Maajabu ya ndoa: Unapewa cheti kabla ya mitihani

Maajabu ya ndoa: Unapewa cheti kabla ya mitihani

ALU255

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2015
Posts
2,089
Reaction score
2,125
Tofauti na tulivyozoea katika ngazi nyingi za elimu duniani unafanya mitihani ndipo upate vyeti lakini kwenye ndoa ni kinyume unapata kwanza cheti ndipo unakutana na mitihani na mitihani yake ni migumu sana nahisi labda ndo sababu wanatoa cheti kabisa,unaweza kukutana na mitihani kama hii kwenye ndoa, Kuchapiwa, Michepuko, Careless, Usaliti, Kiburi, Umaskini, UKIMWI, n.k

Hiyo yote unaweza kukutana nayo kwenye ndoa bila matarajio yako mwenzako anaweza kukufanyia muda wowote na ukishndwa mtaishia kuachana na mkishaachana vyeti havina kazi yoyote tena rai yangu naona ingekuwa vizuri vyeti vya ndoa vingetolewa atleast baada ya miaka mitano wanandoa wafanye mitihani kwanza wakifaulu wapate vyeti vyao na sio vyeti kabisa mtu anafanya anavyotaka kisa ameshapata cheti cha ndoa.

* * * * * * *
 
Kwasababu ungepewa baada ya huo mtihani(ndoa) hakuna ambaye angepasi. Wote wangeishia njiani na kutafuta mwingine
 
Kile chet sio cha kupasi wala kufeli Kile cha makabidhiano kama manunuzi ya nyumba gari shamba. Sawa sawa
 
Umejaribu kujenga hoja yako bila kufikiri inavyotakiwa.

Kwanza cheti sio mwisho wa matatizo! Hata wanaohitimu elimu za darasani wanajua kupata cheti sio tiketi ya ajira au utaalamu wa hali ya juu.

Cheti cha ndoa na cha kitaaluma havijatofautiana malengo! Vyote vina kazi moja tu; kuwatambulisha wahusika kwenye jamii kwamba wao ni wataalam/wanandoa ili kupata haki stahiki kutokana na hadhi zao.

Cheti cha ndoa kinakutambulisha kwamba wewe ni mme/mke wa fulani, hii inasaidia kupata haki zako hata za kiaheria pindi unaona kuna mtu anakuchukulia mme/mke wako, sawa na kwenye taaluma, cheti ndicho kinahalalisha ujuzi ulio nao wakati unatafuta ajira! Bila cheti hata uwe mtaalamu vipi huwezi kupata ajira kwenye taasisi inayoamini kwenye elimu ya darasani/taaluma/vyeti.

Kwa utangulizi huo naamini umeelewa cheti ni nini na nini kazi yake. Kuhusu hoja ya kupewa cheti kama ufaulu kabla ya mtihani, nimeelezea kwenye hapo chini.

Kabla ya ndoa kuna hatua ambazo wahusika wanapitia kabla ya kuhalalishwa kama wanandoa kwa kupewa vyeti kama ilivyoelezwa kwenye mada.

Hatua kubwa inayojulikana ila haileweki vyema ni uchumba. Hatua hiyo ndio mtihani wenyewe, ukiona unapewa cheti basi maana yake ulishinda kwenye hatua hizo kwa kuvuka vikwazo vyote, hata hivyo kiuhalisia ni wengi sana wanaopewa vyeti bila kuruka vikwazo vilivyopo kwenye uchumba, na kwa kuwa sio kazi ya mchungaji, sheikh au padri kuchunguza mahusiano yenu, wao hawana sababu ya kutokukupa cheti, maana ndoa yako ni yako, wao haiwahusu.

Nimesema hapo juu kwamba, uchumba ni hatua kubwa isiyoeleweka kwa sababu, watu wengi hawajui madhumuni yake au wanapuuza, ndio maana tunashuhudia ndoa nyingi zikiwa zinaenda kombo kwa kuwa wahusika waliruka ngazi ya kwanza hadi ya tatu bila kukanyaga ya pili.

