OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,186
- 103,702
Zile mamlaka zinazotathmini maaajabu ya dunia wanatakiwa kuchukua hili kama ni moja la ajabu duniani. Sio lazima liwe kati ya maajabu nane ila liwe tu hata ajabu la 98.
Scenario 1
Mtu anaamini Mh.Freeman Mbowe sio gaidi wala hana kosa. Anaamini anatakiwa kuwa huru kwa hali na mali. Anaamini waliomfunga wanamuonea kwa sababu za kisiasa.
Ajabu ni kwamba mtu huyu anatutaka siye tumbembeleze aliyemfunga Mbowe ili amuachie huru. Anatulaumu kwa nini tunachochea Mbowe akaze hakuna kuomba msamaha? 😥😥😥
Nasema anaamini Mbowe sio gaidi kwa sababu kama ni gaidi kweli kweli kwa nini anataka tumuombee Mbowe msamaha? Kama Mbowe ni gaidi si inabidi apigwe mvua za kutosha? Magaidi mfano wa Osama Bin Laden au Mullah Omar huwa wanatakiwa wawe Guantanamo Bay wasije wakalipua mabomu.
Kama unaamini Mbowe ni gaidi lakini unataka aombewe msahama, basi inabidi upimwe akili. Gaidi linaachiwa kwa kuombewa msahama? Yaani Gaidi la Alshaab likamatwe halafu Wasomali waanze kupaza sauti kuliombea msahama,wakati linataka kuwaua? Utakataa tukikupima akili?
Ajabu ni kwamba inashangaza mtu huyu badala ya kumlaumu yule aliyemfunga Mbowe kwa hila,analaumu wanaomlaumu aliyemfunga Mbowe.
Scenario 2
Lawama hizi kwetu zimechochewa na hukumu ndogo ya jana kwamba Mbowe ana kesi la kujibu. Wanasema makelele yetu yamemfanya jaji akaze.
Kwa hiyo mtu huyu anaamini kabisa ule ushahidi wa upande wa mashtaka hauna vigezo vya kumkuta mtu na kesi la kujibu.
Ajabu ni kwamba mtu huyu anatulaumu siye kwa nini hatuwi wapole yaishe ili Jaji alegeze?
Ajabu ni kwamba mtu huyu ameacha kumlaumu Jaji anayeaminisha watu juu ya ushahidi wa uongo anatulaumu siye tunayemlaumu Jaji,kama yeye.
Nasema mtu huyu anaamini hakuna ushahidi wa kumkuta Mbowe na kesi la kujibu kwa sababu kama Mbowe ana kesi kwa nini utulaumu siye? Kwa nini usione gaidi kakutwa na kesi ya kujibu?
Niwashauri waTz wenzangu lengeni mzizi wa tatizo sio kupaparika na watu wasiostahiki lawama. Hali hii inaonyesha unyonge wa kuzidi kipimo na tunaonekana taifa la hovyo kuliko mfano.
Kama sio taifa la watu wa hovyo, kwa nini umlaumu mtu anayekataa kulamba viatu au makalio?! Mtu huyu anatakiwa kupongezwa na kuungwa mkono
Scenario 1
Mtu anaamini Mh.Freeman Mbowe sio gaidi wala hana kosa. Anaamini anatakiwa kuwa huru kwa hali na mali. Anaamini waliomfunga wanamuonea kwa sababu za kisiasa.
Ajabu ni kwamba mtu huyu anatutaka siye tumbembeleze aliyemfunga Mbowe ili amuachie huru. Anatulaumu kwa nini tunachochea Mbowe akaze hakuna kuomba msamaha? 😥😥😥
Nasema anaamini Mbowe sio gaidi kwa sababu kama ni gaidi kweli kweli kwa nini anataka tumuombee Mbowe msamaha? Kama Mbowe ni gaidi si inabidi apigwe mvua za kutosha? Magaidi mfano wa Osama Bin Laden au Mullah Omar huwa wanatakiwa wawe Guantanamo Bay wasije wakalipua mabomu.
Kama unaamini Mbowe ni gaidi lakini unataka aombewe msahama, basi inabidi upimwe akili. Gaidi linaachiwa kwa kuombewa msahama? Yaani Gaidi la Alshaab likamatwe halafu Wasomali waanze kupaza sauti kuliombea msahama,wakati linataka kuwaua? Utakataa tukikupima akili?
Ajabu ni kwamba inashangaza mtu huyu badala ya kumlaumu yule aliyemfunga Mbowe kwa hila,analaumu wanaomlaumu aliyemfunga Mbowe.
Scenario 2
Lawama hizi kwetu zimechochewa na hukumu ndogo ya jana kwamba Mbowe ana kesi la kujibu. Wanasema makelele yetu yamemfanya jaji akaze.
Kwa hiyo mtu huyu anaamini kabisa ule ushahidi wa upande wa mashtaka hauna vigezo vya kumkuta mtu na kesi la kujibu.
Ajabu ni kwamba mtu huyu anatulaumu siye kwa nini hatuwi wapole yaishe ili Jaji alegeze?
Ajabu ni kwamba mtu huyu ameacha kumlaumu Jaji anayeaminisha watu juu ya ushahidi wa uongo anatulaumu siye tunayemlaumu Jaji,kama yeye.
Nasema mtu huyu anaamini hakuna ushahidi wa kumkuta Mbowe na kesi la kujibu kwa sababu kama Mbowe ana kesi kwa nini utulaumu siye? Kwa nini usione gaidi kakutwa na kesi ya kujibu?
Niwashauri waTz wenzangu lengeni mzizi wa tatizo sio kupaparika na watu wasiostahiki lawama. Hali hii inaonyesha unyonge wa kuzidi kipimo na tunaonekana taifa la hovyo kuliko mfano.
Kama sio taifa la watu wa hovyo, kwa nini umlaumu mtu anayekataa kulamba viatu au makalio?! Mtu huyu anatakiwa kupongezwa na kuungwa mkono