Ni haki kabisa sasa kumuunganisha na Mtikila wa DP kwa namna wanavyoongoza vyama wanavyomiliki.
Tendwa amestaafu na kuacha historia MBAYA kabisa kwa namna alivyosimamia maadili ya sheria ya usajili wa vyama. Kutwa alikuwa anafukuzana na kusumbuana na CHADEMA bila kuangalia vyama kama hivi ambayo vimekiuka usajili wake kwa muda mrefu.
Mwelewe kwamba ana ganga njaa alisha achana na upinzani ni mwana CCM tu a
Mwenyekiti huyu wa TLP hasomeki vizuri.
Utamsikia mara kwa mara akiwabeza wanasiasa wenzake wa upinzani na kumsifia Mwenyekiti wa CCM. Amefanya hivi mara nyingi tu.
Amekibinafsisha chama cha TLP kuwa chake binafsi kama alivyofanya Mzee Mapesa wa UDP.
Wakati wa uchaguzi mkuu 2010 hakuwa tofauti na Mbatia wa NCCR kwa kutumia muda wao mwingi kujinadi nafasi za Ubunge huku wakimnadi mgombea wa CCM nafasi ya urais. Tabia kama hizi ni za usaliti hivyo hazifai kufanywa na mtu ambaye amepitia mafunzo ya kijeshi kama yeye. Anapaswa sasa kukaa pembeni ili kuruhusu chipuo jipya la wanasiasa wa upinzani wa kweli kuendeleza harakati ambazo yeye anazisaliti kwa sasa.
Mwenyekiti huyu wa TLP hasomeki vizuri.
Utamsikia mara kwa mara akiwabeza wanasiasa wenzake wa upinzani na kumsifia Mwenyekiti wa CCM. Amefanya hivi mara nyingi tu.
Amekibinafsisha chama cha TLP kuwa chake binafsi kama alivyofanya Mzee Mapesa wa UDP.
Wakati wa uchaguzi mkuu 2010 hakuwa tofauti na Mbatia wa NCCR kwa kutumia muda wao mwingi kujinadi nafasi za Ubunge huku wakimnadi mgombea wa CCM nafasi ya urais. Tabia kama hizi ni za usaliti hivyo hazifai kufanywa na mtu ambaye amepitia mafunzo ya kijeshi kama yeye. Anapaswa sasa kukaa pembeni ili kuruhusu chipuo jipya la wanasiasa wa upinzani wa kweli kuendeleza harakati ambazo yeye anazisaliti kwa sasa.