Maajabu ya Korea Kaskazini

Maajabu ya Korea Kaskazini

Hakuna anayependa kuishi kwa mashaka
"Korea kaskazini - ndio nchi inayoongoza kwa mabalozi wake wakistaafu kutorudi nchini humo yaani hutorokea hukohuko"

In God we Trust
 
Hao raia wakichoka ipo siku kitanuka hiyo familia inayoongoza kimabavu hatima yake itakuwa ya haja kwelikweli.
 
Propaganda nyingi hapa, kiufupi kwenye developing country hasa za afrika hakuna nchi yoyote inayoifikia korea kaskazini.
Nitakuja na facts na ushahidi kesho.

Asilimia zaidi ya 25 ya defectors waliokimbilia korea kusini wanataka kurudi kwao. Ni kweli kuwa korea kaskazini ni maskini kiasi kinchosemwa hapa?

North korea wana operating system yao wenyewe inaitwa RED STAR OS(Latest release: 4.0 )hawatumii windows hawa.
nitarudi.

red-star-os-590x330.jpg

RED STAR OS
 
Kama ulikua huijui vizuri Korea Kaskazi ngoja nikueleze;-
Sheria za Korea Kaskazini:-
Korea kaskazini - ndio nchi pekee duniani ambayo raia wake hawaruhusiwi kuwa na dini yaani hakuna waislamu wala wakristo marufuku,
Korea kaskazini - ndio nchi pekee duniani ambayo vitabu vitakatifu vya dini haviruhusiwi kuingia nchini humo,
Korea kaskazini - Rais anaheshimika kama mungu,
Korea kaskazini - kuvaa Vimini marufuku,
Korea kaskazini - Rais akiongea ukisinzia unapigwa risasi, mwaka juzi waziri wa ulinzi alipigwa risasi hadharani kwa kosa la kusinzia kwenye kikao wakati rais akiongea,
Korea kaskazini - ndio nchi pekee duniani iliowahi kuiteka Nyambizi ya marekani,
Korea kaskazini - Adhabu ya kifo ni adhabu ya kawaida mno,
Korea kaskazini - ni familia moja tu ndio inayoongoza nchi,
Korea kaskazini - hakuna vyama vingi,
Korea kaskazini - hakuna uchaguzi wa rais hurithishana,
Korea kaskazini - kuna style 18 tu za kunyoa nywele na kila raia anatakiwa anyoe style hizo,
Korea kaskazini - kunyoa kiduku ni style anayo nyoa Rais tu,
Korea kaskazini - ndio nchi inayoongoza kwakuwa na mabalozi wachache duniani,
Korea kaskazini - ndio nchi inayoongoza kwa raia wake kutoroka nchi,
Korea kaskazini - haina ubalozi tanzania ,
Korea kaskazini - raia hawaruhusiwi kuangalia movies za nje ya nchi,
Korea kaskazini - raia hawaruhusiwi kuangalia taarifa za habari za nje,
Korea kaskazini - ndio nchi pekee duniani ambayo rais wake hajawahi kufanya ziara Africa,
Korea kaskazini - ndio nchi pekee duniani ambayo hauruhusu mtu kuomba uraia,
Korea kaskazi - ndio nchi pekee duniani ambayo raia wake hawaruhusiwi kutoka nje ya nchi isipokuwa kwa kazi maalum ya kiserikali,
Korea kaskazini - hutumia kalenda ya peke yao, yaani kwao kwasasa ni mwaka 105, huanza kuhesabu mwaka aliozaliwa babu yake rais wa sasa Kim john Un,
Korea kaskazini - kuvaa jinzi marufuku,
Korea kaskazini - Bangi ruksa kuvuta,kulima na kuuza,
Korea kaskazini - ni marufuku kuongea kiingereza ukigundulika unaongea unanyongwa,
Korea kaskazini - ndio nchi inayoongoza kwa mabalozi wake wakistaafu kutorudi nchini humo yaani hutorokea hukohuko,
Korea kaskazini - raia wa korea kusini haruhusiwi kabisa kuingia korea kaskazini, ila raia wa korea kaskazini anaruhusiwa kuingia korea kusini bila viza,
Korea kaskazini - ndio nchi yenye rais mdogo zaidi duniani,
Korea kaskazini - rafiki yake mkubwa ni china,
Korea kaskazini - hakuna mitandao ya kijamii yaani hakuna Fb,twitter na mingine,

Hiyo ndio korea kaskazini.

Hapo kwenye lugha ya kiingereza naona tunge iga kabisa maana mmmmmmView attachment 1417518

In God we Trust
Kuna nyingine umetudanganya

1: Nchi pekee ambayo raia wa kigeni haruhusiwi kupewa uraia

Hii sio kweli, nenda China au India ukaombe uraia kama utapata.


2: Nchi ambayo raia wake wanaongoza kwa kukimbia nchi.

Sina data kamili lakini sidhani kama wanazizidi Eritrea,Ethiopia na Somalia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unasema huna uhakika!
Kuna nyingine umetudanganya

1: Nchi pekee ambayo raia wa kigeni haruhusiwi kupewa uraia

Hii sio kweli, nenda China au India ukaombe uraia kama utapata.


2: Nchi ambayo raia wake wanaongoza kwa kukimbia nchi.

Sina data kamili lakini sidhani kama wanazizidi Eritrea,Ethiopia na Somalia

Sent using Jamii Forums mobile app

In God we Trust
 
Back
Top Bottom