Moja ya Maamuzi Magumu ya JK ilikuwa kukulazimisha wewe Lowassa Kujiuzulu; Asema Nape Nauye

Jun 8, 2011
52
19
nape-mjumbe.jpg


Akizungumza katika mahojiano na Radio Safari ya mjini Mtwara hivi karibuni Nape amesema serikali ya Rais Jakaya Kikwete ndiyo pekee katika nchi hii iliyokwisha kutoa maamuzi magumu kuliko serikali zote zilizopita.

Nape amenukuliwa akisema...." uamuzi mgumu wa kwanza uliotolewa na serikali ya awamu ya nne ni kwa yeye Lowassa kulazimishwa kujiuzulu, kuvunjwa Baraza la Mawaziri, kuwafungulia kesi kina Mramba na Yona, kuivunja kamati kuu ya CCM na sekretarieti, Ujenzi wa chuo kikuu cha Dodoma na Ujenzi wa shule za kata".
 
Nape hebu kuwa mkweli:
  1. Lowassa kulazimishwa kujiuzulu-ni uamuzi wa JK? au ni nguvu ya umma?
  2. kuvunjwa Baraza la Mawaziri-hii ni kwa mujibu wa katiba na wala si uamuzi wa JK. Waziri Mkuu akijiuzulu automatically baraza linavunjika
  3. kuwafungulia kesi kina Mramba na Yona-halafu akampigia kampeni Mramba.Inaingia akilini kweli?
  4. kuivunja kamati kuu ya CCM na sekretarieti-ambayo aliweka mwenyewe ikamwangusha kwenye uchaguzi kwa kupata kura chache
  5. Ujenzi wa chuo kikuu cha Dodoma na Ujenzi wa shule za kata- haya ni majukumu yake na alitumia pesa za umma na wafadhilki na katu si uamuzi mgumu
 
Maamuzi mengine magumu aliyofanya Jk ni kumshika mkono juu na kumnadi Pesambili Mramba na kusema jembe la zamani haliishi makali! Chukua hiyo Nape ukipenda naomba uipotezee!
 
nape-mjumbe.jpg


Akizungumza katika mahojiano na Radio Safari ya mjini Mtwara hivi karibuni Nape amesema serikali ya Rais Jakaya Kikwete ndiyo pekee katika nchi hii iliyokwisha kutoa maamuzi magumu kuliko serikali zote zilizopita.

Nape amenukuliwa akisema...." uamuzi mgumu wa kwanza uliotolewa na serikali ya awamu ya nne ni kwa yeye Lowassa kulazimishwa kujiuzulu, kuvunjwa Baraza la Mawaziri, kuwafungulia kesi kina Mramba na Yona, kuivunja kamati kuu ya CCM na sekretarieti, Ujenzi wa chuo kikuu cha Dodoma na Ujenzi wa shule za kata".


Safi sana, Nape Nnauye na Samuel Sitta wamemjibu vizuri sana Lowassa. Yeye anajigamba kwa kufanya maamuzi magumu gani, kuchukua mlungula wa Richmond? Haya ndiyo majibu ya kumgonga nayo Lowassa kwa tuhuma zake lukuki za ufisadi. Next step iwe kumpeleka mahakamani. Ukicheza na Mbwa atakufuata mpaka msikitini!
 
Lakini hii ndivyo inavyoonyesha saa nyingine kuwa kijana na Madaraka hakuna heshima kwa Wazee ambao walishika Madaraka kable yake; Nadhani hata wakati wa Uchaguzi wa Kikwete, hajui Lowassa alihusikaje mpaka Kikwete akachaguliwa kuwa Rais; Haonyeshi Heshima? hii ndio hasara ya Utami wa madaraka ya CCM, kweli CCM haingalii ilikotoka.

Kama kwa Sababu ni Fisadi, Mafisadi wengi kweli ndani ya CCM hawakuanza wakati wa utawala wa Kikwete; Ni Tangu Azimio la Zanzibar toka Utawala wa Awamu ya PILI. Kweli CCM mna matatizooooo...
 
Maamuzi magumu nikugeuza kigoma kuwa dubai ya tanzania na kununua meli katika maziwa yote tanganyika,victoria na nyasa na kuchagua kulindwa na marehemu shehe yahaya.
 
nape-mjumbe.jpg
Akizungumza katika mahojiano na Radio Safari ya mjini Mtwara hivi karibuni Nape amesema serikali ya Rais Jakaya Kikwete ndiyo pekee katika nchi hii iliyokwisha kutoa maamuzi magumu kuliko serikali zote zilizopita.Nape amenukuliwa akisema...." uamuzi mgumu wa kwanza uliotolewa na serikali ya awamu ya nne ni kwa yeye Lowassa kulazimishwa kujiuzulu, kuvunjwa Baraza la Mawaziri, kuwafungulia kesi kina Mramba na Yona, kuivunja kamati kuu ya CCM na sekretarieti, Ujenzi wa chuo kikuu cha Dodoma na Ujenzi wa shule za kata".
Tuwekeeni "wimbo" mwingine tafadhali, huu wa maamuzi magumu umechosha masikio, naona sana ni makelele tuuu..!!
 
