chingunduli
JF-Expert Member
- Feb 23, 2012
- 268
- 51
Katika uchaguzi uliopita wa serikali ya mtaa katika mtaa wa migombani kata ya segerea Matokeo ni kama ifuatavyo CHADEMA nafasi ya mwenyekiti ilipata kura 547 na CCM ilipata kura 215 na NCCR ilipata kura 205. Uchaguzi wa wajumbe haukufanyika kutokana na kasoro mbali mbali katika karatasi za wagombea ujumbe hivyo ukarudiwa tarehe 21 na Matokeo ni kwamba Wajumbe wa chadema walishinda kwa kura 410- hadi 390 huku wale wa ccm wakipata kura 20-60 mara zote za uchaguzi, ccm waligoma kusign karatasi za Matokeo . Mara baada ya kumaliza uchaguzi ameibuka mtoto wa makongoro Maanga na Masaburi wanatangaza kuwa uchaguzi utarudiwa bila sababu yoyote na mkuu wa mkoa katangaza kurudia uchaguzi siku ya hotoba ya jk na wazee wake. Wanaojua sheria tunaomba mtusaidie ni halali kurudia uchaguzi baada ya kutangazwa ushindi kwa muda wa wiki mbili? Ni nani anyeweza kutengua Matokeo kisheria baada kutangazwa kisheria? Nimeambatanisha karatasi za Matokeo yote