Maajabu yaliyotokea Chalinze!

Maajabu yaliyotokea Chalinze!

NILICHOSHANGAA CHALINZE:-
Jimbo ambalo JK amekuwa akiliongoza kwa miaka 15 tena amekuwa waziri, Na miaka 9 sasa akiwa Rais

  1. Mtandao wa simu unaopatikana ni Airtell tu!!..yaani akiacha chalinze mjini tu, kwingine kote hakuna mtandao wa Vodacom, Tigo wala Zantel !! Du! Hata Samunge kwa babu kunapashinda Chalinze!!

--Nikajiuliza huyu mkuu wa kaya yaani ameshindwa kushawishi hata makambuni ya simu kuweka minala huku, wananchi wake wawe na uhakika japo wa mawasiliano ya simu tu!
Huu ni dhaifu ya udhaifu!! Huku ni zaidi ya kutojali nyumbani!! huku ni ziadi ya kudhalau wananch wako!!


  1. Kata ya Mkange kijiji cha Tumbilini kuna jengo moja la hospitali linaloonekana halituki na halijamalizwa kujengwa. Wenyeji wanasema ni miaka kadhaa sasa, halijawahi kuletwa daktari wala madawa hamna, hvyo wakiumwa hulazimika kutembea takribani kilometa 8 kutafuta matibabu kwingine.

…Nikapata picha bila shaka hili lilianza kujengwa wakati wa kampeni, baada ya mkuu kushinda kawatelekeza !!


  1. Zaidi ya asilimia 90 ya maeneo ya jimbo hili hayana umeme, wala maji!


  1. Miundo mbinu ni mibovu sana, japo hakuna barabara ya lami zaid ya ile iendayo mikoani, hizi barabara za “vumbi” zilizopo hazina maboresho yoyote kwa miaka kenda sasa!


  1. Zaidi ya asilimia 50 ya wakazi wa jimbo hili hawajui kusoma wala kuandika…(hii ni kwa mujibu wa takwimu za watu waliokuja kupiga kura, mawakara na vijana niloongea nao )


  1. Kwa asilimia kubwa Jimbo halina shule japo za kata! Na hata zile chache zilizopo zimechoka vibaya sana..yaani VIBAYA SANA!! .. hazina madirisha,hazina milango,hazina paa,hazina vyoo,zimechakaa sana..kama hvyo vyamsingi kabisa hazina, shule hizo kuwa na umeme na maji ni ndoto za mchana!

MISHANGAO MINGINE :

  1. Utitiri wa magari ya serikali,magari ya mashirika ya uma, magari ya polisi, magari yenye namba za DFP,SU nk. Inashangaza, utitiri wa viongozi wa kiserikali,kipolisi,..mmh mpaka Raisi wa Znz naye alikuja!! Mheshimiwa Rais kabisa kabisa naye kwenye kampeni za jimbo tu!! Kisa mtoto wa mkuu anagombea…hii ni AIBU zaidi ya kushangaza!


  1. Kituo kimoja kilicho karibu na hifadhi ya Saadani, kilikuwa na idadi ya wapiga kura 320 lakni walijitokeza 20! Niliwauliza baadhi ya wananchi kwanini, hawakujitokeza walijbu kwa kulalamika.

….”Huyu mt0to wa kikwete kagawa elfu kumi- kumi kwa wengine na sisi katuacha, na sisi tumedhila na hatuendi kumchagua!! “….. Nilishangaa!! nikawuliza… kwanin sasa msingeenda kumchau mwingine nanyi mumkomeshe!!..walijibu…”..ahaa tunaogopa kufungwa!”.Kwa kweli, inasikitisha watu wamejazwa imani ya woga!!! Hawaamini hata kuwa kura ni huwa siri kweli kweli!


  1. Kijiji kimoja cha Miono, wanakijiji waliongea wazi kuwa Riz alikuja akawapa wali wakala kaondoka bila kufanya kampeni yoyote ya kisiasa. Na wao wamempa kura zao!! Hahaha.. Nlishindwa kujizuia kucheka ni kama comedy flani, lkn kwa kweli ukifikiria fikra za hawa watu inasikitisha sana..utawaonea huruma tu.


  1. Pamoja na ccm kushinda, wakazi wa jimbo hili hawaonyeshi kushangilia wala shamla shamla zozote! Wanaoshangilia ni wale wachache waliokuja waliokuja kwa “kazi maalumu” tu!


  1. Pamoja na CHADEMA kushindwa lkn kila zilipopita gari za M4C wananchi walishangilia na kuonyesha ishara ya vidole viwili!


  1. Wapiga kura wengi ni wazee, vijana wengi hawamo kwenye daftari la kura. Na wengi wa wazee hawa walikuwa wakiletwa na bodaboda takibani 100 ambazo inaonekana ziliandaliwa kwa shughuli hii.


  1. Wananchi wengi walioongea wazi wazi kuwa wamechagua ccm kwa sababu ya posho walizopewa tu! Lakini hawana mapenzi na ccm. Binafsi niliwasikitikia sana watu hawa..yaani wa nauza haki yako, utu wako kwa sh 5000/- au 10,000 !! ..kwa posho !!!..INASIKITISHA SANA!!

