Taarifa Inasema Maalim Seif Sharif Hamad atazungumza na wandishi wa habari mchana wa leo
----------
UPDATES FROM HIGH COURT DAR ES SALAAM:
Tarehe 18 March, 2019
----------
Mahakama Kuu mbele ya Jaji Benhajj Masoud, imeliondoa (Struck Out) shauri Namba 23/2016 lililokuwa linahoji Uhalali wa Lipumba ndani ya Chama cha CUF. Kwa hoja za kiufundi (Legal Technicality) aidha, Jaji ameeleza kuwa Msajili alikuwa na Mamlaka ya kufanya kile alichokifanya kumrejesha Lipumba ndani ya CUF.
PRESS CONFERENCE:
Maalim Seif Sharif Hamad atazungumza na Waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini katika Mkutano utakaofanyika Leo tarehe 18/3/2019 katika Ukumbi wa Wabunge wa CUF uliopo Magomeni –Dar es Salaam.
Muda: Saa 8:00 mchana .
Nyote Mnakaribishwa.
Imetolewa leo Tarehe 18/3/2019 na;
MBARALA MAHARAGANDE
======
MAALIM SEIF ATANGAZA KUJIUNGA NA ACT-WAZALENDO
Mwanasiasa mkongwe na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF ametangaza kukihama chama hicho na kuhamia ACT Wazalendo
Maalim Seif ametangaza uamuzi huo mchana huu
Wamachama wa CUF wanaomuunga mkono Maalim Seif walianza kubadili tangi za ofisi za chama hicho saa chache kabla ya kiongozi wao kutangaza kuhama
Aidha kwenye matawi mengine ya CUF bendera ya chama hicho imeshushwa na kupandishwa ya ACT Wazalendo