzi magumu ukisema hapana lazima ionekane kuwa ni hapana hakuna kuchekacheka. Ahsante!
 
IMG_20180421_082732.jpg
 
Katika awamu iliyopita ilijengeka dhana kwamba kwa kitendo cha kujiuzulu uwaziri mkuu Lowassa alikuwa amefanya maamuzi magumu. Wapo waliodai kuwa Lowassa ni Waziri Mkuu wa kwanza kujiuzulu kwa hiyari hivyo wakamwita Mzee wa maamuzi magumu. Mimi binafsi niliuchukulia uamuzi ule kama jambo la kawaida kabisa katika kuonyesha uwajibikaji. Ila niwe mkweli katika awamu hii ya 5 chini ya Rais Magufuli nayashuhudia maamuzi magumu yakifikiwa na kutekelezwa na lililonifurahisha zaidi ni yale maandamano yaliyoratibiwa ughaibuni yalivyosambaratishwa. Nilimsikia Rais akiliambia taifa kuwa maandamano yale ni haramu na ole wake atakayethubutu kutia miguu yake barabarani kuandamana. Na jana tukashuhudia nchi ikiwa shwari na leo jamii nzima ya watanzania wakiwemo Chadema wamemkana Mange Kimambi. Mange amebakia mpweke akilia na kusaga meno huko America......haamini kilichotokea. Hayo ndio maamuzi magumu ukisema hapana lazima ionekane kuwa ni hapana hakuna kuchekacheka. Ahsante!
We siyo mzima, jana mtu kashindwa kuingia na gari ya wazi au umesahau?
 
Badala ya kumuonea huruma jinsi alivyotaabishwa na kukoseshwa usingizi na kabinti kadogo tu, akatumia gharama kubwa ya fedha, muda na juhudi kupambana na binti huyo ambaye ameratibu kila kitu kupitia mitandaoni na kufikisha taarifa kwa watu wachache tu, wewe unaigeuza kuwa sifa na kumpamba ili tu akufurahie! Haya, endeleeni kumpigia vigelegele.

Binafsi hakuna wakati niliuona unyanya wa serikali yetu kama jana.
 
Kuna watu wanaongea tu kama kasuku.CAG alikanusha hajaona matumizi ta 1.5tr. Nyie na mzito wenu mtuambie mmetoa wapi hizi data
 
kuna watu utanzania wao unatia mashaka. ripoti ukurasa wa 34 iko wazi. wengine ni majini visirani kwa kweli.
 
A - Rais wa nchi ameacha Shughuli nyingi sana na kumfikiria Dr. Mange
B - Vyombo vyote vya Dola Vikahangaika na Dr. Mange
C - Vyombo ya Kimataifa vimejua hali halisi ya Tanzania
D - Serikali inapambana na wananchi, Je nani wanamuunga mkono huyo Jiwe?
E- Kwa nini aogope maandamano kama anafanya vitu vizuri kwa wananchi, Na wanampenda

Tupo Gizani: Maswali na hoja za wananchi bado kujibiwa

1 - 1.5 Trillioni ziko wapi?

2- Uhuru wa habari na demokrasia?

3 - Unafungia social media lakini hunyongi mafisadi (Eti kama china)

4 - Mafao ya Jamii - CCM na Serikali yake imetafuna

5- Sukari Jiwe akapandisha kutoka 1800 hadi 2800

6- Uchumi Jiwe ameua

7 - Ajira hakuna kabisa

Kejeli za vilaza wachache wa Lumumba, haziwezi kuzima hoja hizo hapo juu.

Vijana wa Lumumba wanalipwa special allowance ili kulinda mkate wa wachache, wanao tafuna keki ya taifa

-Wanajua fika kuwa hoja zao ni dhaifu Mbele ya Jukwaa hili la JF ---Ndio maana Bwana mkubwa analalamika Watanzania kuamini mitandao ya Jamii

Pili, Ni wazi kuwa Mikataba Feki walioingia CCM na Serikali yake ndio wanaibia nchi hii. Bado Wezi na Mabwanyenye wanaiba sana, kwa akili nyingi..Kwa sababu Mikataba bado ipo

CCM wakaingia mkataba na CHina na gesi ya Mtwara haina faida tena

Hivi waliingia mikataba mibaya ya kufilisi nchi si bado wako CCM

Au je, Mahakama ya Mafisadi imefunga wangapi? Vijana wa Lumumba, endelezeni njaa na kuwasaliti Watanzania.
 
Uharamu wake ni upi? Nyie mnapendwa mpk watu wanajiuzulu nafasi zao kuwa support. Mnaogopa nini kuzuia maandamano kwa nguvu zote hizo za nini wkt mnapendwa kwahiyo yasingefanyika? Am getting a feeling kwamba huwa mnawnunua siyo bure. Praise the lord
 
Achana na hizo longo longo za Zitto, ndege ya 7 inakuja nakuhakikishia Zitto atakuwa wa kwanza kuwahi apande!

Anapanda bure au ni hela yake inaongea? Kabla ya hizo ndege zenu hajawahi kupanda ndege. Acho utoto dogo.
 
A - Rais wa nchi ameacha Shughuli nyingi sana na kumfikiria Dr. Mange
B - Vyombo vyote vya Dola Vikahangaika na Dr. Mange
C - Vyombo ya Kimataifa vimejua hali halisi ya Tanzania
D - Serikali inapambana na wananchi, Je nani wanamuunga mkono huyo Jiwe?
E- Kwa nini aogope maandamano kama anafanya vitu vizuri kwa wananchi, Na wanampenda

Tupo Gizani: Maswali na hoja za wananchi bado kujibiwa

1 - 1.5 Trillioni ziko wapi?

2- Uhuru wa habari na demokrasia?

3 - Unafungia social media lakini hunyongi mafisadi (Eti kama china)

4 - Mafao ya Jamii - CCM na Serikali yake imetafuna

5- Sukari Jiwe akapandisha kutoka 1800 hadi 2800

6- Uchumi Jiwe ameua

7 - Ajira hakuna kabisa

Kejeli za vilaza wachache wa Lumumba, haziwezi kuzima hoja hizo hapo juu.

Vijana wa Lumumba wanalipwa special allowance ili kulinda mkate wa wachache, wanao tafuna keki ya taifa

-Wanajua fika kuwa hoja zao ni dhaifu Mbele ya Jukwaa hili la JF ---Ndio maana Bwana mkubwa analalamika Watanzania kuamini mitandao ya Jamii

Pili, Ni wazi kuwa Mikataba Feki walioingia CCM na Serikali yake ndio wanaibia nchi hii. Bado Wezi na Mabwanyenye wanaiba sana, kwa akili nyingi..Kwa sababu Mikataba bado ipo

CCM wakaingia mkataba na CHina na gesi ya Mtwara haina faida tena

Hivi waliingia mikataba mibaya ya kufilisi nchi si bado wako CCM

Au je, Mahakama ya Mafisadi imefunga wangapi? Vijana wa Lumumba, endelezeni njaa na kuwasaliti Watanzania.
Dah....umevuta?
 
Back
Top Bottom