Maadui watatu wa Mwanadamu

Maadui watatu wa Mwanadamu

Kizoku

Senior Member
Joined
Apr 30, 2014
Posts
186
Reaction score
66
Katika dunia ya leo, ili uishi maisha ya amani inabidi upambane na maadui watatu.

1. Nyumba ya kupanga. Huyu ndio adui namba moja. Bora hata uishi kwenye dungu la tope la kwako mwenyewe kuliko kero za kuishi nyumba ya kupanga.

2. Kutumia usafiri wa umma. Hii ya kila siku kunukishana vikwapa kwenye daladala na kero nyingine za vyombo vya usafiri wa umma ni adui namba mbili.

3. Kuajiriwa. Baada ya kero za mwenye nyumba, kero ya usafiri wa umma mwishowe ni hii kero yakuajiriwa. Hasa unapokuta IQ yako kubwa halafu wanaokuongoza wana IQ ndogo. Ndio shida inapoongezeka.

Siku zote tupambane kuwatokomeza maadui hawa watatu.
 
Hapo #3 kwenye kuajiriwa watakuelewa wachache sana na ndo watakaokubaliana na ww, me mekuelewa vizuri.
 
  • Thanks
Reactions: amu
Moja na mbili nimevuka Alhamdulillah hapo kwenye 3 ndio majanga..
 
kuna mtu mmoja niliwahi kumsikia akisema eti maadui watatu wa Mtanzania ni umaskini, shetani na ccm
 
Afadhali huyo wakatikati kuna wakati hupuuza mambo ila huyo wa mwisho, mtumeeeeee meno yangu na kucha zangu!!!!!!!! wacha nipite mie.
Mmmh !! basi tumrudishe MKOLONI..... tutaponyesha meno na kucha !! kawoli Uliwahi ishi enzi za mkoloni?????!!
 
Last edited by a moderator:
Wewe ndo hujui kabisa mleta mada.Adui namba 1 ni ccm.
 
mh we nawe IQ yako bado ni ndogo hizo sababu ulizozitaja zote wala sio maadui ktk maisha bali ni changamoto tu za maisha tu, maadui wakuu ni Ugonjwa, Umasikini, na ukosefu wa elimu. na ukitaka nikudadavulie naweza,
 
sikuwahi, lakini kwa masimulizi ya babu na bibi hawakuwa wabaya kiasi hiki.
 
Katika dunia ya leo, ili uishi maisha ya amani inabidi upambane na maadui watatu.
1. Nyumba ya kupanga. Huyu ndio adui namba moja. Bora hata uishi kwenye dungu la tope la kwako mwenyewe kuliko kero za kuishi nyumba ya kupanga.
2. Kutumia usafiri wa umma. Hii ya kila siku kunukishana vikwapa kwenye daladala na kero nyingine za vyombo vya usafiri wa umma ni adui namba mbili.
3. Kuajiriwa. Baada ya kero za mwenye nyumba, kero ya usafiri wa umma mwishowe ni hii kero yakuajiriwa. Hasa unapokuta IQ yako kubwa halafu wanaokuongoza wana IQ ndogo. Ndio shida inapoongezeka.
Siku zote tupambane kuwatokomeza maadui hawa watatu.

Namba 1 wahindi mpaka leo wanakaa kwenye nyumba za shirika la nyumba ni wachache waliojenga.
Namba 2 usafiri wa kwa nchi za wenzetu ndio usafiru mzuri kuliko hata wa binafsi.
Namba 3....loading erro
 
Katika dunia ya leo, ili uishi maisha ya amani inabidi upambane na maadui watatu.
1. Nyumba ya kupanga. Huyu ndio adui namba moja. Bora hata uishi kwenye dungu la tope la kwako mwenyewe kuliko kero za kuishi nyumba ya kupanga.
2. Kutumia usafiri wa umma. Hii ya kila siku kunukishana vikwapa kwenye daladala na kero nyingine za vyombo vya usafiri wa umma ni adui namba mbili.
3. Kuajiriwa. Baada ya kero za mwenye nyumba, kero ya usafiri wa umma mwishowe ni hii kero yakuajiriwa. Hasa unapokuta IQ yako kubwa halafu wanaokuongoza wana IQ ndogo. Ndio shida inapoongezeka.
Siku zote tupambane kuwatokomeza maadui hawa watatu.

Mkuu,
1. Unamaanisha nyumba ya kupanga au makazi?
2. Kutumia usafiri wote wa umma?
3. Kuajiriwa au Kutegemea kipato cha kuajiriwa?

Unaposema maadui watatu wa Mwanadamu, unamaanisha "maadui" watayu wa mtanzania au, kwasababu si wanadamu wote wenye kuishi katika nyumba za kupanfa lakini huishi katika maisha mazuri! Na wapo waishio katika nyumba zao lakini ni bora wangepanga.
Kuna nchi ambazo ni gharama sana kujenga! Nchi ambazo kwa watu wanaoishi mijini kupata eneo!

Pili, kuna watu waishio katika maeneo ya mbali ambapo ni usafiri wa umma mf. treni, mabasi ndiyo pekee suluhisho. Sasa unaposema hili nalo ni adui, iweje kwa mtu akaaye km 50+ ambaye hawezi kutumia usafiri wake wa binafsi ingawa anao?

Tatu, issue sidhani kama ni kuajiriwa..nadhani kutegemea kipato kimoja cha kile ulichoajiriwa ndiyo shida! Kwa dunia ya sasa, si rahisi (ingawa inawezekana) kutegemea kipato kimoja unless kuwe na rushwa au wizi. Lakini, je ni wote wataweza kujiajiri?

So, binafsi sioni kama hawa ni maadui wa 'mwanadamu', unless tujue mwanadamu huyu yuko katika mazingira yapi/gani! I stand to be corrected.
 
mh we nawe IQ yako bado ni ndogo hizo sababu ulizozitaja zote wala sio maadui ktk maisha bali ni changamoto tu za maisha tu, maadui wakuu ni Ugonjwa, Umasikini, na ukosefu wa elimu. na ukitaka nikudadavulie naweza,

Hizo za Umaskini,maradhi ni propaganda za kisiasa tulizokuwa tunakaririshwa miaka ileee. Ila ya tatu ilikuwa ujinga sio ukosefu wa elimu. Ingekuwa kuwa na elimu dili Tanzania tungekuwa ulimwengu wa kwanza.
 
Hakuna kitu cha hatari kama familia yako iongozwe na mtu mwenye elimu kubwa lakini IQ zero na weledi chini ya sifuri.
 
mh we nawe IQ yako bado ni ndogo hizo sababu ulizozitaja zote wala sio maadui ktk maisha bali ni changamoto tu za maisha tu, maadui wakuu ni Ugonjwa, Umasikini, na ukosefu wa elimu. na ukitaka nikudadavulie naweza,

embu mueleze bana kupanga mbona hakuna tabu. kawaida tu inategeme na ni wapi umepanga ukiwa uswahilini swahilini sana ndo kuna kuwa tabu. sasababu zako hazina mshiko sana.
 
Back
Top Bottom