Uchumba upo kwa dhumuni la kuchunguzana tu kujua ikiwa fulani anafaa kuwa mke/mme au hafai. Katika uchumba huo ndipo unapopimwa uvumilivu, upendo, heshima na adabu, mapenzi ya dhati, ukarimu nk. Kwa siku za sasa maana ya uchumba imepindishwa! Watu wanafikiri uchumba ni kushiriki ngono kitu ambacho si cha kweli na hakitakiwi kwenye hatua ya uchumba.

Hivi unawezaje kujua ikiwa mme/mke wako wako ataweza kustahimili vishawishi vya mwili(ngono) ukiwa upo mbali naye labda masomoni nje ya nchi au hata shughuli za kazi/biashara ikiwa wakati wa uchumba umekuwa ukishiriki naye kwenue ngono?

Utawezaje kujua mke wako atakuwa mvumilivu pale utakapopungukiwa pesa au kufilisika ikiwa katika uchumba wenu umekuwa ukimpa pesa anapokuomba au hata pale asipokuomba?

Nimalizie kwa kusema hivi; uchumba ndio darasa lenyewe ambapo nadharia zote za mapenzi ndipo zinapokuwa. Umakini wako kwenye hatua hiyo(uchumba) ndio unaamua ndoa yako iwe vipi sio cheti. Ukikosea uchumba utakuwa umekosea ndoa/kuoa pia kwa sababu mitihani inayoitwa ya ndoa kimsingi inaonekana wazi kwa wale wanaojua uchumba nini, na ndio maana kwa wakristo inasemwa kwamba, ikiwa unaona hamuendani mkiwa kwenye uchumba ni bora kuvunja uchumba mapema ili kuepuka matatizo kwa sababu ndoa ya kikristo haivunjwi popote pale.
 
unafanishaje ndoa na elimu ya darasani??? how??
 
Chet cha ndoa unapewa ili kukuidentfy kuwa umeolewa au umeoa.

Chet cha shule unapewa kuonesha identification na pia qualification fulani ulizopata kutokana na uwezo uliouonesha.


Kwa hiyo mantik ya chet cha shule na chet cha ndoa huwa ni tofauti....
 
salama mpendwa. mzima wewe?

Wewe cheti chako cha ndoa tukupe baada ya sijui iether ukiwa ajuza? Au pale kifo kitakapo kuachanisha? Au devorce??? Ha haa i joke....

Lin tukupe chet?
 
Wewe cheti chako cha ndoa tukupe baada ya sijui iether ukiwa ajuza? Au pale kifo kitakapo kuachanisha? Au devorce??? Ha haa i joke....

Lin tukupe chet?

hahaaa nataka siku ya tukio lenyewe la kufunga ndoa maana cheti ni uhalali wa kumiliki
 
siku hizi uchumba hautumiki kama inavotakiwa siku hizi watu wako mbali mbali wanapanga kuoana wanajiita wachumba tayari sasa sijui huo muda wa kuchunguzana wanaupata wapi
The intelligent
 
Chet cha ndoa unapewa ili kukuidentfy kuwa umeolewa au umeoa.

Chet cha shule unapewa kuonesha identification na pia qualification fulani ulizopata kutokana na uwezo uliouonesha.


Kwa hiyo mantik ya chet cha shule na chet cha ndoa huwa ni tofauti....

kwanini kisirudishwe baada ya ndoa kuvunjika ili ku-identify kuwa sasa haupo katika ndoa
 
Cheti cha ndoa ni kama hati ya kiwanja/nyumba, tofauti ni kwamba unaanza kupoteza ndoa ndo cheti kinakuwa hakina maana.na unaanza kupoteza hati ndo nyumba inakuwa sio yako.
 
Hujaelewa wewe uckurupuke! meaning ya chet cha ndoa, ni pongezi ya kujisitiri na kuvumiliana mpaka kuushinda mtihan bila kuvuliana chup zenu, na ndio maana kuna amri usizin ila watu ni vichwa maji, pia mkishapata chet ndio mnaenda kutenda na kutekeleza maagizo ya ndoa, sasa, vivo hvo kwenye masomo unasoma unafaulu nakupata chet then unaenda kukitendea haki yake kwa kutekeleza.
 
Back
Top Bottom