Ma-celeb wanaumia wanapoachwa?

Ma-celeb wanaumia wanapoachwa?

Viol

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2009
Posts
25,419
Reaction score
18,341
Wakuu,

Hawa watu wanakutana na warembo au wanaume wenye pesa kila sekunde, hivi kuna celebrity ashaumia seriously?

Messi, Ronaldo, Nicki Minaj, Lil Wayne, wanasiasa, Billgate, Dangote, Mengi, Wema Sepetu, hivi hawa wanafeel pain kweli maana mda wote wanatafutwa.

Au sisi wa kawaida ndo tunaumizwa na mapenzi?
 
Hisia za mapenzi ni kwa mwanadamu. Pesa na vinginevyo vinaweza kujenga hisia kwa muda, ila real love hubaki pale pale...
Mapenzi yanaumiza aisee....!
Kuna vitu huwezi kuvinunua kwa pesa au status yako.....!

Adim saana mkuu Viol
 
Valentina acha hizo ukiwa celeb kuna wakumpenda?kama ni mwanaume marafiki zako wanakuwa kina Nicki minaj,Kim kardishian,amberose,j-lo,Beyonce,sasa hao walivyo wazuri si unafall in love mda wowote
 
Ndiyo wanaumia kama binadamu wengine,kila mtu ana mtu wake anayempenda ndiyo maana unaweza kuona mwanamke anakuchuna pesa halafu anamplekea hamisi muuza madafu.
 
Mapenzi ni kimbilio la starehe kwa wasio na feza,ila sisi wenye feza chafu tuna option nyingi za starehe siyo lazima mapenzi!
Nye wenye hela chafu mkutendwa mnaumia au mnapoachwa mnaumia?
 
Valentina acha hizo ukiwa celeb kuna wakumpenda?kama ni mwanaume marafiki zako wanakuwa kina Nicki minaj,Kim kardishian,amberose,j-lo,Beyonce,sasa hao walivyo wazuri si unafall in love mda wowote
Hata uzungukwe na wazuri wote kuna mmoja tu utadondokea kwake.... Na kampani yake utaihitaji zaidi ya wengine
 
Ndio kisa cha Usher Raymond kutoa Album ya confession 2003-2004.

Au juma nature Ugali
 
Nye wenye hela chafu mkutendwa mnaumia au mnapoachwa mnaumia?
Sisi wenye feza chafu huwa hatuna mpenzi mmoja mkuu,kwa mfano mimi nina wapenzi 19 kati yao watano wanatokea JF na hawajuani kwa hiyo akinitenda mmoja haina shida kabisa ni sawa na nzi mmoja afariki kwenye hii dunia!
 
Kuumizwa kupo tu na wala hakuepukiki. Mapenzi hayana umaarufu Mkuu.
 
Wanaumia tena zaidi ya watu wakawaida, zile show off wanazozifanyaga ndio zinakuja kuwa mwiba kwao,
 
Back
Top Bottom