Wadau naomba msaada wa kueleweshwa .Naomba walio serious pekee ambao wanaweza kujadili ndiyo tujadili .Natoa angalizo baada ya JF kuvamiwa na LT badala ta GT .Lower thinkers wameongezeka sana na kuhabaribu mijadili mingi .Lwakatare ametokea kuhubiri Mbezi sijui Mikocheni .Sikuwahi msikia katika harakati za kutetetea ana kupinga lolote .Niliwahi msikia katia biashara tu na hasa mashule na biashara za kanisa lake .Ghafla akawa Mbunge kwa ticket ya CCM kwa kuteuliwa .Sijajua ndugu Rais alitumia kigezo gani japokuwa ni maamuzi yake yeye anaye wateua.Nikaanza kushagaa sasa Siasa na Dini inakuwaje .Ghafla huyu mama amekuwa na tuhuma yingi katika jamii .Kuwadhurumu mishahara watumishi wake , kuiba umeme , na sasa anatajwa katika madawa ya kulevya .Huyu mama bado najiuliza ilikuwaje hadi akawa mbunge na akaamua kuwatumikia ma bwana wa 2 yaani Bunge pesa za walala hoi na Kanisa anakokusanya zaidi pesa za walio kata tamaa?
Ndugu Lunyungu,
Uongozi una mambo mengi. Ukitaka kuwa na mafanikio katika uongozi kuna mbinu nyingi za kufanya, kutegemea na aina ya mafanikio unayotaka. Nitakupa machache:
1.Kama unakusudia kuwa salama na unaogopa challenges utakimbilia kujaza maswahiba wakuzunguke ili wale unaowaogopa wasikukaribie kwa urahisi. Daima utawapa maswahiba kile roho zao zinapenda ili wakutetee hata kama unachemka.
2. Kama unajua kuna jamaa wanaweza kugeuka maadui zako, utajitahidi siku zote wawe rafiki zako. siyo kwa kuwa unajilazimisha kuwapenda ila kwa kuwa inakuwa ni rahisi kuwa monitor.
3.Kama unajua kuna mtu/kundi linakupinga na huna uwezo wa kushinda vita, utakimbilia kuomba muafaka kwa kjiunga nao hata kama mambo yao yanakukereketa ndani. Kwa wajanja hiyo huwa ni nafasi ya kujipanga na kufanya shambulizi la kushtukiza kwa ndani wakati ukiwa na nguvu za kutosha. Ila ukiwa poyoyo huwa ndo umejizika rasmi.
4.Ukiwa Kiongozi bora utaanza kujenga uongozi wa kujiamini na kuwa na wasaidizi wa haja bila kujali ni maadui au marafiki, kigezo ni kuwa wanaweza kutekeleza majukumu na malengo wanayowekewa na wanayojiwekea. Kiongozi wa aina hii haogopi changamoto za ndani wala nje kwani hataleta jambo lisilo na maslahi kwa jamii yake na hivyo upinzani atakaopata utakuwa ni katika kuboresha kile alichokianza. kwa hiyo kwa kuwa lengo lake huwa ni ustawi wa jamii yake atafurahi kila anapokutana na challenge itakayopelekea kuboresha hoja kwa maendeleo ya jamii.
Ndugu Lunyungu, Ukiangalia serikali yetu, matokeo yake kiutendaji na hasa ukijikita kwenye hii hali ya viongozi kuboronga hadharani( kama Waziri Nchimbi, IGP, DPP, Waziri wa elimu na Rais mwenyewe) utagundua kuwa serikali hii imejaa marafiki wa karibu wa rais, ukiongelea wizara na idara nyeti. Marafiki ambao wengine wamekuwa ni tatizo la wazi na kwa kuwa ni marafiki ameshindwa kuchukua hatua yoyote. Uteuzi wa wengine waliobaki umekuwa ni wa kujaza wenzetu zaidi. Eitha wale ambao walitusaidia kwa hali na mali na tumekosa nafasi ya kuwapa kama kulipa fadhila, ama kwa kuwa ni watu ambao tunajua hawajui kujitegemea kimawazo hivyo itakuwa rahisi kuwaendesha tunavyotaka.
Tatizo kubwa ni pale kiongozi anapokubali sapoti ya watu waovu na akakubali kulipa fadhila kwa watu hao! Matokeo yake ni kununuliwa na kukosa uamuzi, hasa inapokuja kutolea uamuzi jambo litakaloingilia maslahi ya hao jamaa. Na hilo pamoja na mengine ni kati ya matatizo ya kuwa na serikali ambazo ni zao la corruption.
Kutoka hapo nadhani unaweza kuona ni kwa nini mchungaji gani ameteuliwa kuwa nani, au ni kwa nini kina nani wamekuwa nani pamoja na kuwa hawawezi kazi na hawafanywi lolote na yeyote!