Maajabu ya Kijiji cha Myamba, Same Mkoani Kilimanjaro

Maajabu ya Kijiji cha Myamba, Same Mkoani Kilimanjaro

Hivi punde

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2017
Posts
2,554
Reaction score
8,606
Ni Kijiji chenye kabila la Wapare na dini ya Kisabato. Kipo juu sana kwenye milima ya Upareni yenye msitu mkubwa wa Shengena.

1. Kuanzia Ijumaa saa 10 hadi Jumapili huwezi kupata huduma muhimu za kijamii mfano usafiri wa basi, hiace au Costa.

Maduka yote hufungwa. Huwezi kupata huduma hata ya kununua mswaki au Wakala wa pesa.

Ni muda ambao watu hawafanyi kazi kabisa, hata kama ni kazi ya hela nyingi.

Wanaume wana wivu kupindukia juu ya wanawake, hata kama siyo mke wake, siyo mwanae, siyo ndugu yake. Wivu fulani wa ajabu sana.

Wananchi wakikuitikia Ndiyo, ni ya mdomoni tu, moyoni mwao ni hapana na wako na confidence ya kukukana live mbele hata ya kiongozi. Hata kiongozi mkubwa kugeukwa ni dakika sifuri.

Ni wakulima wazuri sana wa Tangawizi inayolimwe kwenye miteremko mikali sana.
 
Mkuu ukishapita kimasihara eneo hilo nini?

Hebu tupia kapicha ka kijijini hapo basi tuone hizo pisi za kuonewa wivu kupindukia.
 
Ila hao mambo ya uwizi, zinaa , utapeli sijui nn mambo ya hovyo kama yote ni mwiko ...Nimekaa nao sana kwa Mbuta na mkomazi Wana misimamo mikali yaani hata sigara hawataki na kambale wale hawali kabisa .

Ni watu waaminifu kwa niliwaona maana bibi yangu ni mpare wa pure wa mazinde ...Yaani na sifa nyingine zile ndio wapo sana yaani hawezi bibi kukubali mkatupa chakula hata siku moja na kile Kijiji Chao kama Kuna msiba basi mfiwa hatoi hata shilling mia atafanyiwa usafi na kila nyumba wanamletea debe la nafaka yaani anaweza kukusanya magunia mengi kama sehemu ya kumfariji.

Kingine kande zinaweza kupikwa ijumaa Tena sio za Nazi ni zile bila ya mahindi sisi tunaita "MAGUGU" zinapikwa nyingi nyingine zinawekwa mpaka kweny chupa ya chai ili zisipoe basi wanaenda mpaka jumapili usiku au j3.

Wana upendo sana kwa hilo.

Kitu lilikuwa kinaniboa ni kimoja yaani tumeenda kweny harusi mwisho wa siku ni kande wameweka maboga wali hawanaga time nao kabisa.
 
Ni Kijiji chenye kabila la Wapare na dini ya Kisabato. Kipo juu sana kwenye milima ya Upareni yenye msitu mkubwa wa Shengena.

1. Kuanzia Ijumaa saa 10 hadi Jumapili huwezi kupata huduma muhimu za kijamii mfano usafiri wa basi, hiace au Costa.

Maduka yote hufungwa. Huwezi kupata huduma hata ya kununua mswaki au Wakala wa pesa.

Ni muda ambao watu hawafanyi kazi kabisa, hata kama ni kazi ya hela nyingi.

Wanaume wana wivu kupindukia juu ya wanawake, hata kama siyo mke wake, siyo mwanae, siyo ndugu yake. Wivu fulani wa ajabu sana.

Wananchi wakikuitikia Ndiyo, ni ya mdomoni tu, moyoni mwao ni hapana na wako na confidence ya kukukana live mbele hata ya kiongozi. Hata kiongozi mkubwa kugeukwa ni dakika sifuri.

Ni wakulima wazuri sana wa Tangawizi inayolimwe kwenye miteremko mikali sana.
Kumbe unaongerea wapale powa
 
Back
Top Bottom