Maajabu vifaranga viwili ndani ya yai

Maajabu vifaranga viwili ndani ya yai

Pawaga

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2011
Posts
1,349
Reaction score
1,011
Habari ya majukumu,

Jamani mimi ni mfugaji wa kuku wa kienyeji toka mwaka 2011 na sasa nina zaidi ya kuku 700. Tatizo langu ni kuwa mwanzoni mwa mwezi huu niliatamisha kuku 18 ambao jana wametotoa vifaranga lakini nimeshangaa hawa KUKU WAMETOA VIFARANGA VIWILI VIWILI KWA KILA YAI na leo hii wale kuku wazazi wote wanaumwa wengne washakufa lakini vifaranga wote ni wazima na nimewaweka kwenye banda la kulelea vifaranga.

Je, hili ni tatizo gani na nini suluhisho lake?
 
Ni jambo la kawaida.
Nyumban kwetu kuna kuku wa kienyeji hutaga mayai 10 had 12 na kat ya hayo yenye mapacha huwa 3 had 4.
Kizaz chake kimekuwako tangu niko mdgo had sasa
Duhhh... kwenu wap mkuu
 
hilo la mapacha ni kawaida, ila kwa hao mama kuku kufa ndio pana tatizo. Yawezekana wakati wa kutamia hukuwawekea chakula chenye virutubisho vya kutosha hali iliyosababisha kupoteza nguvu na kinga mwilini, hiyo yaweza kuwa hasa sababu ya hao kuku wazazi kufa.
 
Hao kuku umewatamishia mara ngapi? Nauliza km umewaatamishia zaidi ya mara moja itakuwa ni njaa. Kuna kuku niliwaatamishia mara mbili mmoja alitoka hoi hata kusimama shida. Nikanunua glucose nijampa kwenye uji mwepesi baada ya masaa kadhaa akala chakula chake cha kawaida
 
kuku 700 hizo sifa,ungeuliza kuhusu pacha tu
Genda Heka Linapita.......
 
Habar ya majukum?,jaman mi ni mfugaj wa kuku wa kienyeji toka mwaka 2011 na sasa nina zaid ya kuku 700. Tatizo langu ni kuwa:mwanzon mwa mwez huu nliatamisha kuku 18 ambao jana wametotoa vifaranga lakin nimeshangaa hawa KUKU WAMETOA VIFARANGA VIWILI VIWILI KWA KILA YAI na leo hii wale kuku wazaz wote wanaumwa wengne washakufa lakin vifanga wote ni wazima na nimewaweka kwny banda la kulelea vfaranga,je hli ni tatizo gan na nin suluhisho lake?
Mkuu hao kuku wote 700 unawalisha chAkula gan hiki cha madukani au pumbA za kawaida
 
nawalisha chakula cha kawaida tu yaan pumba na mabaki ya vyakula tunavyokula sisi pia wanajitafutia maana natumia nusu huria kuwafuga
 
Habar ya majukum?,jaman mi ni mfugaj wa kuku wa kienyeji toka mwaka 2011 na sasa nina zaid ya kuku 700. Tatizo langu ni kuwa:mwanzon mwa mwez huu nliatamisha kuku 18 ambao jana wametotoa vifaranga lakin nimeshangaa hawa KUKU WAMETOA VIFARANGA VIWILI VIWILI KWA KILA YAI na leo hii wale kuku wazaz wote wanaumwa wengne washakufa lakin vifanga wote ni wazima na nimewaweka kwny banda la kulelea vfaranga,je hli ni tatizo gan na nin suluhisho lake?
Salama Mkuu tuwasiliane 0763370175
 
Back
Top Bottom