Hata kumtetea Ngeleja ni maamuzi magumu sana yaliyofanywa na JK. Kwa kuwa si rahisi mtu mwengine kumtetea mtu kama Ngeleja.
 
maamuzi mengine magumu ni kukaa hewani kuliko kiongozi mwingine yeyote bila kuhofia kama ndege itaanguka.
 
nimerejea. Nape ni mwongo mkubwa sana kudai eti serikali hii ndo iliyowahi kuchukua maamuzi makubwa kuliko serikali zote.

Kwa taarifa yake serikali ya kwanza na ya pili zimechukuwa maamuzi mazito mara nyingi sana. Pia serikali yya awamu ya tatu nayo imechukua maamuzi mengi makubwa yenye faida kuliko hawa maf..a..la wa awamu ya nne waliochukua maamuzi ya kutuweka gizani mwaka wa tano sasa. Serikali inayowasafisha mafisadi. Serikali inayowapa watu siku tisini kisha inasema haikuwapa. Serikali hii inayosema haitaki kura za wafanyakazi kwa kuwa ilikuwa na uhakika wa kuiba kura.

Naichukia hii serikali na magamba kuliko maelezo. Inayafanya maisha kuwa magumu kila siku. Pesa haipatikani halafu haina thamani. Huduma kama elimu zinakumbwa na migogoro kila siku. Ni serikali inayoongoza kwa migomo halafu. Serikali ambayo maamuzi makubwa zaidi kuwahi kuyafanya ni kupanga safari za nje kila baada ya siku chache.

Nape ni mpu...zi sana na digrii yake ya Kihindi nadhani amesomea vyuo vya mkabala na....maana hana logiki katika maongezi yake. Ni kilaza aliyeteuliwa na kilaza gentleman.
 
Kama kweli Nape kasema hata kujenga UDOM na shule za kata ni maamuzi magumu sasa naanza kujuliza kwa nini kapewa nafasi hiyo.

Alitaka serikali isijenge shule halafu iweje. Wamejenga shule kwa sababu ndiyo moja ya kazi zake na pesa za wananchi pamoja na nguvu zao zilitumika. Pengine Nape haelewi maana ya hii sentensi: "Fanyeni maamuzi magumu" msaidieni jamani.
 
Kwa hili la shule za kata pamoja na Ujenzi wa UDOM nape muogope mungu anayestahili credit hizo ni LOWASA kwani ni juhudi zake binafsi ndizo zilizofanikisha hayo yote na siyo serikali kama unavyohubiri.
 
Wasiwasi wangu huyu bwana anacheza ngoma asiyoijua! aombe Mungu mabo yasiharibike, otherwise . . . . .
 
Safi sana, Nape Nnauye na Samuel Sitta wamemjibu vizuri sana Lowassa. Yeye anajigamba kwa kufanya maamuzi magumu gani, kuchukua mlungula wa Richmond? Haya ndiyo majibu ya kumgonga nayo Lowassa kwa tuhuma zake lukuki za ufisadi. Next step iwe kumpeleka mahakamani. Ukicheza na Mbwa atakufuata mpaka msikitini!


Pumbavu wewe una ushahidi wowote kuwa lowasa alichukua mlungula wa Richmond? Hizo ni propaganda za ccm ili kuwaangalia hao wanao itwa mapacha watatu mkasahau matatizo makubwa ya nchi. Tumetengenezewa chuki kwa hawa watu ili kila unapolala njaa unakumbuka Lowasa, umeme ukikatika unakumbuka lowasa maji yakikatika Lowasa, hatakama lowasa ni mbaya lakini si source of our problem, source is CCM, Tuna sherehekea 50 yrs nchi ikiwa masiki, wameshindwa wakae kando.
MAAMUZI MAKUBWA NA MAGUMU YA KIKWETE NI KUJIUZULU NA KUITISHA UCHAGUZI
 
Pumbavu wewe una ushahidi wowote kuwa lowasa alichukua mlungula wa Richmond? Hizo ni propaganda za ccm ili kuwaangalia hao wanao itwa mapacha watatu mkasahau matatizo makubwa ya nchi. Tumetengenezewa chuki kwa hawa watu ili kila unapolala njaa unakumbuka Lowasa, umeme ukikatika unakumbuka lowasa maji yakikatika Lowasa, hatakama lowasa ni mbaya lakini si source of our problem, source is CCM, Tuna sherehekea 50 yrs nchi ikiwa masiki, wameshindwa wakae kando.
MAAMUZI MAKUBWA NA MAGUMU YA KIKWETE NI KUJIUZULU NA KUITISHA UCHAGUZI
dah muvi kali sana hili.... nitalicheki hadi mwisho
 
Back
Top Bottom