MSHANGAO MKUBWA ZAIDI :
Mtoto wa mkuu wa kaya kaahidi kujenga mashule, mahospitali,barabara,kuleta maji na umeme, n.k..kwa mwaka 1 na nusu tu alionao! Wakati mkuu wa mwenyewe kashindwa kwa miaka yote hiyo akiwa mmbunge,waziri na hata raisi!! watoto wa mjini wanaweza kuita hili..CHANGA LA MACHO…..LIVE- LIVE!!.

“WANACHALINZE WAMELUKA MKOJO WAMEKANYAGA MAVI”
sehemu zote zenye matatizo makubwa kama hayo uliyoyataja ndio mtaji wa ccm,ccm hawawezi kushinda sehemu zenye maendeleo na wasomi, ccm hushinda sehemu kama hizo zisizokuwa na wasomi na zenye maendeleo duni
 
Watu wa huko hayo yote hayawahusu! Ukipiga marufuku ngoma tu ndipo utakua umewagusa! Usiwaingilie kwenye utamaduni wao!
 
Wahafidhina tunawaambia kila siku badilisheni siasa zenu, na mara zote mnaona mapungufu ya wenzenu. Sasa oneni na yenu ili mbadilike, mnakosa mno wakati semeni mtafanya nini na mmefanya nini. Waambie wapiga kura kama mmeacha ukaskazini na kudumisha fikra za viongozi wenu. Fanyeni siasa tofauti wenzenu wanaenda kimya kimya nyie mnapayuka sana ndio maana mnakula za uso, muache kuwaiga viongozi wenu sauti kuweni real.
 
attachment.php

asante kwa ushahidi wenye vielelezo .
 
Kwa hiyo ina maana wewe umeona mabaya tu! mazuri yaliyofanyika hakuna hata moja??? na kama lipo japo moja mbona hujaandika au unataka kutuaminisha nini

mbona wewe hujatuwekea hayo unayosema ni mazuri ?
 
Kaka 86.6% (wa kishindo)itakuuma sana! Hayo mambo uliyoongea ungekwenda na Chopa ili watoto wakasikilize na wahsngae chopa,but for now its too late! RIP Chagadema!

hii ndiyo post ya kichovu sana !
 
hivi JK mwaka 2010 alipigia kura wapi maana jana kapiga kuza huko jimbo la chalinje 2010 alipigia kura dar auimekosea naulizo tu jamani
 
Wataalam wa demokrasia wanasema huwezi kujenga demokrasia ya kweli katika jamii ambayo watu wengi ni maskini na hawana elimu. Mjinga ni rahisi kudanganywa, kuuza uhuru wake, kuacha kutumia haki yake, na hata kutishwa. Na pia mtu mjinga si rahisi kujua vipaumbele vyake. Ndiyo maana ukichunguza kwa umakini CCM inaungwa mkono zaidi maeneo ambayo elimu ni duni sana na umaskini umekithiri. Kwa kiasi kikubwa CCM inachukiwa na wasomi wengi. Angalia uungwaji mkono wa CCM upoje katika mashule na vyuo, na kwenye miji mikubwa mingi ambako ndiko inakojulikana watu wenye upeo wapo.

Watakaoiondoa CCM madarakani ni wahitimu wa shule za kata. Hawa japo hawapati elimu bora lakini wanaelimu ya kujitambua.

Yawezekana unayosema yakawa ya kweli. Lakini mmmh! Ebu turejee kwenye jiji la Salaam, mbona hali haishabiiani na hicho ulichosema au ndo hiyo kanuni haufanyi kazi kila sehemu.
 
Porojo hazitaisaidia CHADEMA kutoporomoka zaidi kisiasa,Jitathimini upya kama Taasisi na mkijenge upya Chama chenu.Msiwe kama yule Waziri wa Propaganda wa Iraq Ally Chemicals.Shauri yenu.

mkuu sio chemical ally yule wazir alekuwa msrmaji mkuu wa serikali ya irak wakati wa vita alikuea ni jeneral mohammed saeed al. sahhaf. daah mkuu umenikumbusha mbali sana na alsahaf wa chadema ni slaaa manenoo mengii ya uongo ila vitendo ziroo
 
Sidhani usemi huu una ukweli wowote ndani yake. Kwa mwanasiasa na mwanajamii yeyote hufurahia maendeleo - na kulaani kitendo cha kuwaacha wananchi katika limbu la maskini kiasi cha kupoteza ujasiri wa kukubali au kukataa wanachoambiwa. Kilio chetu kimekuwa siku zote kukomboa watu kwenye umaskini na sasa hivi ni muhimu kuelekeza nguvu ukanda wa pwani, kwani huko umaskini umeshamiri.

Tabu na changamoto kubwa ni kuaminika kwa watu waliokolezwa tororo na umaskini! Watakusikiliza lakini ni waoga sana kukubali mabadiliko, kwani kwa maskni hii ni 'risk' kubwa mno, yaani wanahofu hata kile kidogo walicho nahco chaweza kupokonywana mageuzi. Tuzidi kuwahimiza tu watu wapende kuukataa umaskini!

Katika khali hii Kikwete angekuwa amewafanyia upendeleo, upendeleo huo ni sawa kabisa! Unaitwa positive discrimination kwani una tija kwa taifa na jamii

Haya tulia basi , kesho nisikusikie unalalama hapa kwamba kwanini bandari inajengwa Bagamoyo.
 
Back
Top Bottom