Ma uza uza ya Fedha

Ma uza uza ya Fedha

666 chata

JF-Expert Member
Joined
Mar 14, 2013
Posts
1,710
Reaction score
4,044
Yawezekana Historia yake ya jinsi mfumo huu wa kutumia fedha ikawa ni ndefu sana na isio na u lazima sanaa kuijua, ila kwa hakika ni lazima tukubaliane tu kua watu waliobuni na kuuleta mfumo huu tangu karne na karne hawakua binadamu wa kawaida tu.

Fedha au Pesa imekua na sifa zisizo tambuliwa kwa ufasaha na wanadamu wenyewe, mfano mtu mwenye uoga nayo na akajiathiri hadi kisaikolojia basi hua bahili balaa yaani akipata elf 10 ni atakula tu mandazi,maji na kujibana bana wee ili isiishe, na watu wa aina hii wachunguze uone, fedha ni tatizo lao kubwa, inawanyima amani. Au yule aliewai kuzipata nyingi baadae akaja kufilisika kabisa mpaka chini asilimia 98 watu wa hivi hua hawapati tena pesa, ata wafanye nini, yaani na pesa zinaona kama hawa labda wameua ndugu yao pesa mwingine.

Wakati mwingine pesa uonekana kama ni uchawi au majini hivi, mfano kama umewahi kuishi maeneo ya karibu na migodi ya wachimbaji wadogo wadogo utaelewa hapa, binafsi nimewai kukaa geita, nlijionea haya, unakuta kakijana tu kamepata milion 20 jumatatu leo ijumaa hakana ata senti tano, na wanaambiana kabisa mzee hizi hela za majini tukizipata tu ziishe, na ndicho kinachotokea, na hapa mie nna ushaidi mwingi toka huko geita, nlijionea mwenyewe haya, mpaka unaanza kujiuliza hawa watu vp wamerogwa au?

Mtu anaezimiliki nyingi kwenye akaunti kiu ya kutaka kuzitafta zaidi uzidi maradufu, na wengine uvuka mipaka na kuua kabisa, mfano pale Mwanza kuna mmiliki wa mabus ya j4 aliwaua vijana wawili ambao walikua wamemtapeli milion moja au mbili hivi, na hili linajulikana mkoa mzima hata magazeti yali report sana hii, sasa unaweza jiuliza jamani hawa watu vp, fedha zote hizo wewe Mo si umrudie Mungu wako na uanze kula pepo duniani na masafari tu ya kila namna all over the world? forbes ya nini labda?

Ukipiga hesabu kwa mtu alie na bilion moja benki basi ana uwezo wa kua anaenda kutoa milion moja kila mwisho wa mwezi kwa muda wa miaka 82, sasa njoo tuangalie wangapi wanalipwa milion moja kwa mwesi hapa nchini? vp sasa chenge aliekutwa na bilion 22 na akaita vijisenti na bado kila madili tunaskia yumo? wazee hela is something else sivyo tunavyoiwaza, kwa taarifa yako tu vijisenti hivi vya chenge kama mtu akiamua kua kila siku awe anatumia milion moja moja kwa siku itamlazimu kutumia kwa muda wa miaka sita mfululizo kila siku mzee unatumia milion moja, hahahaha ila mbona hawa hawaridhiki kila siku wanazisaka tu, wanashida gani hawa?

Ukiwa nazo hauwi na akili hizo na usipokua nazo hauwi na akili hizo pia

Report ya Legal and Human Right Center ya miaka kama mitatu iliyopita ilichapisha utafiti wake kuhusu haya mambo ya mauaji na ilionesha kua kanda ya ziwa kuna wauaji walilipwa hadi laki mbili na elfu 50 kwa ajili watekeleze mauaji na walitekeleza kweli, jiulize sasa laki mbili ni fedha gani nayo? usihukum hold on mbona nyie mtaani kwenu mliua kibaka alieiba pochi yenye elf tano ndani?

Anyway ni stori za hapa na pale tu, ila ndugu kua na nidhamu na icho kinachoitwa fedha, kumbuka na UTU pia.

Kama Plato alivyokwisha sema kua "Yewezekana tukawa tunaishi katika dunia tusioifahamu na siku tukiambiwa iko hivi na sio ivyo sisi tutabisha sanaa".
 
Pesa mwna haram
Pesa ndio chanzo cha machafu yote hakuna dhambi unashindwa ifanya aliye na pesa
Money is a power
Ukitaka kujua tabia ya mtu subiri awe na pesa
Iache iitwe pesa
Ila mkuu Kuna usemi mmoja usemao tajiri bahili Hana tofaut na masikini nawasilisha
 
Watu wengine wakipata pesa wanaitumia wee ikiisha anajutia hivi nilitumiaje hii hela mbona imekata fasta??
 
Watu wengine wakipata pesa wanaitumia wee ikiisha anajutia hivi nilitumiaje hii hela mbona imekata fasta??

Ndo maana nkasema yawezekana bado hatuitambui vizuri fedha, yaan tukawa kila saa tunajiona sisi wanadamu ndio wenye matatizo nazo ila sio zenyewe, yaani haya mambo nafikiri yapo ki roho sanaa
 
Pesa mwna haram
Pesa ndio chanzo cha machafu yote hakuna dhambi unashindwa ifanya aliye na pesa
Money is a power
Ukitaka kujua tabia ya mtu subiri awe na pesa
Iache iitwe pesa
Ila mkuu Kuna usemi mmoja usemao tajiri bahili Hana tofaut na masikini nawasilisha


Mkuu kuna wale matajiri wamezipata kwa njia ya ushirikina, asee hawa bora ata na maskini wakutupwa, wame archieve vyote af hawana furaha wala amani.
 
kweli mkuu
Ndo maana nkasema yawezekana bado hatuitambui vizuri fedha, yaan tukawa kila saa tunajiona sisi wanadamu ndio wenye matatizo nazo ila sio zenyewe, yaani haya mambo nafikiri yapo ki roho sanaa
 
Nilivyokua na umri mdogo niliwah kufikiria kwamba ukiwa na pesa lets say 10 ml matatizo yte yanakwisha,,na mbaya zaid nilizid kuamin kwamba ili binadamu uwe tajiri sana lazima uwe na pesa nying sana,na nilipotea zaid kwa kuamin na kuiwaza hela asubuh,mchana,jion na usiku, aseeh nilipotea sana kama sio mama mmoja aliefanikiwa kuniondolea utumwa akilin,,aliniambia ukiwaza pesa muda wote hakika kuna muda utajichukia na hutarudhika kwa chochote,na kama unadhan pesa nying inaweza kukupa furaha bas umefel sana ktk ubongo wako,na akanisisitizia kwamba ukijua kuitafuta sana bas ujue nankuitumia sna,na mwsho akanisisitizia kwamba hakuna muda maalum wa kupata pesa ikiwa tu una uhai na afya bora,bila kusahau pia hakuna muda ambao utafirah maishan kama utaweka hela ndio kila kitu,muda wa kufurah ni kipind hcho hcho ambacho unazisaka lazma utenge muda wa kuyafurahia maisha,,bila kuogopa kwamba nasubiri zijae maana kikanuni hua haizitoshi kila siku... Nam nikabadilika sa hzi nakula maisha bila stress nying za mambo ya hela japo nazisaka vizur tu bila bugudha
 
Back
Top Bottom