M-pesa na tigo-pesa kunani?

M-pesa na tigo-pesa kunani?

Igangilonga

Senior Member
Joined
Mar 11, 2006
Posts
133
Reaction score
27
Mara kadhaa nimekuwa nikitaka kutumia huduma aidha ya m-pesa au tigo-pesa nashindwa kufanikiwa au inachukua muda sana, ukiwauliza wahusika wanasema 'mtandao upo down'..... hivi sababu ya mitandao hiyo kuwa down most of the times ni nini? Naombeni maelekezo wajuzi wa jambo hilo becoz I am in dilemma na naathirika sn becoz mimi ni mtumiaji mzuri sn wa huduma hizi.
 
Kwa kweli hii nchi si jui inakwenda wapi, mitandao ya simu inafanya biashara za pesa,je ni halali au kwenye mikataba (ambayo najua viongozi wanasaini tu bila kusoma) ya kuendesha hizi biashara imo hii ya kuendesha biashara ya pesa??
 
Niliwahi soma kuwa vodacom na airtel waluiomba leseni mpya toka bot kuendesha biashara ya pesa na sio tanzania pekee ni dunia nzima makampuni simu yanafanya hivyo inasaidia sana hasa vijijini banks hazijafika ila mpesa zappesa tigipesa zimefika....freddywm fanya utafiti zaidi utajua faida ya hiyo huduma
 
Kwa kweli hii nchi si jui inakwenda wapi, mitandao ya simu inafanya biashara za pesa,je ni halali au kwenye mikataba (ambayo najua viongozi wanasaini tu bila kusoma) ya kuendesha hizi biashara imo hii ya kuendesha biashara ya pesa??
Achana na urasimu.Tunachotaka ni huduma za haraka kupeleka na kupokea pesa hata bila mikataba.Tunataka ikiwezekana baadae watengeze simu zenye printer kabisa ya kutoa pesa ambazo zitakuwa halali kwa vile zitakuwa na nembo za tigo pesa m-pesa na hata ikiitwa freddywm-pesa tutatumia ilimradi benki kuu wamesharidhia.
Vipi wewe unataka kuturudisha enzi za zamani.
 
Me nshajitoa ktk hizo huduma mbofumbofu, hakuna cha mpesa ,tigopesa wala zappesa ni wizi mtu. Iweje pesa uitume leo afu imfikie mlengwa baada ya siku 3 na zaidi imekuwa utazan safari ya dar mpaka mwanza kwa treni. Kwel mshika mawili moja humponyoka mara mawasiliano mara pesa wapi na wapi.
 
Niliwahi soma kuwa vodacom na airtel waluiomba leseni mpya toka bot kuendesha biashara ya pesa na sio tanzania pekee ni dunia nzima makampuni simu yanafanya hivyo inasaidia sana hasa vijijini banks hazijafika ila mpesa zappesa tigipesa zimefika....freddywm fanya utafiti zaidi utajua faida ya hiyo huduma

Hatukatai ni huduma nzuri inayopunguza mafoleni ktk mabenki etc but ziwe za uhakika... most of the times zipo down, hapo ndo tunapoboreka watumiaji.... Halafu pia jana nimegundua hawa mawakala hawana elimu nzuri ya huduma hiyo.... rafikiangu alitaka kunitumia elfu 25 akaambiwa ili nipate hiyo hela taslimu chaji yake ni elfu 1 so akalipa elfu 26 (Mwenge), msg ikaja katika cm yangu kuwa nimepokea elfu 25, nikaenda kuchukua kwa wakala mwingine (Tabata), cha kushangaza akanikata tena elfu 1, ikabidi nipige cm tigo kuuliza kulikoni, nikaambiwa yule wakala wa Mwenge ndie aliekosea alitakiwa apokee elfu 26 na aniingizie elfu 26 then mimi nikienda kuchukua ndo nitapewa elfu 25, hiyo elfu 1 inakatwa automatically.... kwaiyo wakala wa Mwenge alichakachua hiyo elfu 1.......
 
Back
Top Bottom